KERO Maafisa wa Kibaha Mji wanatumia Mgambo na Askari mwenye bastola kututisha ili watuondoe katika Makazi yetu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest



Sisi wakazi wa Matuga, Kibaha Vijijini tuna changamoto ya kusumbuliwa na Maafisa wa Halmashauri ya Kibaha Mji, wapo katika mchakato wa kutupora ardhi yetu kiasi cha kutumia Askari Polisi na Mgambo kutekeleza nia yao hiyo.

Hawa Watu wa Halmashauri ya Kibaha Mji huwa wanakuja kwenye makazi na mashamba yetu nyakati za usiku na wakati mwingine mchana kwa lengo la kupima viwanja.

Ikifika asubuhi wanawaleta watu na kuwagawia maeneo hayo huku wakiwa na Askari mwenye bastola, nimeambatanisha picha ya moja ya matukio ambayo inamuonesha jamaa mwenye T-shirt ya njano ambaye ndiye askari wanayemtumia hapo Halmashauri mara kadhaa.

Kibaha Viji.jpg

Maafisa wa Serikali wakiwa na Askari.
Kiba.jpg

Moja ya gari la Halmashauri ya Kibaha Mji lililofika Matuga likiwa na maafisa waliokuja kutoa vitisho kwetu.
Historia fupi hadi kufika hapo tulipofika
Sisi zaidi ya Wananchi 400 tulipata kadhia ya kusikitisha mnamo Februari 2, 2023, tulibomolewa makazi yetu chini ya usimamizi wa Askari na Maafisa wa Serikali pasipokuwa na taarifa yoyote ya awali juu ya ubomoaji huo.

Wabomoaji walifika tu siku hiyo wakaanza kuvunja na kututaka tutoe vitu ndani au tutoke, la sivyo wanavunja bila kujali nani yupo ndani.

Tukaenda kushtaki Mahakama Kuu Divisioni ya Ardhi, Februari 6, 2023 tukafungua kesi na Juni 30, 2023 hukumu ikatolea kuwa tumevunjiwa makazi yetu kinyume cha Sheria.

Kuanzia hukumu ilipotoka tumekuwa tukipata usumbufu kutoka kwa maafisa hao wanaotutishia usalama wetu.

Kuna wakati wanakuja na watu wanaodai wamebomolewa nyumba maeneo ya Mitamba na Loliondo (Kibaha), hivyo wanakuja kuwapatia maeneo huku kwetu kinguvu.

IMG_20240706_113437_060.jpg

Wananchi wa Matuga

Screenshot 2024-07-08 085432.jpg

photo_2024-07-09_08-33-45.jpg

Nyumba zilizobomolewa lakini baada ya muda Mahakama ikatoa hukumu kuwa ubomoaji ulifanyika kimakosa.


Mkuu wa Wilaya anasema tufunge nyumba zetu matairi tuzihamishe
Mkuu wa Mkoa anajua hili jambo lakini hajatuma msada wowote, Mkuu wa Wilaya naye aliwahi kutuambia kuwa kama tunaona hatuko salama tufunge matairi nyumba zetu tuhame.

Tunamuomba Waziri Jerry Silaa na Rais Samia Suluhu Hassan watusaidie, tumekuwa kama wakimbizi ndani ya Nchi yetu wenyewe.

Viongozi wa Kibaha Mji wajue kuwa hii Nchi ni ya ketu sote na inaongozwa na Sheria, wao hawapo juu ya Sheria. Haki tuliyoipata Mahakama Kuu inatakiwa kuheshimiwa.


Msingi wa nyumba uliobomolewa wakati wa bomoabomoa
Majibu ya Kibaha Mji ~ Halmashauri ya Kibaha Mji: Hatuhusiki na eneo la Matuga, walioenda kule ni Maafisa wetu walikuwa na mambo yao binafsi
 
Inaumiza sana raia kuonekana wakimbizi ndani ya Ardhi Yao kwa sababu Tu ya Tamaa ya watu wachache
 
Inaumiza sana raia kuonekana wakimbizi ndani ya Ardhi Yao kwa sababu Tu ya Tamaa ya watu wachache
Raia wenyewe wamekaa kinyonge sana. Kama nimemuelewa mleta mada anasema walishinda kesi mahakamani. Ubomoaji haukuwa halali. Bado wanakaa kinyonge???

Waache waendelee kuzubaa hivyo hivyo
 
Kuna mtu anajenga kwenye eneo langu ikifika muda wa kubomolewa atakuja kuleta malalamiko hapa Jf.

Baada ya kumuuliza nani amekuuzia alijibu alinunua kwenye kampuni ambayo ilipewa kazi ya kupima viwanja.

Mimi nilinunua kwa mwenye shamba na Hati miliki ninayo.

Hawa wanaofikiri kujenga nyumba kwenye maeneo ambayo walitapeliwa sio wa kuwaonea huruma.
 
Hakuna awamu iliyo fufuka changamoto ya ardhi kama ya huyu CHURA!! Na wapigaji wanajua KABISA kua CHURA ayuko upande w wananchi yuko upande wa matajiri na mafisadi.kazi mbona tunayo watanganyika.






KAZI ni kipimo cha UTU
 
Ujinga wetu ndio umetufikisha hapa humo humo utasikia mjumbe unatusaidiaje dah ya mjumbe wa shina la wakereketwa wa CCM ndio akusaidie ugoro wa Masai kabisa
 
Naona mkoa wa Pwani karibu na Dar kuna changamoto nyingi za ardhi. Nasikia kule Kiluvya upande wa Wilaya ya Kisarawe, panaitwa Tondoroni, na kwenyewe kuna mzozo mkubwa, kijiji kizima kimefutwa na nyumba kubomolewa huku kukiwa na shauri Mahakamani!
 
Sisi wakazi wa Matuga, Kibaha Vijijini tuna changamoto ya kusumbuliwa na Maafisa wa Halmashauri ya Kibaha Mji, wapo katika mchakato wa kutupora ardhi yetu kiasi cha kutumia Askari Polisi na Mgambo kutekeleza nia yao hiyo.

Hawa Watu wa Halmashauri ya Kibaha Mji huwa wanakuja kwenye makazi na mashamba yetu nyakati za usiku na wakati mwingine mchana kwa lengo la kupima viwanja.

Ikifika asubuhi wanawaleta watu na kuwagawia maeneo hayo huku wakiwa na Askari mwenye bastola, nimeambatanisha picha ya moja ya matukio ambayo inamuonesha jamaa mwenye T-shirt ya njano ambaye ndiye askari wanayemtumia hapo Halmashauri mara kadhaa.

View attachment 3036358
Maafisa wa Serikali wakiwa na Askari.
View attachment 3036359
Moja ya gari la Halmashauri ya Kibaha Mji lililofika Matuga likiwa na maafisa waliokuja kutoa vitisho kwetu.
Historia fupi hadi kufika hapo tulipofika
Sisi zaidi ya Wananchi 400 tulipata kadhia ya kusikitisha mnamo Februari 2, 2023, tulibomolewa makazi yetu chini ya usimamizi wa Askari na Maafisa wa Serikali pasipokuwa na taarifa yoyote ya awali juu ya ubomoaji huo.

Wabomoaji walifika tu siku hiyo wakaanza kuvunja na kututaka tutoe vitu ndani au tutoke, la sivyo wanavunja bila kujali nani yupo ndani.

Tukaenda kushtaki Mahakama Kuu Divisioni ya Ardhi, Februari 6, 2023 tukafungua kesi na Juni 30, 2023 hukumu ikatolea kuwa tumevunjiwa makazi yetu kinyume cha Sheria.

Kuanzia hukumu ilipotoka tumekuwa tukipata usumbufu kutoka kwa maafisa hao wanaotutishia usalama wetu.

Kuna wakati wanakuja na watu wanaodai wamebomolewa nyumba maeneo ya Mitamba na Loliondo (Kibaha), hivyo wanakuja kuwapatia maeneo huku kwetu kinguvu.

View attachment 3036360
Wananchi wa Matuga
View attachment 3036363
Moja ya nyumba iliyobomolewa lakini baada ya muda Mahakama ikatoa hukumu kuwa ubomoaji ulifanyika kimakosa.
Mkuu wa Wilaya anasema tufunge nyumba zetu matairi tuzihamishe
Mkuu wa Mkoa anajua hili jambo lakini hajatuma msada wowote, Mkuu wa Wilaya naye aliwahi kutuambia kuwa kama tunaona hatuko salama tufunge matairi nyumba zetu tuhame.

Tunamuomba Waziri Jerry Silaa na Rais Samia Suluhu Hassan watusaidie, tumekuwa kama wakimbizi ndani ya Nchi yetu wenyewe.

Viongozi wa Kibaha Mji wajue kuwa hii Nchi ni ya ketu sote na inaongozwa na Sheria, wao hawapo juu ya Sheria. Haki tuliyoipata Mahakama Kuu inatakiwa kuheshimiwa.

View attachment 3036365
Msingi wa nyumba uliyobomolewa wakati wa bomoabomoa
Njia pekee ni kutokukipigia CCM kura vinginevyo hamtoboi.mkiona mnabezwa mjue eneo hilo limeishauzwa na wamechukua chao.pazeni sauti ondosheni chama dharimu madarakani
 
Hivi kwanini wananchi wanakuwa wajinga kiasi hiki? Una nakala ya hukumu ya mahakama mpumbavu mmoja anakuja kukutisha kata panga ua, maana viongozi ndio watajitokeza kwakuwa wanafuatwa kuliliwa shida hawajali wanajali rushwa na kutetea kuchomwa picha ya mtu lakini kubomolewa nyumba za watu na kukiuka agizo la mahakama hakuna
 
kuna vitu vingine ata rais hajui wanajiongeza tu watu wenye tamaa
Ukiona mambo yanafanyika kwa kujirudia rudia basi ujue rais anajua kila kitu na ndiye anaruhusu. Mtaendelea kudanganywa mpaka lini? Poleni sana. Rais angekuwa ni mkali na hapendi manyanyaso kama haya hakuna mkuu wa mkoa au wilaya angethubutu kufanya ujinga kama huu.
 
Hivi kwanini wananchi wanakuwa wajinga kiasi hiki? Una nakala ya hukumu ya mahakama mpumbavu mmoja anakuja kukutisha kata panga ua, maana viongozi ndio watajitokeza kwakuwa wanafuatwa kuliliwa shida hawajali wanajali rushwa na kutetea kuchomwa picha ya mtu lakini kubomolewa nyumba za watu na kukiuka agizo la mahakama hakuna
Ule upole upole muda mwingine unagharimu
Wao wakitaka kitu toka kwako wanatumia nguvu, na nyie tumieni nguvu, suleni mipango hao walugaluga kila wakija hakikisheni hawarudi.
 
Ukiona mambo yanafanyika kwa kujirudia rudia basi ujue rais anajua kila kitu na ndiye anaruhusu. Mtaendelea kudanganywa mpaka lini? Poleni sana. Rais angekuwa ni mkali na hapendi manyanyaso kama haya hakuna mkuu wa mkoa au wilaya angethubutu kufanya ujinga kama huu.
Wanatakiwa kufanya doria wakiwakamata wauawe na magari yao yachomwe moto tumechoka sasa na huo upuuzi wa watendaji wa ccm.wtz tuache kulia lia tuchukue hatua bila ya kuwaonea huruma.kama wao wanavunja sheria kwa nini sisi tusivunje kama wao?
 
Back
Top Bottom