Libya walipewa maisha na Gaddafi ila wakarubuniwa na mabeberu, leo hii nchi imekosa mwelekeo

RASCO BOY

JF-Expert Member
Jul 29, 2018
428
485
June 31, 2007.. Raisi wa Zamani wa Libya Hayati Moummar Gadafi akiwa amesindikizwa na walinzi qake wa kike Waaminifu alihutubia ktk Mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) jijini Accra- Ghana huku akiwa amevalia Shati lake la khaki lenye picha za Wapiganaji na waasisi wa mataifa ya Afrika wenye Misimamo Mikali (Pan Africansts) kama Patrice Lumumba, Abdul Naser, julius kambarage Nyerere, kwame Nkurumah, Nelson Mandela, Sekou Toure, Thomas Sankara n.k.

Ndani ya mkutano Gaddafi akasema "Ndugu zangu Waafrika, tunapaswa Kuchagua Moja aidha kuiunganisha Afrika yetu au kuruhusu ife tunapaswa kuwa na muungano wa Mataifa ya kiafrika na kuunda (United States of Africa) tuna kila kitu ndani ya bara hili sasa ni vema tukaitimiza Ndoto hii kwa kuwa Wamoja tunaweza kupambana na Ulimwengu wa kileo"

Ndipo miaka kadhaa baadae Gaddafi ambaye amekuwa Mwenyekiti wa Afrika Mstaaff (AU) alivamiwa pale Libya.. akauawa pale pale Libya kwa kile kilichopambwa na Mabeberu huko Ulaya na Amerika kwa neno "DIKTETA" neno ambao Mara zote Mabeberu na Vibaraka wamekuwa wakilitumia dhidi ya Viongozi wote wa Mataifa Machanga wanaojaribu kujinasua ktk Mtego wa Ukoloni wa kiuchumi.

Kabla ya kuuawa kwa Gaddafi Libya ilikuwa na Fedha Nyingi kuliko idadi ya wananchi wake, Walikula na kusaza na hata Fedha nyingine zikaelekezwa kuufadhili Umoja wa Afrika (AU) posho zote za vikao na mishahara ilitoka Libya Mbali ya maendeleo Afrika Nzima, Mabilioni ya Dollar yakatumika kumaliza Ghasia za vita kule Niger na Mali, Baadhi ya misaada tuliyopata Tanzania kama Nchi ni pamoja na Kujengewe Msikiti pale Dodoma.

Leo Raia wa Libya wanasaga meno kwa Upumbavu wao, waliyakataa Maisha ya kifahari waliyoishi, Maisha ya kupewa Mishahara bila kufanya kazi kupewa mke na kulipiwa mahari na hata kupewa nyumba uanze Maisha....Leo wana Laana na Damu ya Gaddafi na Chozi la Gaddafi juu ya Ardhi yao ni wapi kwenye Raha? Sirte? Tripoli au Benghazi?... Vurugu tupu.

Tumpende na Tumuunge mkono Raisi wetu Magufuli hatatupa maisha bora na yenye furaha tumpe muda watanzania tuache kukariri Tumepata Raisi anayewarenga hao unaowaona kwenye picha katika shati la shujaa Gaddafi.....

Ni hayo Tu
FB_IMG_1548840129776.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umerogwa !!!? .... yaani unataka kumfananisha mtu aliye ligeuza jangwa kuwa bustani ya eden ... namtu ambaye nchi yake inakila natural resources lakini bado wananchi wake wanalia njaa na ukata mkubwa mifukoni mwao

Mtoa mada kwahiyo raia watanzania nao wanalipwa mishahara !? Wanapewa nyumba ya kuishi bure .. wanapewa pesa ya kuoa na serikali .....!? acha kumfananisha gadaffi na mambo ya kijinga mkuu

Nakushauria kimbilia haraka sana milembe kabla haujaanza kung'ata watu ......

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni maoni yako. Yanaheshimiwa. Ila tu ukipata wasaa wa kuonana naye, mwambie yafuatayo;

mtaani pesa imeadimika sana. Airudishe aisee! Pia awatendee haki watumishi wa umma. Stahiki zao mfano kupanda madaraja, kuongezewa mishahara, malimbikizo yao, hela zao za likizo, nk wapate/walipwe kwa wakati na zisigeuzwe kuwa ni fadhila hadi pale atakapojisikia!

Umwambie tunataka maendeleo ya vitu yaende sambamba na maendeleo ya watu!

Pia atambue kuna ongezeko kubwa la vijana wasio na ajira. Abuni miradi mbalimbali ya kupunguza hili bomu la ajira kwa vijana. Asisahau kuwa elimu yetu si rafiki kumfanya kila mhitimu aweze kujiajiri baada tu ya kuhitimu.
 
Umerogwa !!!? .... yaani unataka kumfananisha mtu aliye ligeuza jangwa kuwa bustani ya eden ... namtu ambaye nchi yake inakila natural resources lakini bado wananchi wake wanalia njaa na ukata mkubwa mifukoni mwao

Mtoa mada kwahiyo raia watanzania nao wanalipwa mishahara !? Wanapewa nyumba ya kuishi bure .. wanapewa pesa ya kuoa na serikali .....!? acha kumfananisha gadaffi na mambo ya kijinga mkuu

Nakushauria kimbilia haraka sana milembe kabla haujaanza kung'ata watu ......

Sent using Jamii Forums mobile app
Duuh kuna sehemu nimeandika kwa watanzania tunafanyiwa ayo acha kujilipua kama vimekaza pole ila nimeswma JPM anaweza kutufikisha uko nazani umenielewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuh kuna sehemu nimeandika kwa watanzania tunafanyiwa ayo acha kujilipua kama vimekaza pole ila nimeswma JPM anaweza kutufikisha uko nazani umenielewa

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kuota ndoto za mchana ...kwanza ngoja ni kwambie jambo .... katika maisha ni aibu kwa mtu aliyeelimika kuja kupewa msaada wakipesa na mtu ambaye hana elimu yoyote kabisaa ..... so sisi kama taifa ambalo tunakila kitu ambacho ni rasilimali amabazo zinalifanya taifa liwe na sifa ya utajiri lakini wananchi wake hawana kitu ... tulipaswa kuona haya aibu na kujisuta ...pindi tulipo kuwa tunapewa msaada na taifa kama libya ambalo lina tegemea kiinua mgongo kikuu kimoja tu ambacho ni mafuta ...... huyo unaye mtarajia kuwa atakufikisha huko unapopaota na yeye sialikuwa anashiriki bungeni katika kupitisha mikataba ambayo inawanufaisha mabeberu zaidi na kuliacha taifa likiwa na kilio

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha kuota ndoto za mchana ...kwanza ngoja ni kwambie jambo .... katika maisha ni aibu kwa mtu aliyeelimika kuja kupewa msaada wakipesa na mtu ambaye hana elimu yoyote kabisaa ..... so sisi kama taifa ambalo tunakila kitu ambacho ni rasilimali amabazo zinalifanya taifa liwe na sifa ya utajiri lakini wananchi wake hawana kitu ... tulipaswa kuona haya aibu na kujisuta ...pindi tulipo kuwa tunapewa msaada na taifa kama libya ambalo lina tegemea kiinua mgongo kikuu kimoja tu ambacho ni mafuta ...... huyo unaye mtarajia kuwa atakufikisha huko unapopaota na yeye sialikuwa anashiriki bungeni katika kupitisha mikataba ambayo inawanufaisha mabeberu zaidi na kuliacha taifa likiwa na kilio

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuwa mpore mafanikio uja taratibu Automatic tumpe muda Rais Magufuli atatufikisha uko tutakapo na kuwa juu zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi ni kweli kuwa tangu awamu ya tatu tangu iingie madarakani kwa miaka 3 watanzania Milioni 2 wametumbukia kwenye umaskini na mwaka 2006 hadi 2012 watanzania Milioni 1 walitolewa kwenye umaskini na utawala Wa JK? Au Jana sikumsikia vizuri Mh. Zitto akinukuu taarifa ya world bank mwenye bunge Jana.?Kama asingekuwa ananukuu WB sheria ya takwimu ingemshika shati. Kama taarifa hizo ni Sahihi basi anayeunga mkono utawala huu aunge na anayepinga utawla na apinge. Mimi ni muumini Wa namba(takwimu) siwezi kuwa shabiki Wa MTU, nadhani akili tumepewa ifanye Kazi ya kutathmini sio kushangilia au kuponda blindly. Ni kudunisha ubongo kama huutumii kuchukua msimamo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom