Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 129,749
- 249,609
Bado tungali tunaendelea na nyuzi za mwezi wa Mungu .
Dkt Bashiru Ally Kakurwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa ccm na wateule waliojiona wako karibu na Mamlaka ya Uteuzi , walijipa utukufu ambao hakuna kiongozi yoyote aliyewahi kujipa Tangu Nchi hii ipate uhuru wake .
Yaani ilifikia Mkuu wa Wilaya anamvimbia mtu yeyote akiwemo hata Mkuu wa Mkoa wake , kwa vile tu yeye yuko karibu na Rais , haifahamiki kama walikuwa wanatumwa na aliyewateua au la
Kwa Mfano ukiacha Bashiru Ally ambaye kiburi chake na ukosefu wake wa Adabu kwa Wazee akina Makamba na Kinana hakuna aliyeusahau , DC Sabaya , Ally Happy , Alexander Mnyeti pamoja na Paulo Makonda walikuwa Jamhuri huru ndani ya Jamhuri ya Tanzania .
Waliopiga U Turn na kurudi kwenye ubinadamu , japo nao walitaka kuingia kwenye Utukufu huo ni Amos Makalla , Chalamila na Mongela , hawa walianza kama wenzao lakini baadaye wakashikwa masikio .
Mara nyingi tumeonya na kufundisha sana hapa jf na kwingineko kuhusu hizi kazi za Kuteuliwa , kwamba hizi kazi ni Dhamana ya muda mfupi sana , ni vema tukazifanya kwa weledi maana hatujui kesho kutwa.
mwangalie Hapa Bashiru Ally baada ya kupigwa chini na kuteuliwa Mbunge wa viti maalum , Picha hii ikupe somo la kazi za kuteuliwa
Kiburi na dharau za wateule wa awamu ya 5 hakijawahi kuwepo kwenye nchi hii tangu iumbwe na Mungu , kila mteule mwenye kiburi cha madaraka ajaribu kumchukulia Salmin Amour , kama Mfano , Salmin alifikia kuitwa Komando kwa kejeli , matusi na dharau kwa wakubwa zake na wadogo , lakini mnafahu kilichomkuta leo ? hana ukomando wowote tena , hawezi kufika hata Kisiwandui , Kibanda maiti wala Mchamba wima , Utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana !
NITASEMA KWELI DAIMA FITNA KWANGU MWIKO
Dkt Bashiru Ally Kakurwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa ccm na wateule waliojiona wako karibu na Mamlaka ya Uteuzi , walijipa utukufu ambao hakuna kiongozi yoyote aliyewahi kujipa Tangu Nchi hii ipate uhuru wake .
Yaani ilifikia Mkuu wa Wilaya anamvimbia mtu yeyote akiwemo hata Mkuu wa Mkoa wake , kwa vile tu yeye yuko karibu na Rais , haifahamiki kama walikuwa wanatumwa na aliyewateua au la
Kwa Mfano ukiacha Bashiru Ally ambaye kiburi chake na ukosefu wake wa Adabu kwa Wazee akina Makamba na Kinana hakuna aliyeusahau , DC Sabaya , Ally Happy , Alexander Mnyeti pamoja na Paulo Makonda walikuwa Jamhuri huru ndani ya Jamhuri ya Tanzania .
Waliopiga U Turn na kurudi kwenye ubinadamu , japo nao walitaka kuingia kwenye Utukufu huo ni Amos Makalla , Chalamila na Mongela , hawa walianza kama wenzao lakini baadaye wakashikwa masikio .
Mara nyingi tumeonya na kufundisha sana hapa jf na kwingineko kuhusu hizi kazi za Kuteuliwa , kwamba hizi kazi ni Dhamana ya muda mfupi sana , ni vema tukazifanya kwa weledi maana hatujui kesho kutwa.
mwangalie Hapa Bashiru Ally baada ya kupigwa chini na kuteuliwa Mbunge wa viti maalum , Picha hii ikupe somo la kazi za kuteuliwa
Kiburi na dharau za wateule wa awamu ya 5 hakijawahi kuwepo kwenye nchi hii tangu iumbwe na Mungu , kila mteule mwenye kiburi cha madaraka ajaribu kumchukulia Salmin Amour , kama Mfano , Salmin alifikia kuitwa Komando kwa kejeli , matusi na dharau kwa wakubwa zake na wadogo , lakini mnafahu kilichomkuta leo ? hana ukomando wowote tena , hawezi kufika hata Kisiwandui , Kibanda maiti wala Mchamba wima , Utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana !
NITASEMA KWELI DAIMA FITNA KWANGU MWIKO