Kwako Lissu; Kwenye public speeches na Live interviews kuna hitaji Sanaa ya kuusema ukweli na kuepuka UKALI wakati usio sahihi ili kushawishi watu

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
28,188
67,755
Hamjamboni wote!

Unapokuwa Mwanasiasa watu ni sehemu ya mtaji katika Kazi yako hiyo. Watu kukukubali ni jambo kubwa na la muhimu kwenye siasa na utawala.
Pesa zinaweza zisiwe na umuhimu Sana mbele ya Kukukubalika kwa Watu.

Sasa kwenye Kukubalika hapa ndipo andiko langu lilipo.

Hapa kuna Makundi matatu:
1. Wanaokukubali Naturally vile ulivyo.

Kuna watu watakukubali vile ulivyo bila hata ya wewe kutumia nguvu yoyote. Yaani wao wamejikuta damu Yao ime-match kwako. Wanakupenda from nowhere. Hawa hata uongee utumbo,ufanye Jambo zuri au baya hawa wapo upande wako tuu.
Kundi Hili wanatoka upande wowote wanaweza kuwa sio wanachama wa chama chako na hata wasiwe na chama

2. Wanaokukubali kwa Sababu mna-share interest, falsafa, mitazamo n.k.
Kundi hili wao hujali zaidi maslahi Yao na kile kinachowaunganisha kama mnafanana falsafa, mitazamo n.k.
Kundi hili wengi huweza kuwa wanachama wenzako.
Lakini kundi hili sio la kudumu Sana kwa Sababu pale vitu vinavyowaunganisha vikiisha basi na ushawishi wako kwao unafikia Kikomo.

3. Wanaokukubali Mpaka uwashawishi.
Hawa ndio wapo wengi zaidi kuliko Makundi mengine.
Na hii ndio hufanya Kazi ya siasa kuwa
ngumu zaidi kuliko Kazi yoyote kwa Sababu ndipo utawala na uongozi wa watu ulipo

Kundi hili ndipo andiko letu litajikitia HAPO!

Ikiwa siasa inahitaji watu hii itamaanisha uwe na uwezo wa kulinda watu wanaokukubali, na kutumia mbinu na mikakati kushawishi wale ambao hawakukubali yaani wale ambao hawakoupande wako
Na hiyo ndio inanifanya niione Siasa ni kama Mchezo wa Draft.

Kwa wale Wachezaji wa Draft mabingwa kama Taikon Master mtakubaliana na Mimi Kuwa Mchezo wa Draft ili ushinde itakupasa uhakikishe unampunja mwenzako kete zake kusudi wewe uwe na kete nyingi kuliko za mshindani wako.

Kanuni ya Pili, ni kuhakikisha unashika Njia kuu za Mchezo ili kumzuia mshindani wako ashindwe kufanya movements zenye madhara kwako. Na Kanuni ya mwisho nikulinda kete zako zisikae katika Hatari ya kuliwa na mshindani wako bila faida. Kwamba ikitokea umeruhusu kete yako kuliwa basi uliandaa Kupata faida kubwa zaidi kupitia Kete hiyo.

Kanuni ya mwisho ni kutega mitego ambayo sio rahisi mshindani wako kuiona kirahisi. Na Jambo hili linawezekana ikiwa utaweza kuweka mitego ya bosheni kumpoteza maboya mshindani wako. Huo ndio Mchezo wa Draft kwa Sisi mabingwa. Unafanana kwa Kiasi kikubwa na michezo ya Siasa.

Kete ni WATU.
Huwezi kushinda kwenye siasa kama huna kete muhimu na hujazipangilia na kuziweka katika Njia sahihi kumiliki Mchezo.
Unahitaji kuwashawishi watu Kwa namna yoyote Ile wawe upande wako.

Kwenye Draft kuna kete zinazoingizwa King. Kete hizo huwa na uwezo wa kuzunguka sehemu yoyote na Kula kete nyingi zaidi
Kwenye siasa lazima utambue watu wenye ushawishi kwa Watu wengine hawa ndio kings wa Mchezo wako ambao ukiwatumia hao unajua nyuma Yao wapo wafuasi wengi ambao watakuwa upande wako.

Sitaki Kuchochora na kusema mambo mengi

Tundu Lisu ni kweli anaushawishi. Lakini ushawishi wake upo kundi la watu wenye mitazamo, falsafa na interests zinazofanana na wale wanaomkubali naturally.
Hii Inamaanisha kuna kundi kubwa la watu ambao wanahitaji awashawishi ili wawe upande wake. Na kwa bahati mbaya kundi Hilo ndilo hubeba watu wengi zaidi kuliko Makundi mengine.

Tundu Lisu pamoja na kwamba anasema Ukweli lakini linapokuja suala la ushawishi kumfanya mtu ambaye hakukubali abadili mtazamo wake juu yako itampasa aongee Ukweli wenye Sanaa ndani yake. Asiongee Ukweli Mkavu Mkavu kama kina Siye Kina Taikon ambao Sisi kwa sasa hatuhitaji kumshawishi mtu yeyote awe upande wetu. Sisi tuna Uhuru wa kuzungumza ukweli wowote kwa namna yoyote.

Ukweli wowote kwa namna yoyote husemwa na Wanaharakati.

Lisu lazima awe na akili ya kujuwa wakati gani awe mwanaharakati na wakati gani awe Mwanasiasa ili Kupata nguvu zaidi.

Ukweli Mkavu Mkavu HAUTAKIWI kwa Watu ambao wapo kinyume na wewe alafu Muda huohuo unawahitaji wawe upande wako. Mambo hayaendi hivyo.

Tundu Lisu anapotoa hotuba zake hujikuta akijisahau na kushindwa kujua ni wakati gani awe Mkali.
Ukali kwenye ushawishi haupogo.
Huwezi mshawishi mtu ambaye yupo upande mwingine kwa kumuonyeshea Ukali.

Ukali wakati usiosahihi unabeba tafsiri ya Udikteta Uchwara.

Watu wasipokuelewa haina maana wao ni wabaya au wanakosea. Unahitaji utumie Mbinu za akili kuwashawishi wakuelewe.

Ukiwa kwenye interviews za kisiasa ni lazima uhakikishe Ukali wako hata kama upo unauhifadhi kwa wakati sahihi.
Ukali mbele za watu huweza KUBEBA tafsiri nyingi hasa kwa wale wasiokukubali hata kama ukali wako unahoja muhimu.
Wengi huweza kuutafsiri kama Ujuaji, kujiona, kiburi au jeuri.

Kufikia hapa Taikon Master Sina la Ziada

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
 
Naunga mkono hoja ila yule Balile alistahili ile Nonsense
Popularity ya Trump ni kutokana na anavowajibu watu namna wanavyostahili kujibiwa.

Hivyo Tundu Lissu hakukosea kumjibu vile Balile maana alistahili kujibiwe vile.

Kwenye mambo serious ya kulibadilisha hili Taifa ambalo ni kama limeshalufa hatuhitaji maneno matamu na busara za kijinga.

Tuwe serious kweli maana CCM walishakataa demokrasia.
 
AhAaaa stereo type

Wananchi wanataka kusikia kile kinachoendana na akili yao na hisia Kama "Rais wa wanyonge n.k"

Wananchi wanatofautiana uelewa, mitazamo,interest.

Kwa mwanasiasa ambaye bado hajawa kiongozi na anahitaji Kupata ushawishi Mkubwa itampasa awe na tahadhari kubwa katika namna ya kuusema UKWELI

Ni tofauti na akishakuwa kiongozi

Ukweli Mkavu Mkavu hauwezi kukupa Matokeo katika ushawishi kwa Watu wengi.
Hata kwenye kutongoza Wanawake.

Ukweli wakati wa ushawishi unahitaji uwe na sanaa. Yaani usibadili ukweli lakini jaribu kuusema ukweli kwa namna ya kumfanya anayekusikiliza kuvutiwa na ukweli unaousema

Lakini sio kusema ukweli usiovutia ilhali unahitaji kuungwa mkono
 
Naunga mkono hoja ila yule Balile alistahili ile Nonsense
KWA MWANASIASA NGULI MWENYE HAIBA KAMA ALIYOISHAURI MLETA MADA, KWANGU MIMI BALILE ALIKUWA NDIO MTAMU SASA. ALIKUWA ANAMCHOKONOA ILI ATOE FACTS NA USHAWISHI KWA UPOLE, MIFANO, HADITHI, HISTORIA ILI WANAOTAGETIWA WAPATE KUSHAWISHIKA.
LKN KILA ALIPOKUWA AKIULIZWA SWALI NA BALILE UNAONA ANAGEUZA GEUZA SHINGO KUASHIRIA HASIRA. KILA MARA ALIKUWA AKIMLAANI BALILE KWA KUMWITA "NYIE" akimaanisha BALILE ni CCM.

Kwa mwanasiasa mtulivu Jana wahariri wangeshawishika sana.
Watamkumbuka DJ very soon. Na makovu ya baada ya uchaguzi wa CDM kwa mtindo huu wa mapovu hayatakuja kupona. Mimi Niko paleee
 
Hamjamboni wote!

Unapokuwa Mwanasiasa watu ni sehemu ya mtaji katika Kazi yako hiyo. Watu kukukubali ni jambo kubwa na la muhimu kwenye siasa na utawala.
Pesa zinaweza zisiwe na umuhimu Sana mbele ya Kukukubalika kwa Watu.

Sasa kwenye Kukubalika hapa ndipo andiko langu lilipo.

Hapa kuna Makundi matatu:
1. Wanaokukubali Naturally vile ulivyo.

Kuna watu watakukubali vile ulivyo bila hata ya wewe kutumia nguvu yoyote. Yaani wao wamejikuta damu Yao ime-match kwako. Wanakupenda from nowhere. Hawa hata uongee utumbo,ufanye Jambo zuri au baya hawa wapo upande wako tuu.
Kundi Hili wanatoka upande wowote wanaweza kuwa sio wanachama wa chama chako na hata wasiwe na chama

2. Wanaokukubali kwa Sababu mna-share interest, falsafa, mitazamo n.k.
Kundi hili wao hujali zaidi maslahi Yao na kile kinachowaunganisha kama mnafanana falsafa, mitazamo n.k.
Kundi hili wengi huweza kuwa wanachama wenzako.
Lakini kundi hili sio la kudumu Sana kwa Sababu pale vitu vinavyowaunganisha vikiisha basi na ushawishi wako kwao unafikia Kikomo.

3. Wanaokukubali Mpaka uwashawishi.
Hawa ndio wapo wengi zaidi kuliko Makundi mengine.
Na hii ndio hufanya Kazi ya siasa kuwa
ngumu zaidi kuliko Kazi yoyote kwa Sababu ndipo utawala na uongozi wa watu ulipo

Kundi hili ndipo andiko letu litajikitia HAPO!

Ikiwa siasa inahitaji watu hii itamaanisha uwe na uwezo wa kulinda watu wanaokukubali, na kutumia mbinu na mikakati kushawishi wale ambao hawakukubali yaani wale ambao hawakoupande wako
Na hiyo ndio inanifanya niione Siasa ni kama Mchezo wa Draft.

Kwa wale Wachezaji wa Draft mabingwa kama Taikon Master mtakubaliana na Mimi Kuwa Mchezo wa Draft ili ushinde itakupasa uhakikishe unampunja mwenzako kete zake kusudi wewe uwe na kete nyingi kuliko za mshindani wako.

Kanuni ya Pili, ni kuhakikisha unashika Njia kuu za Mchezo ili kumzuia mshindani wako ashindwe kufanya movements zenye madhara kwako. Na Kanuni ya mwisho nikulinda kete zako zisikae katika Hatari ya kuliwa na mshindani wako bila faida. Kwamba ikitokea umeruhusu kete yako kuliwa basi uliandaa Kupata faida kubwa zaidi kupitia Kete hiyo.

Kanuni ya mwisho ni kutega mitego ambayo sio rahisi mshindani wako kuiona kirahisi. Na Jambo hili linawezekana ikiwa utaweza kuweka mitego ya bosheni kumpoteza maboya mshindani wako. Huo ndio Mchezo wa Draft kwa Sisi mabingwa. Unafanana kwa Kiasi kikubwa na michezo ya Siasa.

Kete ni WATU.
Huwezi kushinda kwenye siasa kama huna kete muhimu na hujazipangilia na kuziweka katika Njia sahihi kumiliki Mchezo.
Unahitaji kuwashawishi watu Kwa namna yoyote Ile wawe upande wako.

Kwenye Draft kuna kete zinazoingizwa King. Kete hizo huwa na uwezo wa kuzunguka sehemu yoyote na Kula kete nyingi zaidi
Kwenye siasa lazima utambue watu wenye ushawishi kwa Watu wengine hawa ndio kings wa Mchezo wako ambao ukiwatumia hao unajua nyuma Yao wapo wafuasi wengi ambao watakuwa upande wako.

Sitaki Kuchochora na kusema mambo mengi

Tundu Lisu ni kweli anaushawishi. Lakini ushawishi wake upo kundi la watu wenye mitazamo, falsafa na interests zinazofanana na wale wanaomkubali naturally.
Hii Inamaanisha kuna kundi kubwa la watu ambao wanahitaji awashawishi ili wawe upande wake. Na kwa bahati mbaya kundi Hilo ndilo hubeba watu wengi zaidi kuliko Makundi mengine.

Tundu Lisu pamoja na kwamba anasema Ukweli lakini linapokuja suala la ushawishi kumfanya mtu ambaye hakukubali abadili mtazamo wake juu yako itampasa aongee Ukweli wenye Sanaa ndani yake. Asiongee Ukweli Mkavu Mkavu kama kina Siye Kina Taikon ambao Sisi kwa sasa hatuhitaji kumshawishi mtu yeyote awe upande wetu. Sisi tuna Uhuru wa kuzungumza ukweli wowote kwa namna yoyote.

Ukweli wowote kwa namna yoyote husemwa na Wanaharakati.

Lisu lazima awe na akili ya kujuwa wakati gani awe mwanaharakati na wakati gani awe Mwanasiasa ili Kupata nguvu zaidi.

Ukweli Mkavu Mkavu HAUTAKIWI kwa Watu ambao wapo kinyume na wewe alafu Muda huohuo unawahitaji wawe upande wako. Mambo hayaendi hivyo.

Tundu Lisu anapotoa hotuba zake hujikuta akijisahau na kushindwa kujua ni wakati gani awe Mkali.
Ukali kwenye ushawishi haupogo.
Huwezi mshawishi mtu ambaye yupo upande mwingine kwa kumuonyeshea Ukali.

Ukali wakati usiosahihi unabeba tafsiri ya Udikteta Uchwara.

Watu wasipokuelewa haina maana wao ni wabaya au wanakosea. Unahitaji utumie Mbinu za akili kuwashawishi wakuelewe.

Ukiwa kwenye interviews za kisiasa ni lazima uhakikishe Ukali wako hata kama upo unauhifadhi kwa wakati sahihi.
Ukali mbele za watu huweza KUBEBA tafsiri nyingi hasa kwa wale wasiokukubali hata kama ukali wako unahoja muhimu.
Wengi huweza kuutafsiri kama Ujuaji, kujiona, kiburi au jeuri.

Kufikia hapa Taikon Master Sina la Ziada

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
Nafikiri pia tunatakiwa kulitazama suala hili la uanaharakati kwa jicho lingine. Serikali hushawishiwa kwa hoja zilizonyooka na maoni ambayo yakichekechwa huonekana kuleta manufaa. Mbinu ya kutishia serikali bila kuwa na sababu au hoja za msingi haiwezi kuwaleta wahusika mezani. Lengo za harakati inatakiwa kuchochea mabadiliko, zaidi kwa njia ambazo hazibomoi.
 
Hamjamboni wote!

Unapokuwa Mwanasiasa watu ni sehemu ya mtaji katika Kazi yako hiyo. Watu kukukubali ni jambo kubwa na la muhimu kwenye siasa na utawala.
Pesa zinaweza zisiwe na umuhimu Sana mbele ya Kukukubalika kwa Watu.

Sasa kwenye Kukubalika hapa ndipo andiko langu lilipo.

Hapa kuna Makundi matatu:
1. Wanaokukubali Naturally vile ulivyo.

Kuna watu watakukubali vile ulivyo bila hata ya wewe kutumia nguvu yoyote. Yaani wao wamejikuta damu Yao ime-match kwako. Wanakupenda from nowhere. Hawa hata uongee utumbo,ufanye Jambo zuri au baya hawa wapo upande wako tuu.
Kundi Hili wanatoka upande wowote wanaweza kuwa sio wanachama wa chama chako na hata wasiwe na chama

2. Wanaokukubali kwa Sababu mna-share interest, falsafa, mitazamo n.k.
Kundi hili wao hujali zaidi maslahi Yao na kile kinachowaunganisha kama mnafanana falsafa, mitazamo n.k.
Kundi hili wengi huweza kuwa wanachama wenzako.
Lakini kundi hili sio la kudumu Sana kwa Sababu pale vitu vinavyowaunganisha vikiisha basi na ushawishi wako kwao unafikia Kikomo.

3. Wanaokukubali Mpaka uwashawishi.
Hawa ndio wapo wengi zaidi kuliko Makundi mengine.
Na hii ndio hufanya Kazi ya siasa kuwa
ngumu zaidi kuliko Kazi yoyote kwa Sababu ndipo utawala na uongozi wa watu ulipo

Kundi hili ndipo andiko letu litajikitia HAPO!

Ikiwa siasa inahitaji watu hii itamaanisha uwe na uwezo wa kulinda watu wanaokukubali, na kutumia mbinu na mikakati kushawishi wale ambao hawakukubali yaani wale ambao hawakoupande wako
Na hiyo ndio inanifanya niione Siasa ni kama Mchezo wa Draft.

Kwa wale Wachezaji wa Draft mabingwa kama Taikon Master mtakubaliana na Mimi Kuwa Mchezo wa Draft ili ushinde itakupasa uhakikishe unampunja mwenzako kete zake kusudi wewe uwe na kete nyingi kuliko za mshindani wako.

Kanuni ya Pili, ni kuhakikisha unashika Njia kuu za Mchezo ili kumzuia mshindani wako ashindwe kufanya movements zenye madhara kwako. Na Kanuni ya mwisho nikulinda kete zako zisikae katika Hatari ya kuliwa na mshindani wako bila faida. Kwamba ikitokea umeruhusu kete yako kuliwa basi uliandaa Kupata faida kubwa zaidi kupitia Kete hiyo.

Kanuni ya mwisho ni kutega mitego ambayo sio rahisi mshindani wako kuiona kirahisi. Na Jambo hili linawezekana ikiwa utaweza kuweka mitego ya bosheni kumpoteza maboya mshindani wako. Huo ndio Mchezo wa Draft kwa Sisi mabingwa. Unafanana kwa Kiasi kikubwa na michezo ya Siasa.

Kete ni WATU.
Huwezi kushinda kwenye siasa kama huna kete muhimu na hujazipangilia na kuziweka katika Njia sahihi kumiliki Mchezo.
Unahitaji kuwashawishi watu Kwa namna yoyote Ile wawe upande wako.

Kwenye Draft kuna kete zinazoingizwa King. Kete hizo huwa na uwezo wa kuzunguka sehemu yoyote na Kula kete nyingi zaidi
Kwenye siasa lazima utambue watu wenye ushawishi kwa Watu wengine hawa ndio kings wa Mchezo wako ambao ukiwatumia hao unajua nyuma Yao wapo wafuasi wengi ambao watakuwa upande wako.

Sitaki Kuchochora na kusema mambo mengi

Tundu Lisu ni kweli anaushawishi. Lakini ushawishi wake upo kundi la watu wenye mitazamo, falsafa na interests zinazofanana na wale wanaomkubali naturally.
Hii Inamaanisha kuna kundi kubwa la watu ambao wanahitaji awashawishi ili wawe upande wake. Na kwa bahati mbaya kundi Hilo ndilo hubeba watu wengi zaidi kuliko Makundi mengine.

Tundu Lisu pamoja na kwamba anasema Ukweli lakini linapokuja suala la ushawishi kumfanya mtu ambaye hakukubali abadili mtazamo wake juu yako itampasa aongee Ukweli wenye Sanaa ndani yake. Asiongee Ukweli Mkavu Mkavu kama kina Siye Kina Taikon ambao Sisi kwa sasa hatuhitaji kumshawishi mtu yeyote awe upande wetu. Sisi tuna Uhuru wa kuzungumza ukweli wowote kwa namna yoyote.

Ukweli wowote kwa namna yoyote husemwa na Wanaharakati.

Lisu lazima awe na akili ya kujuwa wakati gani awe mwanaharakati na wakati gani awe Mwanasiasa ili Kupata nguvu zaidi.

Ukweli Mkavu Mkavu HAUTAKIWI kwa Watu ambao wapo kinyume na wewe alafu Muda huohuo unawahitaji wawe upande wako. Mambo hayaendi hivyo.

Tundu Lisu anapotoa hotuba zake hujikuta akijisahau na kushindwa kujua ni wakati gani awe Mkali.
Ukali kwenye ushawishi haupogo.
Huwezi mshawishi mtu ambaye yupo upande mwingine kwa kumuonyeshea Ukali.

Ukali wakati usiosahihi unabeba tafsiri ya Udikteta Uchwara.

Watu wasipokuelewa haina maana wao ni wabaya au wanakosea. Unahitaji utumie Mbinu za akili kuwashawishi wakuelewe.

Ukiwa kwenye interviews za kisiasa ni lazima uhakikishe Ukali wako hata kama upo unauhifadhi kwa wakati sahihi.
Ukali mbele za watu huweza KUBEBA tafsiri nyingi hasa kwa wale wasiokukubali hata kama ukali wako unahoja muhimu.
Wengi huweza kuutafsiri kama Ujuaji, kujiona, kiburi au jeuri.

Kufikia hapa Taikon Master Sina la Ziada

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
Janabi anasema ukimsikilza Jamaa yenu huyo unajua kabisa kwamba eti ni mgonjwa wa akili 😆😆
 
Nafikiri pia tunatakiwa kulitazama suala hili la uanaharakati kwa jicho lingine. Serikali hushawishiwa kwa hoja zilizonyooka na maoni ambayo yakichekechwa huonekana kuleta manufaa. Mbinu ya kutishia serikali bila kuwa na sababu au hoja za msingi haiwezi kuwaleta wahusika mezani. Lengo za harakati inatakiwa kuchochea mabadiliko, zaidi kwa njia ambazo hazibomoi.

..mapendekezo ya tume huru ni ya miaka zaidi ya 30 sasa na serikali / CCM wamegoma kuyatekeleza.

..mambo anayoyasema Tundu Lissu hajayatoa kichwani, bali anafuata maoni na rai za Tume za Jaji Mkuu Francis Nyalali, Jaji Robert Kisanga, Jaji Mark Bomani, Jaji Joseph Warioba, na Prof.Mukandala.

..suala sio lugha ya Tundu Lissu, wazee niliowataja na Tume zao walikuwa na lugha za unyenyekevu mnazozipigia upata. Viongozi wa upinzani kama Freeman Mbowe, Maalim Seif, nao walikuwa na lugha za upole, na unyenyekevu, lakini bado CCM imekataa kuunda Tume ya uchaguzi itakayotenda haki mpaka hii leo.

..Suala lingine ni kwamba watu wamepoteza maisha ktk vurugu za kulazimisha ushindi wa CCM. Kama chama CCM walipaswa kushtushwa na kujutia hali hiyo na kufanya mageuzi.
 
Hamjamboni wote!

Unapokuwa Mwanasiasa watu ni sehemu ya mtaji katika Kazi yako hiyo. Watu kukukubali ni jambo kubwa na la muhimu kwenye siasa na utawala.
Pesa zinaweza zisiwe na umuhimu Sana mbele ya Kukukubalika kwa Watu.

Sasa kwenye Kukubalika hapa ndipo andiko langu lilipo.

Hapa kuna Makundi matatu:
1. Wanaokukubali Naturally vile ulivyo.

Kuna watu watakukubali vile ulivyo bila hata ya wewe kutumia nguvu yoyote. Yaani wao wamejikuta damu Yao ime-match kwako. Wanakupenda from nowhere. Hawa hata uongee utumbo,ufanye Jambo zuri au baya hawa wapo upande wako tuu.
Kundi Hili wanatoka upande wowote wanaweza kuwa sio wanachama wa chama chako na hata wasiwe na chama

2. Wanaokukubali kwa Sababu mna-share interest, falsafa, mitazamo n.k.
Kundi hili wao hujali zaidi maslahi Yao na kile kinachowaunganisha kama mnafanana falsafa, mitazamo n.k.
Kundi hili wengi huweza kuwa wanachama wenzako.
Lakini kundi hili sio la kudumu Sana kwa Sababu pale vitu vinavyowaunganisha vikiisha basi na ushawishi wako kwao unafikia Kikomo.

3. Wanaokukubali Mpaka uwashawishi.
Hawa ndio wapo wengi zaidi kuliko Makundi mengine.
Na hii ndio hufanya Kazi ya siasa kuwa
ngumu zaidi kuliko Kazi yoyote kwa Sababu ndipo utawala na uongozi wa watu ulipo

Kundi hili ndipo andiko letu litajikitia HAPO!

Ikiwa siasa inahitaji watu hii itamaanisha uwe na uwezo wa kulinda watu wanaokukubali, na kutumia mbinu na mikakati kushawishi wale ambao hawakukubali yaani wale ambao hawakoupande wako
Na hiyo ndio inanifanya niione Siasa ni kama Mchezo wa Draft.

Kwa wale Wachezaji wa Draft mabingwa kama Taikon Master mtakubaliana na Mimi Kuwa Mchezo wa Draft ili ushinde itakupasa uhakikishe unampunja mwenzako kete zake kusudi wewe uwe na kete nyingi kuliko za mshindani wako.

Kanuni ya Pili, ni kuhakikisha unashika Njia kuu za Mchezo ili kumzuia mshindani wako ashindwe kufanya movements zenye madhara kwako. Na Kanuni ya mwisho nikulinda kete zako zisikae katika Hatari ya kuliwa na mshindani wako bila faida. Kwamba ikitokea umeruhusu kete yako kuliwa basi uliandaa Kupata faida kubwa zaidi kupitia Kete hiyo.

Kanuni ya mwisho ni kutega mitego ambayo sio rahisi mshindani wako kuiona kirahisi. Na Jambo hili linawezekana ikiwa utaweza kuweka mitego ya bosheni kumpoteza maboya mshindani wako. Huo ndio Mchezo wa Draft kwa Sisi mabingwa. Unafanana kwa Kiasi kikubwa na michezo ya Siasa.

Kete ni WATU.
Huwezi kushinda kwenye siasa kama huna kete muhimu na hujazipangilia na kuziweka katika Njia sahihi kumiliki Mchezo.
Unahitaji kuwashawishi watu Kwa namna yoyote Ile wawe upande wako.

Kwenye Draft kuna kete zinazoingizwa King. Kete hizo huwa na uwezo wa kuzunguka sehemu yoyote na Kula kete nyingi zaidi
Kwenye siasa lazima utambue watu wenye ushawishi kwa Watu wengine hawa ndio kings wa Mchezo wako ambao ukiwatumia hao unajua nyuma Yao wapo wafuasi wengi ambao watakuwa upande wako.

Sitaki Kuchochora na kusema mambo mengi

Tundu Lisu ni kweli anaushawishi. Lakini ushawishi wake upo kundi la watu wenye mitazamo, falsafa na interests zinazofanana na wale wanaomkubali naturally.
Hii Inamaanisha kuna kundi kubwa la watu ambao wanahitaji awashawishi ili wawe upande wake. Na kwa bahati mbaya kundi Hilo ndilo hubeba watu wengi zaidi kuliko Makundi mengine.

Tundu Lisu pamoja na kwamba anasema Ukweli lakini linapokuja suala la ushawishi kumfanya mtu ambaye hakukubali abadili mtazamo wake juu yako itampasa aongee Ukweli wenye Sanaa ndani yake. Asiongee Ukweli Mkavu Mkavu kama kina Siye Kina Taikon ambao Sisi kwa sasa hatuhitaji kumshawishi mtu yeyote awe upande wetu. Sisi tuna Uhuru wa kuzungumza ukweli wowote kwa namna yoyote.

Ukweli wowote kwa namna yoyote husemwa na Wanaharakati.

Lisu lazima awe na akili ya kujuwa wakati gani awe mwanaharakati na wakati gani awe Mwanasiasa ili Kupata nguvu zaidi.

Ukweli Mkavu Mkavu HAUTAKIWI kwa Watu ambao wapo kinyume na wewe alafu Muda huohuo unawahitaji wawe upande wako. Mambo hayaendi hivyo.

Tundu Lisu anapotoa hotuba zake hujikuta akijisahau na kushindwa kujua ni wakati gani awe Mkali.
Ukali kwenye ushawishi haupogo.
Huwezi mshawishi mtu ambaye yupo upande mwingine kwa kumuonyeshea Ukali.

Ukali wakati usiosahihi unabeba tafsiri ya Udikteta Uchwara.

Watu wasipokuelewa haina maana wao ni wabaya au wanakosea. Unahitaji utumie Mbinu za akili kuwashawishi wakuelewe.

Ukiwa kwenye interviews za kisiasa ni lazima uhakikishe Ukali wako hata kama upo unauhifadhi kwa wakati sahihi.
Ukali mbele za watu huweza KUBEBA tafsiri nyingi hasa kwa wale wasiokukubali hata kama ukali wako unahoja muhimu.
Wengi huweza kuutafsiri kama Ujuaji, kujiona, kiburi au jeuri.

Kufikia hapa Taikon Master Sina la Ziada

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam

..Nadhani unatumia kalamu yako vibaya.

..Badala ya kuwafichua na kuwalaani CCM wanaoumiza wananchi wakati wa uchaguzi unamlaumu na kumzodoa Lissu mtetezi wa haki.

..Waandishi wa aina yako mna mchango mkubwa sana katika kudumisha dhuluma ktk uchaguzi na mifumo yetu ya kidemokrasia.
 
Nafikiri pia tunatakiwa kulitazama suala hili la uanaharakati kwa jicho lingine. Serikali hushawishiwa kwa hoja zilizonyooka na maoni ambayo yakichekechwa huonekana kuleta manufaa. Mbinu ya kutishia serikali bila kuwa na sababu au hoja za msingi haiwezi kuwaleta wahusika mezani. Lengo za harakati inatakiwa kuchochea mabadiliko, zaidi kwa njia ambazo hazibomoi.
Ni mara ngapi hizo hoja zilizonyooka zinaletwa bila hata vitisho na bado hakuna mabadaliko. Zile taarifa za tume za kina Jaji Kisanga, Warioba nk zina vitisho gani? Mbona hazijaleta mabadiliko yaliyopendekezwa?
 
..Nadhani unatumia kalamu yako vibaya.

..Badala ya kuwafichua na kuwalaani CCM wanaoumiza wananchi wakati wa uchaguzi unamlaumu na kumzodoa Lissu mtetezi wa haki.

..Waandishi wa aina yako mna mchango mkubwa sana katika kudumisha dhuluma ktk uchaguzi na mifumo yetu ya kidemokrasia.

Aiseeh!
Kwamba Mimi niitetee dhulma?

Mimi nimemshauri Lisu namna ya kufika huko anakotaka kufika. Hiyo ni juu yake kuelewa kwa namna yako au Kwa namna atakayoona yeye
 
Back
Top Bottom