Kwa Wapenzi wa Teknolojia: Mwaka 2025 utakua mwaka wa AR na Smart-glasses.

Mad Max

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
26,908
77,640
Smart-glasses na Argumented Reality glasses zimeanza kitambo ila bado hazijafika "peak" ambayo mtu atatamani kununua.

images (6).jpeg

Tokea enzi Google alileta Smart-glasses zake 2013 akawa anawauzia developers tu kwa $1,300 ila hazikufika sokoni nadhani project ikifeli.
images (9).jpeg

(Google Smart-glasses ya 2013)

Wengi wakajaribu ila Snapchat nao wakaleta miwani yao ambayo inafaa waliokua addicted na Snapchat ila naona nayo haijabamba sana kwasababu ya limitations.
images (10).jpeg

(Smart-glasses za Snapchat)

Apple na Visio Pro zao za $3,500 wachache sana wataweza kumudu ndio maana wenyewe kama wame abandon project wanatafuta cheaper alternative.
images (8).jpeg

(Apple Vision Pro, nzuri sana sema bei ghali hafu kubwa saaaana)

Hadi sasa, Meta ndio wana Smart-glasses nzuri ambazo ni reasonable na bei rafiki kununua. Ray-Ban by Meta kwa $400 ila nayo challenge kubwa ina integrate vizuri zaidi na Meta products (FB, IG, WA, nk).
images (11).jpeg

Meta's Ray-Ban Smart-glasses hizi cheap hafu practical sana.

Sasa kwenye maonyesho ya CES 2025 (Consumer Electronics Show) tumeona wengi sana wameonyesha products za Smart-glasses.
07aSSe6bKd3lxfsF8h39IwD-1.fit_lim.size_850x490.v1736380203.jpg
07aSSe6bKd3lxfsF8h39IwD-3.fit_lim.size_963x.jpg
07aSSe6bKd3lxfsF8h39IwD-5.fit_lim.size_963x.jpg
07aSSe6bKd3lxfsF8h39IwD-4.fit_lim.size_963x.jpg

(Hizo juu products za Smart-glasses zilizoonyeshwa CES 2025 kutoka makampuni mbalimbali)

Imagine kuvaa miwani inakupa direction, unapata meseji na notifications bila kutoa simu, unapokea simu, unaongea na Mchina na zinakupa real-time translation pale pale nk.
images (7).jpeg

Kwa bei za $300-500 tutapata products nzuri sana.

Sema hadi tech giants Samsung, Apple, Xiaomi, nk wakiingia officially kwenye hii trend ndio zitabamba.

Google wanasemekana wanakuja upya na Project Astra kwaajili ya Smart-glasses ila bado ni rumors.
 
Nasubiria mchina, najua yupo jikoni anapika Smart Glass zake. Tunamsubiria Huawei, smart glass za tekino na infinix
 
Hii tech ikiwa Worldwide itabamba sn nakumbuka mwaka 2015 nilimuona mchina mmoja pale kariakoo alikuwa na Google Glass ktk kutoa ushamba watu walimuomba kutest tech hiyo nikiwemo mimi.. ilikuwa Device nzuri nashangaa Google walifeli vipi kuisambaza kwa wingi duniani !
 
Back
Top Bottom