SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,683
- 12,709
Nadhani muda umefika tufikishane kwenye vyombo vya sheria.
Hii migao ya umeme haijaanza leo. Hili tatizo lipo kila mwaka na sababu zinazotolewaga ni zile zile. Kusudio langu halihusu kuhoji uhalali wa mgao bali taratibu zinazotumika kuendesha mgao wenyewe.
Hatua hii itajikita kuwahoji na kuwataka TANESCO watoe ufafanuzi ni hatua gani za makusudi wanachukua kuhakikisha wanapunguza madhara ya mgao kwa watumiaji. Nahisi hili halijawahi kufanyiwa kazi ipasavyo.
Kwa mfano, nataka kuwahoji kwa nini maeneo ya makazi wanaacha umeme wakati mwingine siku nzima halafu wanakuja kukata mida ya usiku? Usiku kuna karaha za joto na giza, tofauti na mchana. Kwa nini mgao usijikite tu mida ya asubuhi-jioni. Kwa mchana hata wakikata kila siku masaa 6 kwa siku, wakibadili (saa 12 asubuhi-6 mchana) na (saa 6 mchana-12 jioni) zoezi halitakuwa karaha kama ilivyo hivi sasa.
Pia kwa nini hawatoi ratiba rasmi ya mgao? Ratiba inasaidia mtu au biashara kupanga shughuli zako ipasavyo.
Mahakama na vyombo vingine vya sheria inabidi iwalazimishe TANESCO kutengeneze mwongozo rasmi wa taratibu rafiki watakazokuwa wanazitumia katika migao maana sitegemeo kama huu utakuwa mgao wa mwisho.
Hii migao ya umeme haijaanza leo. Hili tatizo lipo kila mwaka na sababu zinazotolewaga ni zile zile. Kusudio langu halihusu kuhoji uhalali wa mgao bali taratibu zinazotumika kuendesha mgao wenyewe.
Hatua hii itajikita kuwahoji na kuwataka TANESCO watoe ufafanuzi ni hatua gani za makusudi wanachukua kuhakikisha wanapunguza madhara ya mgao kwa watumiaji. Nahisi hili halijawahi kufanyiwa kazi ipasavyo.
Kwa mfano, nataka kuwahoji kwa nini maeneo ya makazi wanaacha umeme wakati mwingine siku nzima halafu wanakuja kukata mida ya usiku? Usiku kuna karaha za joto na giza, tofauti na mchana. Kwa nini mgao usijikite tu mida ya asubuhi-jioni. Kwa mchana hata wakikata kila siku masaa 6 kwa siku, wakibadili (saa 12 asubuhi-6 mchana) na (saa 6 mchana-12 jioni) zoezi halitakuwa karaha kama ilivyo hivi sasa.
Pia kwa nini hawatoi ratiba rasmi ya mgao? Ratiba inasaidia mtu au biashara kupanga shughuli zako ipasavyo.
Mahakama na vyombo vingine vya sheria inabidi iwalazimishe TANESCO kutengeneze mwongozo rasmi wa taratibu rafiki watakazokuwa wanazitumia katika migao maana sitegemeo kama huu utakuwa mgao wa mwisho.