Kodi ya ardhi sijui jengo

Annonymous

JF-Expert Member
May 9, 2013
479
839
Wabari wa jambi kuna kitu nimekuwa nakiwaza naona kinanipa utata aidha mnisaidie kunielekeza

1. Je tanesco wanatoza kodi ya JENGO AU ARDHI?
1.1. kama ni ardhi kwanini mtu mwenye eneo lake anafuga kuku au mbuzi au analima ila anatumia umeme wa solar au hatumii umeme kabisa au mshumaa hapigwi kodi hii
1. 2. Kama ni jengo kwanini baadhi
1.2.1. Kwanini majengo yenye umeme tu sio yasiyo na umeme na ni majengo. Mfano kanisa na misikiti ambayo inatumia umeme wa jua (solar) hayatozwi sio ukwepaji kodi huu
2. JE hii kodi ya ardhi sijui jengo ni Tsh ngapi kwa mwaka. Wengine wanasema ni 10,000 kwa maana kwa mwezi inatakiwa kutozwa chini ya 899 wengine wanasemani elf 26,000 ndio maana kwa mwezi ni elf 2
3. Kwanini nyumba za kupangishwa zitozwe bei moja na nyumba za makazi hali moja inafanya buashara moja haifanyi biashara.
4. Ikiwa ni kodi ya ardhi kwanini ghorofa linatozwa bei 10,000 kwa nwezi (kodi ya zamani kabla ya kupanda) na zingine zilikuwa 1000 tu. Na kama ni kodi ya jengo kwanini mtu anayeweka tu sehemu yake ya kuchomelea welding au kiwanda cha matofali alipe hii hali ya kuwa hana jengo lolote alilojenga?
5. Kama kodi hii ni kwaajili ya ardhi au jengo je ni halali kila mwaka wa budget ikapandishwa ?
6. Nani anafaa kulipia kodi hii je ni
Mwenye nyumba au wapangaji?
7. Ikiwa kila mwaka mtumiaji wa nyumba anapaswa kulipia kodi hii je dhana ya kwamba umetoka kupanga na kwenda kwako ikoje au ni umetoka kupanga kwa mwenye nyumba na kwenda kupanga kwa serikali. Vipi kama serikali ikajenga nyumba ikanipangisha nikalipia hii kodi

hoja nyingine tu
. Ile hela za miamala (tozo) zilisemwa ni za uzalendo za muda, badae zikapandishwa tena na kushushwa na zimeinhizwa hadi kwenye huduma ya lipa kwa simu hali ya kuwa mfanya biashara wa lipa kwa simu tayari nguo zake ameshalipia kodi huko china, bandalini, kwenye lisit ya EFD na bado mteja wake analipishwa kodi anapomlipa hela, aidha manake serikali inamdiscourage mnunuzi kutumia huduma ya Lipa jwa simu ili atumie pesa CASH. JE hii ni sawa

Naomba anayejua vyema juhusu haya mambo anifundishe kidogo
 
TANESCO Wanatoza PROPERTY TAX yaani kodi ya jengo...alafu halmashauri wanatoza LAND RENT yaani kodi ya kiwanja...
 
TANESCO Wanatoza PROPERTY TAX yaani kodi ya jengo...alafu halmashauri wanatoza LAND RENT yaani kodi ya kiwanja...
Kodi ya ardhi hulipwa serikalini wizara ya ardhi na kodi ya jengo pia hulipwa serikalini kupitia Luku.
 
Back
Top Bottom