beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,880
- 6,367
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuona msanii na mlimbwende wa Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu na wafanyakazi wake wawili wana kesi ya kujibu kutokana kukabiliwa na kesi ya kutumia dawa za kulevya.
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Aprili 23 na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na kwamba Wema na wenzake wataanza kujitetea Mei 14 na 15, 2018.
Hakimu Simba ametoa uamuzi huo baada ya kupitia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na mashahidi watano wa upande wa mashtaka waliokuwa wakiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula.
Kabla ya uamuzi huo kutolewa na Hakimu Simba, Wakili Kakula aliiambia mahakama kuwa kesi hiyo leo ilipangwa kwa ajili ya uamuzi kama washtakiwa hao wana kesi ya kujibu ama la.
Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Simba amesema kwa mujibu wa sheria iwapo washtakiwa watapatikana kuwa wana kesi ya kujibu wataanza kujitetea na wakionekana hawana kesi ya kujibu wataachiwa huru.
Hakimu Simba amesema baada ya kupitia hoja zote zilizowasilishwa mahakamani hapo imejitosheleza kwamba washtakiwa wote wana kesi ya kujibu katika mashtaka yote, hivyo wana haki ya kisheria kuanza kujitetea.
Amesema washtakiwa wataanza kujitetea Mei 14 na 15, 2018.
=======
Wema Sepetu kukamatwa na kuhukumiwa kwa kukutwa na madawa ya kulevya
Kuhukumiwa na kuachiwa huru baada ya kulipa faini
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Aprili 23 na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na kwamba Wema na wenzake wataanza kujitetea Mei 14 na 15, 2018.
Hakimu Simba ametoa uamuzi huo baada ya kupitia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na mashahidi watano wa upande wa mashtaka waliokuwa wakiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula.
Kabla ya uamuzi huo kutolewa na Hakimu Simba, Wakili Kakula aliiambia mahakama kuwa kesi hiyo leo ilipangwa kwa ajili ya uamuzi kama washtakiwa hao wana kesi ya kujibu ama la.
Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Simba amesema kwa mujibu wa sheria iwapo washtakiwa watapatikana kuwa wana kesi ya kujibu wataanza kujitetea na wakionekana hawana kesi ya kujibu wataachiwa huru.
Hakimu Simba amesema baada ya kupitia hoja zote zilizowasilishwa mahakamani hapo imejitosheleza kwamba washtakiwa wote wana kesi ya kujibu katika mashtaka yote, hivyo wana haki ya kisheria kuanza kujitetea.
Amesema washtakiwa wataanza kujitetea Mei 14 na 15, 2018.
=======
Wema Sepetu kukamatwa na kuhukumiwa kwa kukutwa na madawa ya kulevya
- Wema Sepetu, Mr. Blue, TID, Recho wahusishwa na Dawa za Kulevya. Watakiwa kuripoti kituo cha Polisi
- Kamanda Siro: Wema Sepetu, TID na Nyandu Tozi bado wanashikiliwa na jeshi la polisi
- Sakata la Madawa ya Kulevya: Wema Sepetu afikishwa Mahakamani, apata dhamana
- Wema Sepetu kapatikana na bangi
- Tundu Lissu kumtetea Wema Sepetu
- Maajabu: Serikali haiwajui Vigogo wa Dawa za Kulevya hadi inataka Wema awatajie?
- Makonda kumfuata Wema mahabusu nyakati za usiku, hii imekaaje?
- Sauti ya Wema Sepetu iliyosambaa akiwatoa hofu Mashabiki
- Kesi ya Wema Sepetu hadi mwakani
- Wema Sepetu amefiwa, kesi yake yapigwa kalenda
- Dawa za Kulevya: Wema adai Makonda anatembea na Agnes Masogange ndio maana hakamatwi
- Wema Sepetu Apandishwa Tena Kizimbani Kisutu leo
- Vita ya Dawa za Kulevya: Steve Nyerere alivyopiga kambi Bungeni Kumuokoa Wema Sepetu
- Kesi ya Wema Sepetu yaahirishwa, uchunguzi haujakamilika
- Kutoka mahakamani: Wema Sepetu hakufanyiwa upekuzi kwenye maungo ya mwili wake, asema Hakimu
- Mkemia Mkuu: Mkojo wa Wema Sepetu ulikuwa na bangi
- Kibatala aandika barua ya kujitoa kesi ya Wema Sepetu, Alberto Msando aandika barua ya kuwa wakili mpya
- KISUTU: Wema Sepetu afika na Wakili wake Msando kwenye kesi. Diamond na Hamisa nao wafika Mahakama ya watoto
- Shahidi kesi ya Wema asema bangi ilikutwa jikoni
- Kisutu: Korti yakataa vielelezo vya ushahidi kesi ya Wema Sepetu. Masogange akutwa na kesi ya kujibu
Kuhukumiwa na kuachiwa huru baada ya kulipa faini