MIMI BABA YENU
JF-Expert Member
- Mar 1, 2019
- 309
- 736
Kanisa LENYE Maadili ni nguzo muhimu katika ujenzi wa Taifa imara lakini Kanisa LENYE NDIMI NYINGI ni hatari sana kwa Usalama wa Nchi!Kanisa linalobeba maslahi ya kisiasa kwa kuhakikisha "linawaprotect"waumini wake hata kama ni Wahalifu ni hatari sana kwa Usalama wa Nchi!
Kanisa la Katoliki limekuwa na historia mbaya sana,mfano kwa majirani zetu(Rwanda + DRC) katika kahatarisha amani na Usalama wa Taifa!
Hakimu mmoja wa Mahakama ya Maalum ya kusimamia Kesi za Mauaji ya Kimbari ya Rwanda mwaka 1994 alilaumu Viongozi wa kanisa la Katoliki la Rwanda kwa kuwalinda wahusika wa Mauaji ya Kimbari ambao walikuwa ni Mapadre wa Katoliki!
Katika Mahojiano na Gazeti la Badisches Tagblatt la Ujerumani Jaji Wolfgang Schaumburg ambaye alikuwa mmoja wa Majaji wa Mahakama Maalum ya Kimbari Nchini Rwanda aliwanyoshea kidole viongozi wa Kanisa la Katoliki kwa kuwalinda mapadre wa Kanisa hilo ambao walishiriki katika Mauaji ya Kimbari Rwanda na kutaka wafikishwe mahakamani!
Padre Wenceslas Munyeshyaka mwaka 1994 alibeba bunduki kama Mwanajeshi na kupanga nyama na waasi wa Kihutu kufanya maauji!Padre Athanase Seromba alikimbizwa Ulaya kwa msaada wa Kanisa la Katoliki na kubadilishiwa Pasipoti yake pamoja na JINA!Maadili ya Kanisa la Katoliki yana tia mashaka sana!
NINI NATAKA KUSEMA?
I.Katika Mkesha wa Pasaka Jana,Baraza la Maaskofu wa Katoliki Tanzania(TEC) limetoa wito kwa Serikali kuwaachia Huru na bila masharti yoyote Viongozi wa kisiasa waliokamatwa kwa kudai haki!Baraza kupitia kwa Rais wake Askofu Wolfgang Pisa wa Jimbo la Katoliki la Lindi!
Katika matamshi yake Askofu huyo wa Katoliki alisisitiza umuhimu wa Mhimili wa Mahakama kutoingiliwa lakini wakati huo huo akaitaka Serikali kuwaachia mara moja tena bila masharti wanasiasa wote waliokamatwa kwa kudai haki!Hizi ndio NDIMI NYINGI za Kanisa la Katoliki la Tanzania!
II.Je,Kanisa la Katoliki limekosa "balance" katika kuwalinda waumini na kuilinda Serikali pia!
Ujumbe mwingi kutoka kwa viongozi wa dini wakati wa Siku ya Ijumaa Kuu ulikuwa ni pamoja na HAKI HAKI HAKI lakini ujumbe huo ukakosa kabisa neno WAJIBU WAJIBU WAJIBU!Kanisa ambalo haliwezi kuwakumbusha waumini wake wajibu wao kwa Serikali yao ni sawa na NGO yoyote ile ya Kiharakati!
Hivi Matamshi ya Mh Tundu Antipas Lissu mbele ya Watanzania"Uchaguzi hautofanyika,tutakinukisha" ni lini yamekemewa na Viongozi wa dini hasa baraza la Maaskofu wa Tanzania(TEC)??
III.Ni Kanisa hili hili la Katoliki la Tanzania wakati wa awamu fulani lisingeweza kuthubutu kutoa tamko kama hili hata wakati wa "madhila" makubwa ya kisiasa ambayo yalikuwa yanatokea wakati wa awamu ile!
Hakuna haki isiyo na wajibu ndani yake na kama Kanisa litaendelea kupigania HAKI bila WAJIBU basi Kanisa la Katoliki Tanzania linataka kutupeleka shimoni!
Acha Kanisa lilinde Imani,Acha Serikali ilinde Amani na Usalama wa Nchi yetu!
Kanisa la Katoliki limekuwa na historia mbaya sana,mfano kwa majirani zetu(Rwanda + DRC) katika kahatarisha amani na Usalama wa Taifa!
Hakimu mmoja wa Mahakama ya Maalum ya kusimamia Kesi za Mauaji ya Kimbari ya Rwanda mwaka 1994 alilaumu Viongozi wa kanisa la Katoliki la Rwanda kwa kuwalinda wahusika wa Mauaji ya Kimbari ambao walikuwa ni Mapadre wa Katoliki!
Katika Mahojiano na Gazeti la Badisches Tagblatt la Ujerumani Jaji Wolfgang Schaumburg ambaye alikuwa mmoja wa Majaji wa Mahakama Maalum ya Kimbari Nchini Rwanda aliwanyoshea kidole viongozi wa Kanisa la Katoliki kwa kuwalinda mapadre wa Kanisa hilo ambao walishiriki katika Mauaji ya Kimbari Rwanda na kutaka wafikishwe mahakamani!
Padre Wenceslas Munyeshyaka mwaka 1994 alibeba bunduki kama Mwanajeshi na kupanga nyama na waasi wa Kihutu kufanya maauji!Padre Athanase Seromba alikimbizwa Ulaya kwa msaada wa Kanisa la Katoliki na kubadilishiwa Pasipoti yake pamoja na JINA!Maadili ya Kanisa la Katoliki yana tia mashaka sana!
NINI NATAKA KUSEMA?
I.Katika Mkesha wa Pasaka Jana,Baraza la Maaskofu wa Katoliki Tanzania(TEC) limetoa wito kwa Serikali kuwaachia Huru na bila masharti yoyote Viongozi wa kisiasa waliokamatwa kwa kudai haki!Baraza kupitia kwa Rais wake Askofu Wolfgang Pisa wa Jimbo la Katoliki la Lindi!
Katika matamshi yake Askofu huyo wa Katoliki alisisitiza umuhimu wa Mhimili wa Mahakama kutoingiliwa lakini wakati huo huo akaitaka Serikali kuwaachia mara moja tena bila masharti wanasiasa wote waliokamatwa kwa kudai haki!Hizi ndio NDIMI NYINGI za Kanisa la Katoliki la Tanzania!
II.Je,Kanisa la Katoliki limekosa "balance" katika kuwalinda waumini na kuilinda Serikali pia!
Ujumbe mwingi kutoka kwa viongozi wa dini wakati wa Siku ya Ijumaa Kuu ulikuwa ni pamoja na HAKI HAKI HAKI lakini ujumbe huo ukakosa kabisa neno WAJIBU WAJIBU WAJIBU!Kanisa ambalo haliwezi kuwakumbusha waumini wake wajibu wao kwa Serikali yao ni sawa na NGO yoyote ile ya Kiharakati!
Hivi Matamshi ya Mh Tundu Antipas Lissu mbele ya Watanzania"Uchaguzi hautofanyika,tutakinukisha" ni lini yamekemewa na Viongozi wa dini hasa baraza la Maaskofu wa Tanzania(TEC)??
III.Ni Kanisa hili hili la Katoliki la Tanzania wakati wa awamu fulani lisingeweza kuthubutu kutoa tamko kama hili hata wakati wa "madhila" makubwa ya kisiasa ambayo yalikuwa yanatokea wakati wa awamu ile!
Hakuna haki isiyo na wajibu ndani yake na kama Kanisa litaendelea kupigania HAKI bila WAJIBU basi Kanisa la Katoliki Tanzania linataka kutupeleka shimoni!
Acha Kanisa lilinde Imani,Acha Serikali ilinde Amani na Usalama wa Nchi yetu!