Pre GE2025 Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Kalambo kwa kushirikina na TRA yatoa vitenge 200 kwa wajawazito

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Aug 29, 2022
783
1,660
Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa kwa kushirikina na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekabidhi msaada wa vitenge 200 kwa wanawake wajawazito katika Hosptali ya Wilaya ya Kalambo na vituo vya kutolea huduma za afya kama sehemu ya kurejesha faida kwa wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Dkt.Lazaro Komba amesema msaada huo umetokana na kodi za wananchi na kusisitiza wafanyabiashara kujenga utamaduni wa kulipa kodi bila kusukumwa ili kuiwezesha Serikali kukamilisha bajeti zake kwa urahisi ikiwemo utekelezaji miradi mbalimbali ya maendeleo.

Soma Pia: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Meneja wa TRA Wilayani humo Wiliam Gwimo amesema kwa kipindi cha miezi saba (7) Serikali imevuka malengo ya ukusanyaji mapato na kwamba zoezi la utoaji misaada litakuwa endelevu.

 
Back
Top Bottom