Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,717
- 4,458
Wakuu,
Hivi kulikuwa na haja ya watu kuitisha press kutuambia kuwa wamefikia asilimia 50 ya majukumu ya kazi yao?
Kwanini wasingetupa majibu baada ya kupata majibu kamili?
===============================================
Baada ya Rais Samia kutoa agizo la kuanzishwa kwa tume ya siku 30 kuchunguza wafanyabiashara wa kigeni Kariakoo tarehe 30 Januari 2025, siku ya leo kamati hiyo imefikia asilimia 50 ya uchunguzi wake na imeahidi kuwasilisha ripoti yake Machi 2, 2025 kama ilivyoagizwa.
Kamati hiyo, iliyoundwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo mnamo Februari 2, 2025, inaongozwa na Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Profesa Edda Lwoga.
Tangu kuanza kazi, imekuwa ikihoji wafanyabiashara wa makundi mbalimbali, wakiwemo machinga, wauza vifaa vya umeme, vipodozi, na bidhaa nyingine, ili kupata uhalisia wa changamoto zinazowakabili.
Akizungumza mwishoni mwa wiki, Profesa Lwoga alisema kuwa kamati hiyo inaendelea kukusanya maoni kutoka kwa wafanyabiashara na wananchi kupitia mahojiano ya moja kwa moja na njia za simu.
Imetoa namba ya bure 080011616 na namba ya WhatsApp 0738 816 113 ili wananchi waweze kushiriki kwa kutoa maoni yao, kuhakikisha ripoti inayowasilishwa inagusa maeneo yote muhimu ya uchunguzi.
Source: Jambo TV
Hivi kulikuwa na haja ya watu kuitisha press kutuambia kuwa wamefikia asilimia 50 ya majukumu ya kazi yao?
Kwanini wasingetupa majibu baada ya kupata majibu kamili?
===============================================
Baada ya Rais Samia kutoa agizo la kuanzishwa kwa tume ya siku 30 kuchunguza wafanyabiashara wa kigeni Kariakoo tarehe 30 Januari 2025, siku ya leo kamati hiyo imefikia asilimia 50 ya uchunguzi wake na imeahidi kuwasilisha ripoti yake Machi 2, 2025 kama ilivyoagizwa.
Kamati hiyo, iliyoundwa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo mnamo Februari 2, 2025, inaongozwa na Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Profesa Edda Lwoga.
Tangu kuanza kazi, imekuwa ikihoji wafanyabiashara wa makundi mbalimbali, wakiwemo machinga, wauza vifaa vya umeme, vipodozi, na bidhaa nyingine, ili kupata uhalisia wa changamoto zinazowakabili.
Akizungumza mwishoni mwa wiki, Profesa Lwoga alisema kuwa kamati hiyo inaendelea kukusanya maoni kutoka kwa wafanyabiashara na wananchi kupitia mahojiano ya moja kwa moja na njia za simu.
Imetoa namba ya bure 080011616 na namba ya WhatsApp 0738 816 113 ili wananchi waweze kushiriki kwa kutoa maoni yao, kuhakikisha ripoti inayowasilishwa inagusa maeneo yote muhimu ya uchunguzi.
Source: Jambo TV