Magical power
JF-Expert Member
- Sep 27, 2022
- 1,990
- 5,249
Kaka nilikutana na huyu mwanamke akiwa amepigika nikamzoa Hadi Akawa mtu katika watu,
alikuwa anatembeza soksi na nguo za nd0ani mtaa Kwa mtaa amepauka miguu ndara zimekatika.
Nilimpa Msaada nikamnunulia sendo hapo ndipo ikawa mwanzo wa kufahamiana niliona mwanga ndani yake na nilitarajia kujenga nae maisha .
Tulifahamiana Baada ya siku kadhaa alipo nieleza hali ya kwao nilipanga nae safari mpk huko nilikuta hali ni mbaya kwel kweli nilijitutumua niliezeka nyumba ya baba yake kijijini kwa hiari kabisa
Upendo wake kwangu uliongezeka aliniambia, sehemu ya maisha yake iliyobaki hapa duniani atamalizia na mimi
Kwa nia njema na upendo nilionao kwake, nilihakikisha kuwa nimsaidia .Hapo ndipo nilipogundua alikuwa chuo mwaka wa kwanza baba yake alifariki akakosa wakumuendeleza akasitisha masomo nikasimamia Hilo jukumu Kwa Nia ya dhati kabisa
Akasoma Bada ya kumaliza amepata ajira visingizio vikaanza mara kazin haruhusiwi kutumia simu muda wote mara haruhusiwi kuonekana na mwanamume nyumbani kwake ikiwa hana cheti Cha ndoa .usku hapokei simu nikasema isiwe tabu nikaenda kwao kuonana mama yake ili nipate baraka za kuoana ,mama yake akashangaa sana ananiambia mwanae anasema tulishaachana muda sana ananiambia Binti yake ameposwa muda na mwanaume mwingine.
Nawaza sana nashindwa nifanyeje.
Nilimpa Msaada nikamnunulia sendo hapo ndipo ikawa mwanzo wa kufahamiana niliona mwanga ndani yake na nilitarajia kujenga nae maisha .
Tulifahamiana Baada ya siku kadhaa alipo nieleza hali ya kwao nilipanga nae safari mpk huko nilikuta hali ni mbaya kwel kweli nilijitutumua niliezeka nyumba ya baba yake kijijini kwa hiari kabisa
Upendo wake kwangu uliongezeka aliniambia, sehemu ya maisha yake iliyobaki hapa duniani atamalizia na mimi
Kwa nia njema na upendo nilionao kwake, nilihakikisha kuwa nimsaidia .Hapo ndipo nilipogundua alikuwa chuo mwaka wa kwanza baba yake alifariki akakosa wakumuendeleza akasitisha masomo nikasimamia Hilo jukumu Kwa Nia ya dhati kabisa
Akasoma Bada ya kumaliza amepata ajira visingizio vikaanza mara kazin haruhusiwi kutumia simu muda wote mara haruhusiwi kuonekana na mwanamume nyumbani kwake ikiwa hana cheti Cha ndoa .usku hapokei simu nikasema isiwe tabu nikaenda kwao kuonana mama yake ili nipate baraka za kuoana ,mama yake akashangaa sana ananiambia mwanae anasema tulishaachana muda sana ananiambia Binti yake ameposwa muda na mwanaume mwingine.
Nawaza sana nashindwa nifanyeje.