Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Bara Vodacom Premier League VPL' kuvurumishwa leo Aprili 21, 2021 ambapo Kagera Sugar wanacheza na Mnyama Mkali Kuliko Wote Mwituni, Mabingwa wa Nchi, Simba SC kwenye uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba.
Kila timu imejiandaa kuweza kushinda na kujikusanyia alama tatu muhimu ili kuweza kujiweka sawa kwenye msimamo wa VPL, ambapo Kagera Sugar wanashika nafasi ya 14 wakiwa na alama 27 huku Simba SC wakishika nafasi ya 2 kwa alama 52.
Kocha wa Kagera Sugar Francis Baraza anasema mchezo utakuwa mgumu lakini anachotaka ni ushindi ili kujinasua nafasi ya chini.
Naye Kocha Didier Gomes amesema anafahamu ushindani utakuwepo katika mechi hiyo kutokana na wapinzani walivyo lakini kwa maandalizi waliofanya wataondoka na alama tatu.
Kumbuka mtanange huu ni kuanzia saa 10: 00 jioni. Usikose Ukasimuliwa
Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
••••
Wakati wowote mpira utaanza. Timu zote mbili zipo uwanjani zikifanyiwa ukaguzi, salamu pamoja na kupiga picha za kumbukumbu.
Naaaam mpira umeanza ni vita vya VPL'
05' Mpira umeanza kwa kasi huku Simba SC wakimiliki zaidi mpira kwa mashambulizi makali ambayo hayakuzaa matunda kuelekea upande wa Kagera Sugar.
10' Kwakweli mpira una kasi huku Simba wakijaribu kupenya lango, na Kagera akijibu kwa kutumia mipira ya kustukiza lango la simba.
12' Miquissone Goooooooooooooaal Gooooal
Luis Miquissone anaipatia Simba SC bao la kwanza akipokea pasi safi kutoka kwa Chama.
Kagera Sugar 0-1 Simba SC
20' Kagera Sugar wanashika dimba, Abdallah Mfuko anapiga shutiiiiii golikipa Manula anadaka bila wasiwasi.
23' Mugalu Goooooooooooooaal Gooooal
Kope Mutshimba Mugalu anaipatia Simba SC bao la pili akipokea pasi safi kutoka kwa Dilunga
Kagera Sugar 0-2 Simba SC
Kasi imepungua hasa kipindi hiki kuelekea kuwa mapumziko, timu zote.
45+2' Anapiga shutiiiiii loooooo golikipa unamngonga na kurudi uwanjani, ilikuwa hatari sana lango la Kagera.
Naaaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wapo mbele kwa mabao mawili kwa bila dhidi ya Kagera Sugar
HT, VPL; Kagera Sugar 0-2 Simba SC.
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Kaitaba.
Kagera Sugar wakifanya mabadiliko, ametoka Abdallah Mfuko na ameingia Mwaterema.
52' Yusuf Mhilu anapiga shutiiiiii linatoka nje ya lango la Simba SC, ilikuwa nafasi bomba kwa Kagera.
59' Mwaterema anaonyesha Kadi ya Njano baada ya kumfanyia madhambi Miquissone.
Ametoka Dilunga na ameingia Rally Bwalya upande wa Simba SC.
Timu zinacheza kwa tahadhari kipindi hiki cha pili. Ametoka Mwalyanzi na ameingia Nanguo upande wa Kagera.
73' Ametoka Mugalu na ameingia Kagere upande wa Simba SC.
83' Kagere kwake Chamaaa loooooo.. golikipa anatema shuti lile na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda
Kagera Sugar 0-2 Simba SC
Ametoka Mzamir na nafasi yake imechukuliwa na Nyoni upande wa Simba SC.
Kadi za njano kwa Taddeo, Miquissone upande wa Simba SC.
90+4' kuelekea kumalizika kwa mchezo huu wa VPL
Naaaam mpira umekwishaaa ambapo Simba SC wanaibuka na ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya Kagera Sugar.
FT, VPL: Kagera Sugar 0-2 Simba SC
Ghazwat
Kila timu imejiandaa kuweza kushinda na kujikusanyia alama tatu muhimu ili kuweza kujiweka sawa kwenye msimamo wa VPL, ambapo Kagera Sugar wanashika nafasi ya 14 wakiwa na alama 27 huku Simba SC wakishika nafasi ya 2 kwa alama 52.
Kocha wa Kagera Sugar Francis Baraza anasema mchezo utakuwa mgumu lakini anachotaka ni ushindi ili kujinasua nafasi ya chini.
Naye Kocha Didier Gomes amesema anafahamu ushindani utakuwepo katika mechi hiyo kutokana na wapinzani walivyo lakini kwa maandalizi waliofanya wataondoka na alama tatu.
Kumbuka mtanange huu ni kuanzia saa 10: 00 jioni. Usikose Ukasimuliwa
Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
••••
Wakati wowote mpira utaanza. Timu zote mbili zipo uwanjani zikifanyiwa ukaguzi, salamu pamoja na kupiga picha za kumbukumbu.
Naaaam mpira umeanza ni vita vya VPL'
05' Mpira umeanza kwa kasi huku Simba SC wakimiliki zaidi mpira kwa mashambulizi makali ambayo hayakuzaa matunda kuelekea upande wa Kagera Sugar.
10' Kwakweli mpira una kasi huku Simba wakijaribu kupenya lango, na Kagera akijibu kwa kutumia mipira ya kustukiza lango la simba.
12' Miquissone Goooooooooooooaal Gooooal
Luis Miquissone anaipatia Simba SC bao la kwanza akipokea pasi safi kutoka kwa Chama.
Kagera Sugar 0-1 Simba SC
20' Kagera Sugar wanashika dimba, Abdallah Mfuko anapiga shutiiiiii golikipa Manula anadaka bila wasiwasi.
23' Mugalu Goooooooooooooaal Gooooal
Kope Mutshimba Mugalu anaipatia Simba SC bao la pili akipokea pasi safi kutoka kwa Dilunga
Kagera Sugar 0-2 Simba SC
Kasi imepungua hasa kipindi hiki kuelekea kuwa mapumziko, timu zote.
45+2' Anapiga shutiiiiii loooooo golikipa unamngonga na kurudi uwanjani, ilikuwa hatari sana lango la Kagera.
Naaaam mpira ni mapumziko ambapo Simba wapo mbele kwa mabao mawili kwa bila dhidi ya Kagera Sugar
HT, VPL; Kagera Sugar 0-2 Simba SC.
Kipindi cha pili kimeanza uwanja wa Kaitaba.
Kagera Sugar wakifanya mabadiliko, ametoka Abdallah Mfuko na ameingia Mwaterema.
52' Yusuf Mhilu anapiga shutiiiiii linatoka nje ya lango la Simba SC, ilikuwa nafasi bomba kwa Kagera.
59' Mwaterema anaonyesha Kadi ya Njano baada ya kumfanyia madhambi Miquissone.
Ametoka Dilunga na ameingia Rally Bwalya upande wa Simba SC.
Timu zinacheza kwa tahadhari kipindi hiki cha pili. Ametoka Mwalyanzi na ameingia Nanguo upande wa Kagera.
73' Ametoka Mugalu na ameingia Kagere upande wa Simba SC.
83' Kagere kwake Chamaaa loooooo.. golikipa anatema shuti lile na kuwa kona ambayo haikuzaa matunda
Kagera Sugar 0-2 Simba SC
Ametoka Mzamir na nafasi yake imechukuliwa na Nyoni upande wa Simba SC.
Kadi za njano kwa Taddeo, Miquissone upande wa Simba SC.
90+4' kuelekea kumalizika kwa mchezo huu wa VPL
Naaaam mpira umekwishaaa ambapo Simba SC wanaibuka na ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya Kagera Sugar.
FT, VPL: Kagera Sugar 0-2 Simba SC
Ghazwat