Mwananchi Huru
JF-Expert Member
- Nov 20, 2021
- 2,082
- 1,871
===
Huu ni mwaka ambao Dira ya Maendeleo ya Taifa ya awamu ya tatu chini ya Rais Benjamin Mkapa (2000-2025) imekamilika kwa mafanikio wakati Dira ya Sasa ya 2025-2050 chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeandaliwa na inasubiri kuzinduliwa tu kwa mafanikio pamoja na kwamba huu ni mwaka wa Uchaguzi alisema David Kafulila Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia nchini Tanzania PPPC Bw David Kafulila.
Kwenye Dunia hii ambayo ni ya Utandawazi ( information age ) Mahitaji ya binadamu duniani kote yamezidi kuwa makubwa zaidi ukilinganisha na uwezo w Serikali zetu zote duniani kuyakidhi Mahitaji hayo kwa kutumia Mikopo na Kodi ndio sababu Dunia inatutaka sisi kama Serikali kutafuta njia Mbadala ya kuendesha bajeti zetu nje ya Kodi au Mikopo alisisitiza.
Anasema, Kwa mujibu wa Ripoti ya IMF ya Oct 2024 uchumi wa dunia wa Serikali zote duniani umefikia US$ 102trilion wakati deni la dunia ni asilimia 95 ya Uchumi huo, Vile vile Deni lote la sekta binafsi nalo limefikia $164Trilioni huku Uchumi wote wa Dunia ukifikia $110trilioni ( Serikali & private ) lakini deni lote la Serikali, Sekta binafsi na Kaya jumla yake ni US$ 320 trilioni, Kwa maana nyingine deni la Dunia ni karibu mara tatu ya Uchumi wote wa Dunia kwa lugha nyepesi Dunia hii inaendeshwa kwa Mikopo.
Kafulila anasema wakati Uwiano wa deni la Africa kwa Uchumi wa Africa ni 67% Tanzania iko katika Hali nzuri kwani Uchumi kwa deni ni 47% wakati Kenya ni 70%, Rwanda% 71, Malawi 84% Msumbiji 96% Ghana 90% hivyo mwenendo wa deni la Tanzània kwa Uchumi wake ni mzuri ukilingamishwa na Chumi za nchi nyingi za Africa Mashariki na kati na Kusini.
Huu ni mwaka ambao Dira ya Maendeleo ya Taifa ya awamu ya tatu chini ya Rais Benjamin Mkapa (2000-2025) imekamilika kwa mafanikio wakati Dira ya Sasa ya 2025-2050 chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeandaliwa na inasubiri kuzinduliwa tu kwa mafanikio pamoja na kwamba huu ni mwaka wa Uchaguzi alisema David Kafulila Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia nchini Tanzania PPPC Bw David Kafulila.
Kwenye Dunia hii ambayo ni ya Utandawazi ( information age ) Mahitaji ya binadamu duniani kote yamezidi kuwa makubwa zaidi ukilinganisha na uwezo w Serikali zetu zote duniani kuyakidhi Mahitaji hayo kwa kutumia Mikopo na Kodi ndio sababu Dunia inatutaka sisi kama Serikali kutafuta njia Mbadala ya kuendesha bajeti zetu nje ya Kodi au Mikopo alisisitiza.
Anasema, Kwa mujibu wa Ripoti ya IMF ya Oct 2024 uchumi wa dunia wa Serikali zote duniani umefikia US$ 102trilion wakati deni la dunia ni asilimia 95 ya Uchumi huo, Vile vile Deni lote la sekta binafsi nalo limefikia $164Trilioni huku Uchumi wote wa Dunia ukifikia $110trilioni ( Serikali & private ) lakini deni lote la Serikali, Sekta binafsi na Kaya jumla yake ni US$ 320 trilioni, Kwa maana nyingine deni la Dunia ni karibu mara tatu ya Uchumi wote wa Dunia kwa lugha nyepesi Dunia hii inaendeshwa kwa Mikopo.
Kafulila anasema wakati Uwiano wa deni la Africa kwa Uchumi wa Africa ni 67% Tanzania iko katika Hali nzuri kwani Uchumi kwa deni ni 47% wakati Kenya ni 70%, Rwanda% 71, Malawi 84% Msumbiji 96% Ghana 90% hivyo mwenendo wa deni la Tanzània kwa Uchumi wake ni mzuri ukilingamishwa na Chumi za nchi nyingi za Africa Mashariki na kati na Kusini.