KERO Kada ya Afya - Halmashauri ya Kilosa hatujalipwa fedha za kujikimu, tumeambiwa hadi hali ya fedha itakapotengemaa

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Screenshot 2025-02-10 091821.png
Sisi Watumishi wa Umma ambao ni waajiriwa wapya Serikalini katika Kada ya Afya, Halmashauri ya Kilosa Mkoani Morogoro tuna changamoto ya kutolipwa stahiki zetu za fedha za kujikimu na majibu tunayopewa yanatukatisha tamaa.

Huu ni mwezi wa tatu sasa tunafuatulia malipo hayo, awali tuliambiwa tujaze fomu za kuonesha uhitaji wetu wa malipo hayo lakin juzi tumepewa majibu yaliyotolewa kwa barua, yametukatisha tamaa.

Tumejibiwa na Mkurugenzi kuwa tutapatiwa endapo hali ya kifedha itakapotengemaa, sasa tunajiuliza lini hali ya kiuchumi itakaa sawa?

Tunaomba kilio chetu kifike kwa Wizara ya Afya kuwa Watumishi tunahitaji malipo hayo kwa kuwa tunajua ni haki yetu, watusaidie kupata, yatatusaidia kujikimu kwani wengi wetu ndio kwanza tunaanza maisha na tulitarajia kutumia kulipa kodi na mahitaji mengine ya msingi.

Pia soma ~ Ajira mpya kada ya afya halmashauri nyingi hatujapokea fedha za kujikimu toka November 2024
 
Ila cha ajabu hao wakubwa hapo Halmashauri wanalipana posho kama kawaida.
 
Sisi Watumishi wa Umma ambao ni waajiriwa wapya Serikalini katika Kada ya Afya, Halmashauri ya Kilosa Mkoani Morogoro tuna changamoto ya kutolipwa stahiki zetu za fedha za kujikimu na majibu tunayopewa yanatukatisha tamaa.

Huu ni mwezi wa tatu sasa tunafuatulia malipo hayo, awali tuliambiwa tujaze fomu za kuonesha uhitaji wetu wa malipo hayo lakin juzi tumepewa majibu yaliyotolewa kwa barua, yametukatisha tamaa.

Tumejibiwa na Mkurugenzi kuwa tutapatiwa endapo hali ya kifedha itakapotengemaa, sasa tunajiuliza lini hali ya kiuchumi itakaa sawa?

Tunaomba kilio chetu kifike kwa Wizara ya Afya kuwa Watumishi tunahitaji malipo hayo kwa kuwa tunajua ni haki yetu, watusaidie kupata, yatatusaidia kujikimu kwani wengi wetu ndio kwanza tunaanza maisha na tulitarajia kutumia kulipa kodi na mahitaji mengine ya msingi.
Mishahara mnalipwa? Kama mnalipwa pigeni kazi
 
Barua imeandikwa kikatiri sanaaa inaonyesha uliandika essay afu wahuni wamejibu easy sana
 
Kwanza shukuru umepata ajira, hayo mengine ni madogo maadamu umejibiwa kuwa utalipwa, endelea kuchapa kazi.
 
Sisi Watumishi wa Umma ambao ni waajiriwa wapya Serikalini katika Kada ya Afya, Halmashauri ya Kilosa Mkoani Morogoro tuna changamoto ya kutolipwa stahiki zetu za fedha za kujikimu na majibu tunayopewa yanatukatisha tamaa.

Huu ni mwezi wa tatu sasa tunafuatulia malipo hayo, awali tuliambiwa tujaze fomu za kuonesha uhitaji wetu wa malipo hayo lakin juzi tumepewa majibu yaliyotolewa kwa barua, yametukatisha tamaa.

Tumejibiwa na Mkurugenzi kuwa tutapatiwa endapo hali ya kifedha itakapotengemaa, sasa tunajiuliza lini hali ya kiuchumi itakaa sawa?

Tunaomba kilio chetu kifike kwa Wizara ya Afya kuwa Watumishi tunahitaji malipo hayo kwa kuwa tunajua ni haki yetu, watusaidie kupata, yatatusaidia kujikimu kwani wengi wetu ndio kwanza tunaanza maisha na tulitarajia kutumia kulipa kodi na mahitaji mengine ya msingi.
Vijana amjui ethics za kazi ndo nini sasa hiki ungeweka lalamiko bila kiambatanisha barua ingekuwa poa sana . Hizo pesa utalipwa kikubwa si uliomba ajira ? Kama unajiweza kaendelee na mishe zako mtaani huko
 
Vijana amjui ethics za kazi ndo nini sasa hiki ungeweka lalamiko bila kiambatanisha barua ingekuwa poa sana . Hizo pesa utalipwa kikubwa si uliomba ajira ? Kama unajiweza kaendelee na mishe zako mtaani huko
Habari bila picha hainogi mkuu
 
Yaani sio halmashauri ya Kilosa tu tunateseka kwakweli, na ilitakiwa tupewe pesa ya kujikimu ndio twende kazini huko na sio halmashauri moja ni zote tunateseka na hapa mishahara yote hatujapewa toka Novemba

Wanategemea usafiri, usafirishe watoto ufike ulipe kodi, ununue matumizi kwa huo huo mshahara wakati hiyo ilikuwa pesa ya kujikimu tupewe kwa matumizi hayo yaani ufanye kila kitu kwa mshahara mmoja wa mwezi kweli?

Mpaka sasa watu wanateseka wengine mpaka wanatamani kuacha kazi pesa ya shida wamefikia sehemu hakuna nyumba maji wala internet wala huduma za kijamii lakini wanataka hiyo pesa ifanye mambo yote hayo jamani. Hapana ni mateso

Barua zenyewe hatupewi za kuomba mishahara yetu iliyopita, pesa za kujikimu mpaka sasa halmashauri na makatibu wapo kimya sijui wanategemea tuishi vipi halafu wategemee kuwa hawa watumishi watahudumia kwa weledi jamii kweli?

Sidhani.
 
Back
Top Bottom