Jinsi 'Made in China' ilivyowapoteza wafanyabiashara wengi Tanzania na Afrika

Mar 23, 2023
83
100
Hebu tuchambue vipi "MADE IN CHINA" imeleta taharuki na dhana potofu hadi watu wanahangaika bila sababu na kupoteza pesa Nyingi. 🤔


1. Mfano mzuri ni ving’amuzi vya Azam TV! Ving’amuzi vya Azam vina lebo ya “Made in China,” lakini ukifika China hutavikuta madukani hata ukahangaika vipi, na wakati mwingine hata wafanyabiashara huko hawajui.


Kwanini? Kwa sababu mali yenyewe ni ya Azam, kampuni ya nyumbani Tanzania. Wanavitengeneza kwa specifications zao huko China wanapo pajua wao , lakini umiliki na uendeshaji ni wa Tanzania.

Hivyo, chukua hili na ulinganishe na bidhaa nyingine—hii siyo pekee iliyopo kwenye mfumo huo !

2. Changamoto ni kuwa… Watu wengi wanadhani ili wapate bidhaa fulani bora kwa bei nafuu, lazima wasafiri mbali kama China au nchi nyingine au kuzani kila kitu wanavho kiona kwenye masoko yao basi na wao wanaweza kikifata na kukipata china, wakidhani kuwa kila kitu kilicho “Made in China” lazima kitapatikana huko.

Lakini zipo bidhaa “Made in China” ambapo kampuni husika iko nchini nyingine, kama Italia, na bidhaa zinafaniyika China lakini usambazaji unaendeshwa kwa njia maalum. Hii ina maana, kuagiza bidhaa nje ya mfumo rasmi inaweza kukupeleka kwenye bidhaa feki au matatizo ya haki miliki, ambayo yanaweza kutumika dhidi yako.

3. Kwa mfano, kuna wafanyabiashara wengi ambao husafiri kutafuta vitu kama vifaa vya umeme, nguo, au simu, bila kujua kuwa kuna bidhaa nyingi Made in China zinazomilikiwa na Wakenya, Watanzania, au Wauganda. Hii inamaanisha kuwa wanaenda China na kurudi mikono mitupu, wakati kumbe bidhaa hizo zipo na zinaweza kupatikana hapa kwenye soko letu.


4. Hii ni changamoto kubwa kwa wafanyabiashara wanapojaribu kufuata bidhaa zinazozunguka "Made in China." Mfano mmoja mzuri ni story ya wafanyabiashara waliokwenda China kutafuta bidhaa za Oraimo. 🎧 Walijua Oraimo ni brand maarufu inayotengenezwa China, na walijiamini kuwa wataweza kuagiza bidhaa moja kwa moja kutoka huko. Lakini, waliporudi na makontena ya bidhaa hizo, walijikuta wakiwa na bidhaa za fake, na bidhaa zao zikakamatwa kwa tuhuma za uuzaji wa bidhaa feki.

5. Nini kilitokea? Oraimo, ingawa inatengenezwa China (hasa Hong Kong), ina supply policy kali. Wanapeleka bidhaa zao kupitia mawakala wao waliothibitishwa tu katika nchi husika, na wateja wengi wanaohudumia bidhaa za Oraimo ni mawakala hao pekee. Hivyo, ukienda China, hautapata bidhaa halisi za Oraimo moja kwa moja, bali utahitaji kupitia wakala wa kisheria aliyeidhinishwa. Hii inawafanya wafanyabiashara wengi kujikuta wakiagiza high copy za bidhaa na kupoteza hela nyingi, kwa sababu walikosa maarifa ya mfumo wa usambazaji.

Kuna watu ambao wamewahi kunionyesha bidhaa za Oraimo kwenye Alibaba.com na kuniambia "ona Zinapatikana kwa bei rahisi sana", lakini ukweli ni kwamba bidhaa hizi ni fake zote kwenye mtandao huo , akuna bidhaa ya oraimo humo original and genuine. Wakati mwingine, huwezi kupata bidhaa halisi za Oraimo kutoka kwenye majukwaa kama hayo.


6. Ushauri kwa wafanyabiashara wote: Kabla hujaamua kuagiza au kusafiri kwa bidhaa, tafuta taarifa kamili kwanza! Hii itakusaidia kujua kama bidhaa hiyo tayari ipo nchini kwako au inapatikana kwa wakala wa nyumbani. Inaweza kukuokoa muda, gharama, na kukufanya ufanye biashara kwa ufanisi zaidi. Tafuta kwa kina, uliza wenye uzoefu, na utafanya maamuzi bora zaidi!

7. Mwisho wa siku: “Made in China” haimaanishi lazima ukasafiri huko kupata kila kitu. Hakikisha unafanya due diligence na unajua sera za usambazaji za bidhaa ili kuepuka changamoto za biashara na kuhakikisha unapata bidhaa bora kwa wateja wako!

Unapojipanga kuingia kwenye uhuzaji wa bidhaa yoyote, hasa kwenye miradi mikubwa, Market Intelligence lazima ifanye kazi. Hii ni muhimu ili kuhakikisha unapata taarifa sahihi, unafanya uamuzi bora, na unafika kwenye lengo lako bila kupoteza rasilimali. Nipo hapa kukusaidia kuhakikisha kampuni yako inafikia malengo yake kwa ufanisi, kama vile Russia’s hypersonic missile – lengo kubwa, hatua thabiti, mafanikio yaliyothibitishwa.

By Mrndumbarojl
0626201416
 
Kwa sasa hivi wachina ni wengi sana hapa mjini.

Biashara nyingi zitaathirika kwa kweli kama watakuwa na uwezo wa kufanya kola kitu kama wazawa.
 
Umeandika kisomi na sio kimtaani(practical)
Binafsi nafanya biashara kkoo,bidhaa zote zenye mawakala zinafahamika na wakala anajulikana.
Wanaoenda china sio kwamba hawajui kama ulivyosema,wanajua vizuri kwamba wanaenda kutengeneza copy/fake ya bidhaa husika ili kutengeneza faida kubwa kwa muda mfupi.

Seala la kukamatwa ni katika risk za kawaida katika utafutaji,bidbaa copy zipo na zinaigia nyingi kila uchwao.
Tatizo kubwa ni wabongo kupenda kitu kizuri kwa bei ndogo.
 
Soma kichwa cha uzi . hata mimi najua wanajua ila wapo watu wengi hasa wafanya biashara wa kati wanahamasishwa kununua na kutafuta vitu china bila kua na prior Intelligence kama uliyo nayo wewe. na wengine utumia watu ambao they don't tell them the truth kua wataletewa bidhaa copy au ualisia wa soko upoje. kuhusu kufanya biashara kariakoo hata mimi nafanya kaka. ila upo sahihi
 
Nashukuru sana kwa elimu hii nzuri na muhimu kwa ustawi wa biashara zetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…