briophyta plantae
Senior Member
- Feb 18, 2017
- 114
- 129
Umeupiga mwingi sana mkuu. You are the true son of Arusha. Arusha ya miaka ya 2000 mwanzoni ilikuwa kituko. Barabara za mitaani zilikuwa vumbi tupu. Hapo kwenye jengo la NSSF karibu na roundabout florida kulikua patupu. Hali ilikuwa mbaya sana.Licha ya changamoto ulizozitaja ni vyema pia kufahamu nchi yetu bado ni maskini na kama serikali inajitahidi sana kuboresha miundombinu kwa usawia katika mikoa yote ndio maana unaona mpanda na sumbawanga kuna stendi nzuri kuliko Arusha kwa vile nao ni sehemu ya Tanzania nao wanastahili stendi za kisasa, tangu uhuru kuna miji hadi leo stendi zao ni za vumbi ikiwemo bukoba, musoma na mtwara ila arusha stendi ya sasa hivi ilifanyiwa ukarabati mkubwa sana mwaka 2003 tu kiserikali ni karibuni sana bado arusha kuna kumbi za kimataifa + taasisi nyingi mikoa mingine nao pia wana haki ya kujiskia watanzani
Tayari wako kwenye kufunga taa mitaa yote ya mjini na camera ili mji uwe smart city
Ukiachana na Daresalaam na Dodoma kutokana na umuhimu wake miji yote iliyobaki inachangamoto zinazofanana lakini kwa sisi tunaoijua arusha ni mashuhuda pia wa kazi kubwa serikali iliyofanya arusha kwa kipindi hichi kifupi tu cha ndani ya miaka 10 tu tangu 2014 hadi leo 2024
1. Sakina Tengeru dual carriage way moja ya barabara za kisasa mno nchini km 14
2.Arusha bypass km 42
3.Ujenzi wa barabara mpya 27km ukizijumlisha zinafika 100km ndani ya miaka 10 tu na hii na Arusha jiji sio wilaya zake
4.Mradi wa maji wa bilioni 520 ambao hata makao makuu dodoma hawakupendelewa mradi mkubwa kama huu + Maji taka na dampo la kisasa
5.Uboreshwaji wa uwanja mdogo wa ndege Arusha licha ya kuwa Arusha inahudumiwa na KIA kwa usafiri wa kimataifa km 40 kutoka arusha lakini uwanja mdogo wa arusha ulikua ni aibu njia ya kuingia uwanjani ilikua ni vumbi kulikua hamna hata sehemu ya kupumzika abiria leo umeongezwa na hata air Tanzania inatua
Kwa hiyo hatua iliyopigwa ni kubwa mno na bado kuna mikakati na miradi iliyokwishasainiwa ambayo naimani ndani ya miaka 10 mingine tutakua Tumefika mahali pazuri,
kujibu hoja zako ulizoainisha
1.Mipango miji tayari viwanja vyote vimepimwa na kutakua na satellite city 3 au zaidi ikiwemo afcon City ambayo ilisemwa kwenye bajeti, safari city ya nhc na bondeni city
2. Uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu wa samia pamoja na Indoor arena
3. Upanuzi wa barabara ya Arusha kisongo kuwa njia nne
4. Tayari Latra wameshatangaza daladala zile za mjini ziwe na abiria kuanzia 30 na hizo ndogo zote zimalizie tu mda wake
5. Themi living garden bustani ya aina yake mkataba umeshasainiwa
6.Stendi mpya ya Arusha mkataba umeshasainiwa
7.Stendi ya kilombero kama ulivoitaja mkataba umesainiwa na renders zipo
8..Nyamachoma kwa morombo napo ujenzi wake umeshasainiwa
9.Kuna barabara nyingine zipo pia kwenye ujenzi na design ya kuleta SGR na mwendokasi BRT kwa siku za usoni umeshasanifiwa
10. Sekta ya Afya hospital zimejegwa sana pia Sekta binafsi
Kwa tunaoijua Arusha ilipotoka serikali imefanya jitihada kubwa sana naamini kama ungefika Arusha zaidi ya miaka 10 iliyopita leo ungeona mabadiliko makubwa
Naiona Tanzania πΉπΏ ikichanua sana kwa siku za mbeleni kwa hii miji 10 ya Dodoma, Dar,Zanzibar, Mbeya, Kahama,Arusha, Morogoro, Iringa,Tanga na Mwanza huko kote kuna miradi mikubwa ambapo naamini ndani ya miaka 10 nchi yetu itakua ni ya kutembelewa π
Update:Umeupiga mwingi sana mkuu. You are the true son of Arusha. Arusha ya miaka ya 2000 mwanzoni ilikuwa kituko. Barabara za mitaani zilikuwa vumbi tupu. Hapo kwenye jengo la NSSF karibu na roundabout florida kulikua patupu. Hali ilikuwa mbaya sana.
Nimeondoka Arusha miaka mingi. Niliacha lami imeishia njiapanda ya kwenda Nalopa school kwenye ile sheli. Sasa hivi imefika wapi?Update:
1.Kuna ujenzi wa uwanja mkubwa unakuja wa zaidi ya billion 200
2.Barabara ya esso paloti annex ujenzi unaanza mwaka huu
Nafurah kuona kuna vijana wanaotambua kujenga hoja sio lazima kukosoa kila hatua ya serikali na wengi hawajui hali ya arusha ilivyokua tulipotoka na tulipo sasa kuna wakati ili uone lami ilikua lazima uende mjini tena vimitaa michache tu kipindi hicho walami na sisi wengine wa mavumbini le hii arusha njiro kule lami inaenda hadi sehemu ambayo hamna makazi ya watu atomic kule ni hatua kubwa sana. π
Kweli arusha unaijuaNimeondoka Arusha miaka mingi. Niliacha lami imeishia njiapanda ya kwenda Nalopa school kwenye ile sheli. Sasa hivi imefika wapi?
Duh balaa. Ina maana watu wa Mkonoo wamefikiwa.Kweli arusha unaijua
Sasa lami imeendelea hadi sehemu inaitwa kwa msola ikaendelea hadi kwa masista hadi sehemu inaitwa atomic na ni barabara ya kiwango inanjia za waenda kwa miguu na taa za barabarani usiku kama mchana
Katikati yake pale kwa msola inapita barabara ya bypass maarufu kama east africa kuanzia usa inapita njiro kwa morombo kisongo inakuja kutokea ngaramtoni km42 nayo ni lami tena ya kiwango sana
Mji Tanzania hii ni Dodoma na angalau TangaMiji ya Tanzania yote ni hovyo na Ina Changamoto hizo hizo ukitoa Dodoma na Dar Kwa kiasi Fulani.
View: https://www.instagram.com/reel/C9PRYJFszTS/?igsh=MWxpc2Zhd3c2M2Jpdg==
Mkono sasa hivi ni mjini brother bei ya viwanja kule haishkiki kuna matajiri balaa kipindi kile ulikua ukisema mkonoo ilikua kama unaongelea mkoa mwingine ilikua ni mbali mno lakin leo imekua katikati ya nyumba za matajiri mkonoo ya leo ni ndani ya jijiDuh balaa. Ina maana watu wa Mkonoo wamefikiwa.
Umaarufu na Changamoto ni bangi na rizzla.Arusha ni jiji lenye hadhi yake ya kipekee katika nchi yetu.kwanza ni jiji la kitalii na pili lina utamaduni wake wa kipekee sana.
Changamoto ipo katika mtazamo kabla hujalifikia hili jiji,picha unayokuwa nayo kichwani ni kwamba arusha ni mji mzuri sana,uliostaarabika sana na wenye elimu,biashara na ubunifu wa kibiashara,mpangilio mji na usafi,watalii kibao n.k
Nilikuwa arusha kwa siku tatu juzi tu na kwakweli ni mkoa wa kipekee sana ila ndo hvyo kila kizuri hakikosi kasoro:
KWA MOROMBO kwenye nyama choma. Asee hii sehemu ni maarufu sanaa,hata nikiwa mbeya,dar na mwanza nilikuwa nikipasikia sanaa, na nyama inachomwa sana hapa,ila pako local vibaya mnoo, na hivi vi mvua mvua aisee ni kuchafu sanaa. Hii sehemu kwa heshima na umaarufu wake nashauri tu pangeandaliwa mazingira yake yawe mazuri na ya kipekee hata kwenye AFCON patakuwa na wageni wengi sana hapa nina uhakika.
SOKO LA KILOMBERO: Moja ya eneo ambalo ustaarabu ni sifuri ni hapa kilombero,hapana mpangilio wa kitu chochote, foleni, uchafu, miundombinu, maji taka ndo usiseme,mikokoteni,bodaboda n.k. Hapo hapo kuna kama mall kubwa tu(wanapaita TFA) na supermarket ya maana kabisa (shopers) watalii wanapishana hapo ni kuingia na kutoka ila hayo mazingira sijui yanaleta picha gani. Serekali isaidie kufanya namna hapa maana hata hiyo barabara ukiiona.
DALADALA: Daladala za huku unaingia mzima tu, ila unashuka ukiwa unachechemea,huko ndani ni kubanwa,kukunjwa,kupangwa yani tafrani. Kwa jiji kama Arusha hapana aisee hii sio sawa kuwa na vigari kama hv eti ndio usafiri wa umma. Kwanza ndio vinafanya foleni inakuwa kubwa na ni vibovu hatari, ANGALIZO:-bajaji nazo ni zakuwekewa mipaka,mtakuja kuona umuhimu wake
MIPANGO MIJI: Hawa watu huwa sijuagi kazi yao hasa ni nini maana hii miji hata kupagwa inapangwa sasa,watu wanajenga shaghalabagala,hata ukija katikati ya mji kuna nyumba za ajabu ajabu.kuna kipindi nilikuja tena arusha, hapa kaloleni kulikuwa kuna mtaa unaitwa magorofani,saiv yale majengo wamebomoa halafu what next πππ hakuna kitu kinafanyika pale, watu wanapaki magari tu na kuna bar wanalewa kuanzia asubuhi mpaka jioni.ukija ule mtaa wa kaloleni nyuma ya polisi kwenda tank la maji,wamebomoa zile nyumba zote za kizamani ila hapajaendelezwa chochote,kumekuwa msitu tu, siongelei ungaltd wala ngarenero,nipaache tu.
MIUNDOMBINU: Barabara nyingi ni mbovu sana na pia haziwezi kumudu ongezeko la matumizi ya barabara kwa sasa, magari ni mengi, parking hakuna so watu wanapaki barabarahi tu na kusababisha foleni zisizo za lazima, miferiji ya maji mingi imeziba na michafu mnoo, huko Sakina, Ngaramtoni, Mianzini, Ungaltd hakuna barabara za mitaa ile ni mito ya kupitisha maji.
Samaki mkunje angali mbichi,huu mji unazidi kukua,kama ni kubadili baadhi ya mambo kuuweka mji uwe sawa na maridadi muda ni sasa,huko mbeleni kazi itakuwa ni ngumu haswa kukishaharibika kabisa.
Nawasilisha kwenu.
View attachment 3038376
View attachment 3038377
Tatizo la nchi hii ni ccm TU!Arusha ni jiji lenye hadhi yake ya kipekee katika nchi yetu.kwanza ni jiji la kitalii na pili lina utamaduni wake wa kipekee sana.
Changamoto ipo katika mtazamo kabla hujalifikia hili jiji,picha unayokuwa nayo kichwani ni kwamba arusha ni mji mzuri sana,uliostaarabika sana na wenye elimu,biashara na ubunifu wa kibiashara,mpangilio mji na usafi,watalii kibao n.k
Nilikuwa arusha kwa siku tatu juzi tu na kwakweli ni mkoa wa kipekee sana ila ndo hvyo kila kizuri hakikosi kasoro:
KWA MOROMBO kwenye nyama choma. Asee hii sehemu ni maarufu sanaa,hata nikiwa mbeya,dar na mwanza nilikuwa nikipasikia sanaa, na nyama inachomwa sana hapa,ila pako local vibaya mnoo, na hivi vi mvua mvua aisee ni kuchafu sanaa. Hii sehemu kwa heshima na umaarufu wake nashauri tu pangeandaliwa mazingira yake yawe mazuri na ya kipekee hata kwenye AFCON patakuwa na wageni wengi sana hapa nina uhakika.
SOKO LA KILOMBERO: Moja ya eneo ambalo ustaarabu ni sifuri ni hapa kilombero,hapana mpangilio wa kitu chochote, foleni, uchafu, miundombinu, maji taka ndo usiseme,mikokoteni,bodaboda n.k. Hapo hapo kuna kama mall kubwa tu(wanapaita TFA) na supermarket ya maana kabisa (shopers) watalii wanapishana hapo ni kuingia na kutoka ila hayo mazingira sijui yanaleta picha gani. Serekali isaidie kufanya namna hapa maana hata hiyo barabara ukiiona.
DALADALA: Daladala za huku unaingia mzima tu, ila unashuka ukiwa unachechemea,huko ndani ni kubanwa,kukunjwa,kupangwa yani tafrani. Kwa jiji kama Arusha hapana aisee hii sio sawa kuwa na vigari kama hv eti ndio usafiri wa umma. Kwanza ndio vinafanya foleni inakuwa kubwa na ni vibovu hatari, ANGALIZO:-bajaji nazo ni zakuwekewa mipaka,mtakuja kuona umuhimu wake
MIPANGO MIJI: Hawa watu huwa sijuagi kazi yao hasa ni nini maana hii miji hata kupagwa inapangwa sasa,watu wanajenga shaghalabagala,hata ukija katikati ya mji kuna nyumba za ajabu ajabu.kuna kipindi nilikuja tena arusha, hapa kaloleni kulikuwa kuna mtaa unaitwa magorofani,saiv yale majengo wamebomoa halafu what next πππ hakuna kitu kinafanyika pale, watu wanapaki magari tu na kuna bar wanalewa kuanzia asubuhi mpaka jioni.ukija ule mtaa wa kaloleni nyuma ya polisi kwenda tank la maji,wamebomoa zile nyumba zote za kizamani ila hapajaendelezwa chochote,kumekuwa msitu tu, siongelei ungaltd wala ngarenero,nipaache tu.
MIUNDOMBINU: Barabara nyingi ni mbovu sana na pia haziwezi kumudu ongezeko la matumizi ya barabara kwa sasa, magari ni mengi, parking hakuna so watu wanapaki barabarahi tu na kusababisha foleni zisizo za lazima, miferiji ya maji mingi imeziba na michafu mnoo, huko Sakina, Ngaramtoni, Mianzini, Ungaltd hakuna barabara za mitaa ile ni mito ya kupitisha maji.
Samaki mkunje angali mbichi,huu mji unazidi kukua,kama ni kubadili baadhi ya mambo kuuweka mji uwe sawa na maridadi muda ni sasa,huko mbeleni kazi itakuwa ni ngumu haswa kukishaharibika kabisa.
Nawasilisha kwenu.
View attachment 3038376
View attachment 3038377