Jeshi la Polisi Morogoro lawakamata maofisa saba wa LBL kwa tuhuma za biashara haramu ya fedha

the guardian 17

JF-Expert Member
Aug 15, 2024
334
489
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limewakamata watu saba wanaodaiwa kuendesha biashara haramu ya fedha mtandaoni bila kibali cha Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Soma pia: Jeshi la polisi Mbeya limewakamata watu watano kwa kuhusika na mchezo wa upatu wa LBL

Watuhumiwa hao ni wawakilishi wa kampuni ya Leo Beneth London (LBL), wakifanya shughuli zao katika Manispaa ya Morogoro na Turiani, Mvomero.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Alex Mkama akizungumza leo Alhamisi, Februari 20, 2025 amesema waliwakamata watuhumiwa hao Februari 18, 2025, Kilakala, Manispaa ya Morogoro wakiwa na vifaa vinavyohusiana na biashara hiyo.

Watuhumiwa ni David Francis (35), Boazi Amboniye (42), Kundi Msalaba (31), Moses Dugomela (22), Isaya Paulo (25) na Baraka Sanga (32).

Msako huo umefanyika kwa kushirikiana na BoT, ikiwa ni sehemu ya kudhibiti utapeli wa fedha kupitia mitandao ya simu na teknolojia nyingine za kifedha.

Source: MwananchiDigital
 
Mbona kwa kuwakamata hao jamaa ni kama wamewakomoa wananchi waliowekeza pesa zao huko yaani ndio wame waharibia kabisa raia maana kabla ya kuwakamata hao jamaa ina maana wanachama walikuwa wanapokea gawio lao.? kwa polisi kuwakamata washika mkoba wa fedha hapo wanachama hawapati pesa tena..sasa kifuatacho ni kilio na kusaga meno maana polisi wameongeza tatizo zaidi..kwanza hao polisi walikuwepo wapi siku zote wasiwakamate ni zaidi ya miezi 6 hao jamaa wapo tena wakijitangaza kwenye TV na mitandaoni why hawajawauliza kuhusu leseni toka BOT.!
 
Mbona kwa kuwakamata hao jamaa ni kama wamewakomoa wananchi waliowekeza pesa zao huko yaani ndio wame waharibia kabisa raia maana kabla ya kuwakamata hao jamaa ina maana wanachama walikuwa wanapokea gawio lao.? kwa polisi kuwakamata washika mkoba wa fedha hapo wanachama hawapati pesa tena..sasa kifuatacho ni kilio na kusaga meno maana polisi wameongeza tatizo zaidi..kwanza hao polisi walikuwepo wapi siku zote wasiwakamate ni zaidi ya miezi 6 hao jamaa wapo tena wakijitangaza kwenye TV na mitandaoni why hawajawauliza kuhusu leseni toka BOT.!
Wapigwe tu
Haya makampuni ya kitapeli siyo mageni wananchi mbona hawajifunzi?
 
Mbona kwa kuwakamata hao jamaa ni kama wamewakomoa wananchi waliowekeza pesa zao huko yaani ndio wame waharibia kabisa raia maana kabla ya kuwakamata hao jamaa ina maana wanachama walikuwa wanapokea gawio lao.? kwa polisi kuwakamata washika mkoba wa fedha hapo wanachama hawapati pesa tena..sasa kifuatacho ni kilio na kusaga meno maana polisi wameongeza tatizo zaidi..kwanza hao polisi walikuwepo wapi siku zote wasiwakamate ni zaidi ya miezi 6 hao jamaa wapo tena wakijitangaza kwenye TV na mitandaoni why hawajawauliza kuhusu leseni toka BOT.!
Sahihi kabisa, Kuna videos U- tubes zinaonesha hadi baadhi ya viongozi wa serikali wakiwahamasisha watu wajiunge , Tena ITV wametangaza
Je jeshi la police walikuwa wapi kuzuia hilo , watu wamejiunga na wanapokea Fidia zao bila shida kama hawakufata utaratib wa BoT tu ila lessen wanazozo za Biashara why wawafungie ili wananchi waasilike , mm nipo Dar Kuna office za LBL kibao na zingine zipo karibu na police jiran kabisa, KUNA MAMBO POLICE WANATUPA UKAKASI .
 
Sahihi kabisa, Kuna videos U- tubes zinaonesha hadi baadhi ya viongozi wa serikali wakiwahamasisha watu wajiunge , Tena ITV wametangaza
Je jeshi la police walikuwa wapi kuzuia hilo , watu wamejiunga na wanapokea Fidia zao bila shida kama hawakufata utaratib wa BoT tu ila lessen wanazozo za Biashara why wawafungie ili wananchi waasilike , mm nipo Dar Kuna office za LBL kibao na zingine zipo karibu na police jiran kabisa, KUNA MAMBO POLICE WANATUPA UKAKASI .
MKipewa maelezo hua mnakua wabishi sana. Tuendelee tu hivihivi
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limewakamata watu saba wanaodaiwa kuendesha biashara haramu ya fedha mtandaoni bila kibali cha Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Soma pia: Jeshi la polisi Mbeya limewakamata watu watano kwa kuhusika na mchezo wa upatu wa LBL

Watuhumiwa hao ni wawakilishi wa kampuni ya Leo Beneth London (LBL), wakifanya shughuli zao katika Manispaa ya Morogoro na Turiani, Mvomero.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Alex Mkama akizungumza leo Alhamisi, Februari 20, 2025 amesema waliwakamata watuhumiwa hao Februari 18, 2025, Kilakala, Manispaa ya Morogoro wakiwa na vifaa vinavyohusiana na biashara hiyo.

Watuhumiwa ni David Francis (35), Boazi Amboniye (42), Kundi Msalaba (31), Moses Dugomela (22), Isaya Paulo (25) na Baraka Sanga (32).

Msako huo umefanyika kwa kushirikiana na BoT, ikiwa ni sehemu ya kudhibiti utapeli wa fedha kupitia mitandao ya simu na teknolojia nyingine za kifedha.

Source: MwananchiDigital
Jeshi la Polisi badala ya kushughulikia masuala ambayo yapo serious wao wanahangaika na 'petty issues,' Wananchi wengi zaidi tunataka kuona kwamba Jeshi la Polisi linashughulika na Mambo ambayo ni nyeti kabisa yanayohatarisha Usalama wa Umma/Watu kama vile janga hili la Utekaji Watu, suala ambalo linawakosesha usingizi Watu wengi Sana na kuondoa kabisa amani katika nafsi miongoni mwa Wananchi wengi zaidi hapa Tanzania.
 
Sahihi kabisa, Kuna videos U- tubes zinaonesha hadi baadhi ya viongozi wa serikali wakiwahamasisha watu wajiunge , Tena ITV wametangaza
Je jeshi la police walikuwa wapi kuzuia hilo , watu wamejiunga na wanapokea Fidia zao bila shida kama hawakufata utaratib wa BoT tu ila lessen wanazozo za Biashara why wawafungie ili wananchi waasilike , mm nipo Dar Kuna office za LBL kibao na zingine zipo karibu na police jiran kabisa, KUNA MAMBO POLICE WANATUPA UKAKASI .
Vichwa vyenu ni vya kitoto sana ...hivi amjui kuwa mara nyingi polisi wakigundua njama za ujambazi wa pesa nyingi kabla ya kufanyika basi ungoja hadi tukio litokee kwanza ? Mnajua kwa nini ? Sababu ni kwamba nao watakomba pesa zilizo mikononi mwa wahalifu....mfano majambazi yakizibitiwa kabla ya kupora milioni 300 polisi awawezi kupata kitu...ila pesa zikisha porwa na kuwa mikononi mwa wahalifu hapo ndipo polisi wakizi kamata ukwapua na wao hata milioni 200 kisha milioni 100 ndiyo udaiwa kipatikana ...Sasa hiyo LBL ni hivyo hivyo kwa vyombo usika zilichelewesha kuwakamata ili vinufaike na pesa za wananchi wapumbavu walizo kusanya LBL
 
Sahihi kabisa, Kuna videos U- tubes zinaonesha hadi baadhi ya viongozi wa serikali wakiwahamasisha watu wajiunge , Tena ITV wametangaza
Je jeshi la police walikuwa wapi kuzuia hilo , watu wamejiunga na wanapokea Fidia zao bila shida kama hawakufata utaratib wa BoT tu ila lessen wanazozo za Biashara why wawafungie ili wananchi waasilike , mm nipo Dar Kuna office za LBL kibao na zingine zipo karibu na police jiran kabisa, KUNA MAMBO POLICE WANATUPA UKAKASI .
Kama ulikuwepo Dar miaka ya 2008,2009 kulikuwa na kampuni iliitwa DECI. Hiyo ilikuwa inatangazwa makanisani lakini walikuwa matapeli
 
Jeshi la Polisi badala ya kushughulikia masuala ambayo yapo serious wao wanahangaika na 'petty issues,' Wananchi wengi zaidi tunataka kuona kwamba Jeshi la Polisi linashughulika na Mambo ambayo ni nyeti kabisa yanayohatarisha Usalama wa Umma/Watu kama vile janga hili la Utekaji Watu, suala ambalo linawakosesha usingizi Watu wengi Sana na kuondoa kabisa amani katika nafsi miongoni mwa Wananchi wengi zaidi hapa Tanzania.
Kwa hiyo huamini kama LBL ni utapeli
 
Mbona kwa kuwakamata hao jamaa ni kama wamewakomoa wananchi waliowekeza pesa zao huko yaani ndio wame waharibia kabisa raia maana kabla ya kuwakamata hao jamaa ina maana wanachama walikuwa wanapokea gawio lao.? kwa polisi kuwakamata washika mkoba wa fedha hapo wanachama hawapati pesa tena..sasa kifuatacho ni kilio na kusaga meno maana polisi wameongeza tatizo zaidi..kwanza hao polisi walikuwepo wapi siku zote wasiwakamate ni zaidi ya miezi 6 hao jamaa wapo tena wakijitangaza kwenye TV na mitandaoni why hawajawauliza kuhusu leseni toka BOT.!
Mimi niweke wazi kwa nini watu Wana chukua maamuzi magumu,kwa watumishi wa umma BOT imebariki mambo mengi ya ajabu kinyume na ILO,imagine alipoingia mwenda zake aliondoa malipo yafuatayo
1.Pesa ya likizo
2.Overtime
Na nyingine nyingi,kuanzia hapo watumishi wameishi kama njiwa tunduni,hatimae akaja kula kwa ulefu wa kamba yako.
Hakuna uwiano mzuri kati ya wanasiasa na watumishi wa kawaida.
Nimeshuhudia Miradi ya kimkakati inaisha na hakuna BOT ofisa aliehangaika kurudisha haki za watumishi wa umma,hizi haki sio za ajabu,ukiwa kazini huwezi wekeza mradi wa biashara na ukawa salama,lazima ufirisike.sababu muda mwingi unatumikia umma,sasa wafanyabiashara hawana lao pia isipokuwa mafisadi wanaochota pesa za umma ndo wenye nguvu kuwekeza kwa uwiano mkubwa na kufaidi keki ya taifa mbele na nyuma,hii mambo inaumiza sana,ukijenga unavurugwa na mafundi,sababu muda mwingi uko kazini.
LBL ni Moja ya uwekezaji tumekuwa na nguvu kudhibiti na kipato Kiko vizuri,shida ni mafisadi wameona watu wa kimaskini wanakwenda kupata uhuru wa kiuchumi sasa bot imepiga Pini,kwanini bot haijajiuliza mbona watu wanaohangaika nao ni wale wa chini kabisa sababu hata vijisenti vilivyo huko ni kiasi cha Tsh 100,000/- laki,150,000/- Hawa ni watu wa kawaida kabisa,wanatafuta mkate tuu.
Majizi makuu yako huko huko kwenye urefu wa kamba,Miradi ya kimkakati inaisha kwanini msiwape pesa za likizo wenye sifa,baya zaidi wizi mwingine ni bajeti hewa.Hakuna mafungu kabisa sasa mnaumiza watu wa chini na kodi mnakusanya na bado mambo yenu hatuyaoni,BOT NI TAWI la siasa chafu za Tanzania.
Kuna Kampuni kibao zimeuliwa,sababu kuu ni utitili wa regulators na moja wapi ni kuhakikisha watu wanateseka,mbona mnatuchanganya.
 
Kama ulikuwepo Dar miaka ya 2008,2009 kulikuwa na kampuni iliitwa DECI. Hiyo ilikuwa inatangazwa makanisani lakini walikuwa matapeli
Kwani Hawa OYA nao unawaonaje.mkuu,hata haya makamouni ya kubahatisha yameweka
makopo ya kamali kila Kona wewe unaonaje,shida njaa zetu ndo zinatutesa.Kila Kona shida tuu.
 
Jeshi la Polisi badala ya kushughulikia masuala ambayo yapo serious wao wanahangaika na 'petty issues,' Wananchi wengi zaidi tunataka kuona kwamba Jeshi la Polisi linashughulika na Mambo ambayo ni nyeti kabisa yanayohatarisha Usalama wa Umma/Watu kama vile janga hili la Utekaji Watu, suala ambalo linawakosesha usingizi Watu wengi Sana na kuondoa kabisa amani katika nafsi miongoni mwa Wananchi wengi zaidi hapa Tanzania.
Kutapeliwa wananchi ni petty issue? Hizi akili ni za wafuasi wa tundu
 
Back
Top Bottom