Je, WCB inaenda kuzaliwa upya au inaelekea kwenye kifo?

GadoTz

JF-Expert Member
Nov 20, 2014
370
636
WCB moja ya lebo zilizofanya vizuri na wanaendelea kufanya vizuri kwenye kiwanda cha muziki Tanzania na hata nje ya mipaka.

Ila hapa kati ni kama lebo ilianza kudorola haswa baada ya kuondoka wasanii wao powerful, Harmonize na Rayvanny.

Ile nguvu ya WCB kuisikia kila kona ya nchi imepungua sana.

Walau Zuchu na Mbosso ndio walibaki kama mihimili ya lebo.

Sasa nimesikia Mbosso tayari kaondoka Wasafi na washamalizana na Diamond yupo huru.

Pia Lavalava mkataba wake umefika mwisho muda wowote wanamalizana na WCB.

Kwa mantiki hiyo Wasafi itabaki na wasanii wawili, Zuchu na D Voice ambae hafanyi vizuri bado. Kwa kifupi WCB ipo kwenye kilele kinachofata ni kudondoka.

Sasa ili isidondoke inatakiwa kufanya nini? Wanatakiwa kubadilisha ladha na kuendana na zama mpya za muziki (new generation).

WCB inatakiwa kubadilisha kuanzia management mpaka wasanii, yani inatakiwa kuzaliwa upya, ionekane mpya machoni na masikioni kwa watu.

Refreshment hii sio kuondoa wasanii waliobaki bali kuongeza wengine wenye ladha tofauti.

Nimeona Laizer ameweka tangazo wanatafuta wasanii wapya na ametoa details za wasanii kutuma profile na kazi zao. Well and good, lakini kwa sasa wanahitaji zaidi ya wasanii wapya wanahitaji pia ladha mpya.

Baibuda ndio imekuwa kama identity ya WCB lakini kwa sasa nafikiri wangejaribu kuleta pia aina nyingine ya muziki kama fusion ya choir na afro pop kwa mtazamo wangu wasanii wanaoimba huu muziki ni dili kwenye soko la Africa. Lakini pia wangejaribu kuleta msanii wa kumuuza kwenye international market ambae anaweza akapanda majukwaa makubwa Africa na akasound kama wenzie kwenye majukwaa asiwe msanii wa playback.

Kibishara sidhani kama ni sahihi kumchukua msanii kama Aslay kama tetesi zinavyosema nafikiri waingize damu changa tupu, though itachukua muda kupromoti wasanii wapya ila ina uhai kwenye biashara.

Don Jazzy alishawai kutumia hii formula akaja na kina Rema, Ladpoe na Ayrastarr baada ya kina Tiwa savage kusepa, Rema na Ayrastarr wamemlipa sana Don Jazzy.

Kwa hiyo Diamond kwenye hii refresh anayotaka kufanya aangalie sura mpya na radha mpya, kuna wasanii kama Ivra na Treysa (sina hakika na spelling), wanajua na wanaweza kufanya vizuri wakipata usimamizi wa lebo kubwa kama Wasafi.

Lakini pia atafute ghost writers kama Don Jazzy pale Marvin ana waandishi kama kumi kazi yao ni kuandika tu, japo falsafa ya WCB inataka msanii anaeweza kuandika mwenyewe lakini waandishi wanasaidia kubadilisha fleva za msanii anakuwa achoshi kumskiliza hata akikaa kwenye muziki muda mrefu.

Kwa sasa WCB naweza kusema ipo kwenye nafasi mbili kuimalika na kuzidi kuwa powerful au kudondoka kabisa na kupotea.

Inategemea na maamuzi atayofanya Diamond.
 
Kila lenye mwanzo lina mwisho..boss wao naona kawa teja mazima
 
Soko la mziki limebadilika sana, wasanii wako motivated zaidi ku perform kama solo artist, wengi wameshagundua mfumo wa Lebo ni wa kinyonyaji na kuwa unaweza kutoka bila kuwa affiliated na record label yyt, alafu pia ukiangalia toka harmonize aondoke na recently rayvanny ni kama vile WCB wamepoteza karata zao muhimu zilizokuwa zikiwaingizia mpunga wa kutosha , na mbosso naye anaondoka ni pigo kwao, wanabakiwa na Zuchu tu, maana ingizo lao jipya la D voice ni kama vile waliingia mkenge
ungeweka na sababu za kusema hvyo ingekuwa ni vyema sana hata kama ni mtihani ungemshawishi msahihishaji
 
Soko la mziki limebadilika sana, wasanii wako motivated zaidi ku perform kama solo artist, wengi wameshagundua mfumo wa Lebo ni wa kinyonyaji na kuwa unaweza kutoka bila kuwa affiliated na record label yyt, alafu pia ukiangalia toka harmonize aondoke na recently rayvanny ni kama vile WCB wamepoteza karata zao muhimu zilizokuwa zikiwaingizia mpunga wa kutosha , na mbosso naye anaondoka ni pigo kwao, wanabakiwa na Zuchu tu, maana ingizo lao jipya la D voice ni kama vile waliingia mkenge
Hapo sawa,ila kutoka kama solo artist hadi uje kutoboa inatakiwa awe pia na backup nzuri ya fedha kwani kuna issue za kurekod audio kali,video kali nk,si unajua priducer kama s2kizz tu kukugongea ngoma moja tu anataka nafikiri 10m,hiyo ni audio tu,jevideo tu.

So maranyingu wanalazimika kuwa chini ya label ili kuwa supported financially hata kama wana vipaji.
 
Soko la mziki limebadilika sana, wasanii wako motivated zaidi ku perform kama solo artist, wengi wameshagundua mfumo wa Lebo ni wa kinyonyaji na kuwa unaweza kutoka bila kuwa affiliated na record label yyt, alafu pia ukiangalia toka harmonize aondoke na recently rayvanny ni kama vile WCB wamepoteza karata zao muhimu zilizokuwa zikiwaingizia mpunga wa kutosha , na mbosso naye anaondoka ni pigo kwao, wanabakiwa na Zuchu tu, maana ingizo lao jipya la D voice ni kama vile waliingia mkenge
Wasanii wengi bado wanahitaji lebo kuwasogeza sio rahisi kwa muziki wa sasa kutoboa bila lebo sio rahisi na hata ikitokea umepata wimbo mkali ukapenya wenyewe bila uwekezaji shughuli inakuja kwenye kumaintain.
Kumbuka video ya kawaida ambayo itakupa standard za msanii anaejielewa haiwezi kuwa chini ya million 15 hiyo ni video moja na walau uwe na videos tatu kwa mwaka ili uwe machoni pa watu, kwa msanii ambae anajitafuta sio kazi rahisi.
 
Wcb ilikuwaga zamani siku hizi imekufa kabisa tembea mikoani husikii hata wakijadili wasanii wao siku hizi gospel imekuja juu kila kona
 
Hapo sawa,ila kutoka kama solo artist hadi uje kutoboa inatakiwa awe pia na backup nzuri ya fedha kwani kuna issue za kurekod audio kali,video kali nk,si unajua priducer kama s2kizz tu kukugongea ngoma moja tu anataka nafikiri 10m,hiyo ni audio tu,jevideo tu.

So maranyingu wanalazimika kuwa chini ya label ili kuwa supported financially hata kama wana vipaji.
Ni kweli kutoboa bila lebo ni ngumu sana kwa muziki wa wakati huu. Yes umlipe producer, umlipe na video director. Hapo pia unatakiwa uwe na social media manager anaesimamia akaunti zako anakupiga picha nzuri, video clips nk.

Muziki umebadilika sana bila uwekezaji lazima uwe unajiweza sana.
 
Wcb ilikuwaga zamani siku hizi imekufa kabisa tembea mikoani husikii hata wakijadili wasanii wao siku hizi gospel imekuja juu kila kona
Muziki wa gospel unafanya vizuri sana kwa sasa, wasanii wa gospel wakishtuka watapiga pesa nzuri wakati huu.
 
Kila kitu chini ya jua kina mwisho wa kuwa.. End of existence
CcM hawaamini hilo, wao wanaamini kuwa ni wa Milele, yaani hata CCM ya Wasira, Samia na akina Bashite, Chalamila na akina Mwijaku na Shilole inaamini yenyewe ni ya milele na bora kuliko upande walipo akina Tundu Lissu, Mbowe, Heche, Jussa, Zitto Mnyika, Ado na John Mnyika
 
Hapo sawa,ila kutoka kama solo artist hadi uje kutoboa inatakiwa awe pia na backup nzuri ya fedha kwani kuna issue za kurekod audio kali,video kali nk,si unajua priducer kama s2kizz tu kukugongea ngoma moja tu anataka nafikiri 10m,hiyo ni audio tu,jevideo tu.

So maranyingu wanalazimika kuwa chini ya label ili kuwa supported financially hata kama wana vipaj ya k

Hapo sawa,ila kutoka kama solo artist hadi uje kutoboa inatakiwa awe pia na backup nzuri ya fedha kwani kuna issue za kurekod audio kali,video kali nk,si unajua priducer kama s2kizz tu kukugongea ngoma moja tu anataka nafikiri 10m,hiyo ni audio tu,jevideo tu.

So maranyingu wanalazimika kuwa chini ya label ili kuwa supported financially hata kama wana vipaji.
S2kizzy ni 12 m
 
Na ni vile kama soko la records label linaanza kukosa mvuto
Tunazo lebo ambazo hazifanyi vizuri lakini si kweli kwamba lebo zinakosa mvuto ila uendeshaji wa lebo nafikiri ndio changamoto. Lebo kama Kings Music, Konde gang, Next level hazifanyi vizuri sababu ya poor management.

Nandy msanii wake yule Yami anaenda vizuri japo ni mdogo mdogo sababu nyuma ya Nandy kulikuwa na mtu anaejua kazi za management.

I think lebo zichukue watu kama kina D fighter wanaojua kusimamia wasanii, msanii pekee hatoshi kusimamia wasanii wenzake. WCB ilikuwa kubwa sababu ya Fella na Tale ambao kwa sasa wamegeukia kwenye siasa.
 
Back
Top Bottom