Je, Umoja wa Afrika (AU) ni project iliyoshindwa?

Strong ladg

Senior Member
Jul 15, 2021
155
435
Niende kwenye mada . Swali ambalo nimeanza kujiuliza hivi karibuni, ni nini faida ya kuwa na AU kwa sasa hapa Afrika. Kwanza fedha tu za kujiendesha AU zinatolewa kwa asilimia kubwa na Umoja wa Ulaya. Hizo fedha haziji bure zinakuja na masharti kibao, maana yake ni kwamba Umoja wa Afrika unaendeshwa na Umoja wa Ulaya,nini maana ya kuwa na AU kama bajeti yake tu inatushinda?

Pili AU imeshindwa kuleta suluhisho la kudumu kuhusu vita na ukosefu wa usalama kwenye nchi za Afrika. Mfano sasahivi Sudan kuna vita ambayo hatuoni ikiisha karibuni lakini AU wako kimya kama hakuna kinachoendelea hapo Sudan.

AU imeshindwa kuweka utaratibu wa kurahisisha usafirishaji rahisi wa bidhaa na usafiri rahisi wa watu kati ya nchi za Afrika.

Kama hiyo haitoshi viongozi wa Afrika ambao ndio wanakutana Addis Ababa Ethiopia asilimia kubwa ni wala Rushwa, vibaraka, n.k n.k . Yaani umoja unaundwa na Ruto, Tinubu, Ouattara aisée what do you expect.

Hitimisho langu ni kwamba Umoja wa Afrika umeshindwa kufikia ndoto za waanzilishi wake kina Kwame Nkrumah na badala yake umekuwa ukitumiwa na maadui wa Afrika kutekeleza ajenda zao.

Naomba kuwasilisha na nakubali kukosolewa.
 
AU haijawahi kuwa na maana yoyote kwa raia wa kawaida Africa
 
Niende kwenye mada . Swali ambalo nimeanza kujiuliza hivi karibuni, ni nini faida ya kuwa na AU kwa sasa hapa Afrika. Kwanza fedha tu za kujiendesha AU zinatolewa kwa asilimia kubwa na Umoja wa Ulaya!!!!!. Hizo fedha haziji bure zinakuja na masharti kibao, maana yake ni kwamba Umoja wa Afrika unaendeshwa na Umoja wa Ulaya,nini maana ya kuwa na AU kama bajeti yake tu inatushinda?

Pili AU imeshindwa kuleta suluhisho la kudumu kuhusu vita na ukosefu wa usalama kwenye nchi za Afrika. Mfano sasahivi Sudan kuna vita ambayo hatuoni ikiisha karibuni lakini AU wako kimya kama hakuna kinachoendelea hapo Sudan.

AU imeshindwa kuweka utaratibu wa kurahisisha usafirishaji rahisi wa bidhaa na usafiri rahisi wa watu kati ya nchi za Afrika.

Kama hiyo haitoshi viongozi wa Afrika ambao ndio wanakutana Addis Ababa Ethiopia asilimia kubwa ni wala Rushwa, vibaraka, n.k n.k . Yaani umoja unaundwa na Ruto, Tinubu, Ouattara aisée what do you expect.

Hitimisho langu ni kwamba Umoja wa Afrika umeshindwa kufikia ndoto za waanzilishi wake kina Kwame Nkrumah na badala yake umekuwa ukitumiwa na maadui wa Afrika kutekeleza ajenda zao..
Naomba kuwasilisha na nakubali kukosolewa
Umoja w Afrika ni kijiwe cha kupiga soga tu naona.. sionagi maazimio ya maana yanayotoka huko

Sijawah kuona hata initiative iliyoanziabwa mfano kitu rahis kabisa ambacho wangefanya ni kujitengenezea soko la ndan la afrika kama walivyofanya Europe ..

Yaan bara lingejitosheleza kuanzia source za Enegry ( mafuta na madini) kwenda kwenye vyakula.. wanashindwa akutengeneza mnyororo wa thaman wa ndan ya afrika kutengeneza masoko mkajitosheleza wenyewe..

Wenye mafuta na gas wakauza Humu ndani. Wenye vyakula vya kutoaha wakauza ndani kwanza.. wenye madini hali kadhalika

Chukulia bank za afrika zingefadhili
Mirad kama ya kuzalisha umeme, mafuta na gas kisha nchi za Afrika wakauziana hizo product na kupeana mikopo nafuu..

Reli zijengwe kimkakati kuunganisha border..Zingejengwa reli kuunganisha miji na nchi kusafirisha watu na mizigo
Ila matokeo yake nchi zetu zimekuwa hub za western kuchuma. Na kuondoka

We ona ulaya watu walijenga mabomba ya gas kilometers and kilometers .. (toka Urusi had Ujerumani)
 
AU Haina faida yoyote kwa Africa iyo ndio Ile indirect rule wazungu wanakutumia icho chama kututawala kama bajeti tu inatoka kwao ivi Kuna Nini hapo,waafrika tumekuwa watu wa hovyo kwenye kila eneo wewe fikiria ni mambo mangapi ambayo yanatokea afrika yanayotia aibu mpaka unijiuliza ivi kwanini nipo afrika
Waafrika tunatakiwa tubadilishe mambo mengi ili tuwe kujitawala wenzetu wako serious na kujenga nchi zao na kufanya atu wao waishi vzr hapa duniani lkn afrika sasa ni vituko
 
Back
Top Bottom