Je, Uhusiano wa Mbowe na Lissu ni wa Kinafiki au Mkakati wa Kisiasa?

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Aug 29, 2022
790
1,669
Kwa kuangalia jinsi Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, na Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, wanavyoishi na kushirikiana kisiasa, ni dhahiri kwamba kuna hali ya kutatanisha. Naamini maisha wanayoonyesha hadharani ni ya kinafiki, ambapo kila mmoja anamtamani mwenzake "aingie kwenye 18 zake."

Leo, katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika makao makuu ya chama hicho huko Mikocheni, Dar es Salaam, nimewashuhudia Mbowe na Lissu wakionekana kufurahia na kuonyesha mshikamano kana kwamba hakuna tofauti yoyote kati yao. Hata hivyo, ukitazama kihalisia, inaonekana kwamba furaha hiyo ni ya juujuu na imejaa unafiki wa kisiasa.

Hili linathibitishwa na historia yao ya kutoelewana hadharani kupitia maneno makali kwenye majukwaa ya kisiasa. Kitendo cha ghafla cha kuonyesha wapo sawa mbele ya watu ni dhihirisho la kutengeneza sura ya umoja ilhali ndani ya mioyo yao kuna mgawanyiko mkubwa.

Soma Pia: PICHA: Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwenye Kamati Kuu Chadema

Ni wazi kuwa kuna chuki za dhati kati yao, na ushahidi wa vita vyao vya ndani umeonekana mara kadhaa, ambapo kila mmoja amekiri, kwa njia moja au nyingine, kwamba hawana mawasiliano mazuri. Kinachoendelea sasa kinafanana na msemo wa Kiswahili: "kuficha kombe mwanaharamu apite."

Hata hivyo, ni vyema Mbowe na Lissu kutambua kuwa michezo hii ya kisiasa wanayoitengeneza iko wazi kwa raia wa kawaida. Tunatambua namna wanavyojaribu kuficha mgogoro wao kwa vikao na matukio ya pamoja. Lakini, ukweli ni kwamba hali hii siyo endelevu na inaweza kuathiri nguvu ya chama chao kisiasa.

Swali linalobaki ni je, wataweza kuweka tofauti zao kando na kushirikiana kwa dhati kwa maslahi ya chama na taifa, au mgogoro huu wa chini kwa chini utaendelea kudhoofisha harakati za CHADEMA? Huu ni mtihani mkubwa kwao kama viongozi wa upinzani Tanzania.

Screenshot 2025-01-10 153917.png
 
Waombee ili upendo kati yao utamalaki...

Wewe unafikiri binadamu tuna shida basi? Wanadamu daima hawana shida. Shida ni shetani anapopata nafasi ya kusimama katikati yenu na kuanza kuchochea moto na kuingiza fitina zake. Na hii hutokea kwa mmoja kumfungulia mlango huyu shetani...

Mimi nimeipenda sana picha hii...

Na kwangu mimi ninavyomfahamu Tundu Lissu, he is always genuine, truthful and harmless...

Unavyomuona hapo physically, ndivyo alivyo hata ndani ya moyo na nafsi...

Kama ana tatizo na wewe, atakuambia waziwazi mchana kweupe ili kama mtalimaliza mlimalize na inakuwa imetoka hiyo...
 
Kwa kuangalia jinsi Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, na Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, wanavyoishi na kushirikiana kisiasa, ni dhahiri kwamba kuna hali ya kutatanisha. Naamini maisha wanayoonyesha hadharani ni ya kinafiki, ambapo kila mmoja anamtamani mwenzake "aingie kwenye 18 zake."

Leo, katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika makao makuu ya chama hicho huko Mikocheni, Dar es Salaam, nimewashuhudia Mbowe na Lissu wakionekana kufurahia na kuonyesha mshikamano kana kwamba hakuna tofauti yoyote kati yao. Hata hivyo, ukitazama kihalisia, inaonekana kwamba furaha hiyo ni ya juujuu na imejaa unafiki wa kisiasa.

Hili linathibitishwa na historia yao ya kutoelewana hadharani kupitia maneno makali kwenye majukwaa ya kisiasa. Kitendo cha ghafla cha kuonyesha wapo sawa mbele ya watu ni dhihirisho la kutengeneza sura ya umoja ilhali ndani ya mioyo yao kuna mgawanyiko mkubwa.

Soma Pia: PICHA: Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwenye Kamati Kuu Chadema

Ni wazi kuwa kuna chuki za dhati kati yao, na ushahidi wa vita vyao vya ndani umeonekana mara kadhaa, ambapo kila mmoja amekiri, kwa njia moja au nyingine, kwamba hawana mawasiliano mazuri. Kinachoendelea sasa kinafanana na msemo wa Kiswahili: "kuficha kombe mwanaharamu apite."

Hata hivyo, ni vyema Mbowe na Lissu kutambua kuwa michezo hii ya kisiasa wanayoitengeneza iko wazi kwa raia wa kawaida. Tunatambua namna wanavyojaribu kuficha mgogoro wao kwa vikao na matukio ya pamoja. Lakini, ukweli ni kwamba hali hii siyo endelevu na inaweza kuathiri nguvu ya chama chao kisiasa.

Swali linalobaki ni je, wataweza kuweka tofauti zao kando na kushirikiana kwa dhati kwa maslahi ya chama na taifa, au mgogoro huu wa chini kwa chini utaendelea kudhoofisha harakati za CHADEMA? Huu ni mtihani mkubwa kwao kama viongozi wa upinzani Tanzania.

View attachment 3197575
Kwani wewe inakuhusu nini?.
 
Waombee ili upendo kati yao utamalaki...

Wewe unafikiri binadamu tuna shida basi? Wanadamu daima hawana shida. Shida ni shetani anapopata nafasi ya kusimama katikati yenu na kuanza kuchochea moto na kuingiza fitina zake. Na hii hutokea kwa mmoja kumfungulia mlango huyu shetani...

Mimi nimeipenda sana picha hii...

Na kwangu mimi ninavyomfahamu Tundu Lissu, he is always genuine, truthful and harmless...

Unavyomuona hapo physically, ndivyo alivyo hata ndani ya moyo na nafsi...

Kama ana tatizo na wewe, atakuambia waziwazi mchana kweupe ili kama mtalimaliza mlimalize na inakuwa imetoka hiyo...

Hakunaga Mwanaharakati mwenye kinyongo na visasi .
Wanaharakati hua hawajawahi kutumia silaha zaidi ya maneno ya mdomo.

Hakuna Mwanaharakati anayeteka watu.

Hata mimi nimeipenda sana hiyo picha .
Hawa ni miamba kweli kweli ..

Lisu atashinda na chama kitaimarika sana . Mbowe atakumbukwa kwa mazuri aliyofanya .

Madikteta hua wana mazuri yao.
 
Waombee ili upendo kati yao utamalaki...

Wewe unafikiri binadamu tuna shida basi? Wanadamu daima hawana shida. Shida ni shetani anapopata nafasi ya kusimama katikati yenu na kuanza kuchochea moto na kuingiza fitina zake. Na hii hutokea kwa mmoja kumfungulia mlango huyu shetani...

Mimi nimeipenda sana picha hii...

Na kwangu mimi ninavyomfahamu Tundu Lissu, he is always genuine, truthful and harmless...

Unavyomuona hapo physically, ndivyo alivyo hata ndani ya moyo na nafsi...

Kama ana tatizo na wewe, atakuambia waziwazi mchana kweupe ili kama mtalimaliza mlimalize na inakuwa imetoka hiyo...
Utakuwa huja fuatilia majadiliano ya Mbowe na Clouds leo usikilize hoja zake
 
Kwa kuangalia jinsi Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, na Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, wanavyoishi na kushirikiana kisiasa, ni dhahiri kwamba kuna hali ya kutatanisha. Naamini maisha wanayoonyesha hadharani ni ya kinafiki, ambapo kila mmoja anamtamani mwenzake "aingie kwenye 18 zake."

Leo, katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika makao makuu ya chama hicho huko Mikocheni, Dar es Salaam, nimewashuhudia Mbowe na Lissu wakionekana kufurahia na kuonyesha mshikamano kana kwamba hakuna tofauti yoyote kati yao. Hata hivyo, ukitazama kihalisia, inaonekana kwamba furaha hiyo ni ya juujuu na imejaa unafiki wa kisiasa.

Hili linathibitishwa na historia yao ya kutoelewana hadharani kupitia maneno makali kwenye majukwaa ya kisiasa. Kitendo cha ghafla cha kuonyesha wapo sawa mbele ya watu ni dhihirisho la kutengeneza sura ya umoja ilhali ndani ya mioyo yao kuna mgawanyiko mkubwa.

Soma Pia: PICHA: Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwenye Kamati Kuu Chadema

Ni wazi kuwa kuna chuki za dhati kati yao, na ushahidi wa vita vyao vya ndani umeonekana mara kadhaa, ambapo kila mmoja amekiri, kwa njia moja au nyingine, kwamba hawana mawasiliano mazuri. Kinachoendelea sasa kinafanana na msemo wa Kiswahili: "kuficha kombe mwanaharamu apite."

Hata hivyo, ni vyema Mbowe na Lissu kutambua kuwa michezo hii ya kisiasa wanayoitengeneza iko wazi kwa raia wa kawaida. Tunatambua namna wanavyojaribu kuficha mgogoro wao kwa vikao na matukio ya pamoja. Lakini, ukweli ni kwamba hali hii siyo endelevu na inaweza kuathiri nguvu ya chama chao kisiasa.

Swali linalobaki ni je, wataweza kuweka tofauti zao kando na kushirikiana kwa dhati kwa maslahi ya chama na taifa, au mgogoro huu wa chini kwa chini utaendelea kudhoofisha harakati za CHADEMA? Huu ni mtihani mkubwa kwao kama viongozi wa upinzani Tanzania.

View attachment 3197575
Mkakati wa kumchuna mama Abdul.
 
Kwa kuangalia jinsi Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, na Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, wanavyoishi na kushirikiana kisiasa, ni dhahiri kwamba kuna hali ya kutatanisha. Naamini maisha wanayoonyesha hadharani ni ya kinafiki, ambapo kila mmoja anamtamani mwenzake "aingie kwenye 18 zake."

Leo, katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika makao makuu ya chama hicho huko Mikocheni, Dar es Salaam, nimewashuhudia Mbowe na Lissu wakionekana kufurahia na kuonyesha mshikamano kana kwamba hakuna tofauti yoyote kati yao. Hata hivyo, ukitazama kihalisia, inaonekana kwamba furaha hiyo ni ya juujuu na imejaa unafiki wa kisiasa.

Hili linathibitishwa na historia yao ya kutoelewana hadharani kupitia maneno makali kwenye majukwaa ya kisiasa. Kitendo cha ghafla cha kuonyesha wapo sawa mbele ya watu ni dhihirisho la kutengeneza sura ya umoja ilhali ndani ya mioyo yao kuna mgawanyiko mkubwa.

Soma Pia: PICHA: Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwenye Kamati Kuu Chadema

Ni wazi kuwa kuna chuki za dhati kati yao, na ushahidi wa vita vyao vya ndani umeonekana mara kadhaa, ambapo kila mmoja amekiri, kwa njia moja au nyingine, kwamba hawana mawasiliano mazuri. Kinachoendelea sasa kinafanana na msemo wa Kiswahili: "kuficha kombe mwanaharamu apite."

Hata hivyo, ni vyema Mbowe na Lissu kutambua kuwa michezo hii ya kisiasa wanayoitengeneza iko wazi kwa raia wa kawaida. Tunatambua namna wanavyojaribu kuficha mgogoro wao kwa vikao na matukio ya pamoja. Lakini, ukweli ni kwamba hali hii siyo endelevu na inaweza kuathiri nguvu ya chama chao kisiasa.

Swali linalobaki ni je, wataweza kuweka tofauti zao kando na kushirikiana kwa dhati kwa maslahi ya chama na taifa, au mgogoro huu wa chini kwa chini utaendelea kudhoofisha harakati za CHADEMA? Huu ni mtihani mkubwa kwao kama viongozi wa upinzani Tanzania.

View attachment 3197575
Tatizo hamsikilizi mahojiano vzr
Mbowe aliuliuzwa na kikeke,Kwa haya yanayoendelea mkikutana itakuaje?.
Akamjibu, huwa tunacheka sana....Tena tuna vikao wiki 2 mfululizo

Fuatailia mahojiano Yale ,Iko part 1&2
 
Hakunaga Mwanaharakati mwenye kinyongo na visasi .
Wanaharakati hua hawajawahi kutumia silaha zaidi ya maneno ya mdomo.

Hakuna Mwanaharakati anayeteka watu.

Hata mimi nimeipenda sana hiyo picha .
Hawa ni miamba kweli kweli ..

Lisu atashinda na chama kitaimarika sana . Mbowe atakumbukwa kwa mazuri aliyofanya .

Madikteta hua wana mazuri yao.
Na akishindwa?
 
Kwa kuangalia jinsi Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, na Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, wanavyoishi na kushirikiana kisiasa, ni dhahiri kwamba kuna hali ya kutatanisha. Naamini maisha wanayoonyesha hadharani ni ya kinafiki, ambapo kila mmoja anamtamani mwenzake "aingie kwenye 18 zake."

Leo, katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika makao makuu ya chama hicho huko Mikocheni, Dar es Salaam, nimewashuhudia Mbowe na Lissu wakionekana kufurahia na kuonyesha mshikamano kana kwamba hakuna tofauti yoyote kati yao. Hata hivyo, ukitazama kihalisia, inaonekana kwamba furaha hiyo ni ya juujuu na imejaa unafiki wa kisiasa.

Hili linathibitishwa na historia yao ya kutoelewana hadharani kupitia maneno makali kwenye majukwaa ya kisiasa. Kitendo cha ghafla cha kuonyesha wapo sawa mbele ya watu ni dhihirisho la kutengeneza sura ya umoja ilhali ndani ya mioyo yao kuna mgawanyiko mkubwa.

Soma Pia: PICHA: Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwenye Kamati Kuu Chadema

Ni wazi kuwa kuna chuki za dhati kati yao, na ushahidi wa vita vyao vya ndani umeonekana mara kadhaa, ambapo kila mmoja amekiri, kwa njia moja au nyingine, kwamba hawana mawasiliano mazuri. Kinachoendelea sasa kinafanana na msemo wa Kiswahili: "kuficha kombe mwanaharamu apite."

Hata hivyo, ni vyema Mbowe na Lissu kutambua kuwa michezo hii ya kisiasa wanayoitengeneza iko wazi kwa raia wa kawaida. Tunatambua namna wanavyojaribu kuficha mgogoro wao kwa vikao na matukio ya pamoja. Lakini, ukweli ni kwamba hali hii siyo endelevu na inaweza kuathiri nguvu ya chama chao kisiasa.

Swali linalobaki ni je, wataweza kuweka tofauti zao kando na kushirikiana kwa dhati kwa maslahi ya chama na taifa, au mgogoro huu wa chini kwa chini utaendelea kudhoofisha harakati za CHADEMA? Huu ni mtihani mkubwa kwao kama viongozi wa upinzani Tanzania.

View attachment 3197575
Siasa sip uadui
 
Na akishindwa?

Mbona mnakwepa neno akishindwa kihalali . Ndio maana akaomba uwazi uwepo na pawe na waangalizi kutoka kwenye nchi wahisani na wadau wa Demokrasia lakini pia viongozi wa dini.
Ngoma ya uchaguzi izinduliwe kwa Sala na dua .
Uwazi uwepo .
Atakayeshindwa apongezwe na kuheshimiwa.

CCM inashinda kila mwaka lakini kuna tofauti ya ushindi kila mwaka jinsi unavyopokelewa na wapinzani kutokana na kukosekana kwa haki .

Kura tangu enzi za manabii ilikua inapigwa ili kuamua jambo . Anayepata anapongeza.

Hata kamari siku hizi ni za haki kwa sababu zinafanywa na Mashine zisizo na udanganyifu kama enzi hizo ilipokuwa inaharamishwa .
Binadamu walikua wanachezesha kamari za chekundu cheusi kwa hila na udanganyifu mkubwa ndio maana ikawa ni haramu . Lakini leo watu kwa mamilioni wanapata kulingana na kwamba ni Computer inayowekewa program na hakuna ushawishi wa kilaghai zaidi ya mtu mwenyewe kuamua . Sio yale mambo ya mtoto ametumwa dukani anakutana na wahuni wanacheza kamari wanamlaghi na akipata wanageuza kile alichopata na kumwonyesha cha uwongo ili asishinde.

Hatutaki uchaguzi wa Chekundu Cheusi.
Tunataka ngoma icheze kweupe kama Yanga na ALGER itakayoamua ugomvi wa Club bingwa hadharani pale Taifa . 😂😂😂😂😂😂
No hate no fear.
Tumechoka .
Hatutaki siasa za kinafiki.

Waachieni polisi na usalama wapumzike . Maana hivi vyombo vya dola pakiwa na demokrasia ya kweli vinaondokana na lawama na kutumika kuwadhuru na kuwaumiza ndugu zao kwa sababu tu ya kazi ya siasa kushindwa kufanywa kwa misingi ya haki , na mwisho vyombo vya dola kuja kuonekana kuwa ni watu katili kumbe ni kwa sababu ya kakundi kadogo kanakokosa agenda na mipango zaidi ya kutumia udanganyifu..

No reform no Election ianzie ndani ya Chadema wenyewe 😂😂😂😂
 
Kwa kuangalia jinsi Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CHADEMA, na Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, wanavyoishi na kushirikiana kisiasa, ni dhahiri kwamba kuna hali ya kutatanisha. Naamini maisha wanayoonyesha hadharani ni ya kinafiki, ambapo kila mmoja anamtamani mwenzake "aingie kwenye 18 zake."

Leo, katika kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA kilichofanyika makao makuu ya chama hicho huko Mikocheni, Dar es Salaam, nimewashuhudia Mbowe na Lissu wakionekana kufurahia na kuonyesha mshikamano kana kwamba hakuna tofauti yoyote kati yao. Hata hivyo, ukitazama kihalisia, inaonekana kwamba furaha hiyo ni ya juujuu na imejaa unafiki wa kisiasa.

Hili linathibitishwa na historia yao ya kutoelewana hadharani kupitia maneno makali kwenye majukwaa ya kisiasa. Kitendo cha ghafla cha kuonyesha wapo sawa mbele ya watu ni dhihirisho la kutengeneza sura ya umoja ilhali ndani ya mioyo yao kuna mgawanyiko mkubwa.

Soma Pia: PICHA: Mbowe, Lissu walivyokutana uso kwa uso kwenye Kamati Kuu Chadema

Ni wazi kuwa kuna chuki za dhati kati yao, na ushahidi wa vita vyao vya ndani umeonekana mara kadhaa, ambapo kila mmoja amekiri, kwa njia moja au nyingine, kwamba hawana mawasiliano mazuri. Kinachoendelea sasa kinafanana na msemo wa Kiswahili: "kuficha kombe mwanaharamu apite."

Hata hivyo, ni vyema Mbowe na Lissu kutambua kuwa michezo hii ya kisiasa wanayoitengeneza iko wazi kwa raia wa kawaida. Tunatambua namna wanavyojaribu kuficha mgogoro wao kwa vikao na matukio ya pamoja. Lakini, ukweli ni kwamba hali hii siyo endelevu na inaweza kuathiri nguvu ya chama chao kisiasa.

Swali linalobaki ni je, wataweza kuweka tofauti zao kando na kushirikiana kwa dhati kwa maslahi ya chama na taifa, au mgogoro huu wa chini kwa chini utaendelea kudhoofisha harakati za CHADEMA? Huu ni mtihani mkubwa kwao kama viongozi wa upinzani Tanzania.

View attachment 3197575
Watoto kuelewa hii.
Huu unaitwa ukomavu..
Mnapigana virungu then maisha yanaendelea tena
 
Back
Top Bottom