Je, ni kwa jinsi gani FOCAC inaweza kudumisha uhai wake kwa muda mrefu?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,064
1,075
VCG111379374819.jpg


Mkutano wa 2024 wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC utafanyika Beijing kuanzia Septemba 4 hadi 6. Hii itakuwa ni mara ya nne kwa Baraza hilo kufanya mkutano wake kuwa wa kilele, ambapo China na Afrika zitapanga kwa pamoja mwelekeo wa maendeleo ya ushirikiano wa siku zijazo kuhusu kauli mbiu ya "kuendeleza kwa pamoja mambo ya kisasa na kujenga jumuiya ya ngazi ya juu ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja." Hivi karibuni viongozi wengi waandamizi kutoka nchi za Afrika akiwemo Rais wa Zanzibar, Tanzania na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya walieleza matarajio yao makubwa kwa mkutano huo.

Tangu kuanzishwa kwake miaka 24 iliyopita, kupitia juhudi za pamoja za China na Afrika, FOCAC imekuwa makubaliano yenye ufanisi zaidi kati ya Afrika na nchi fulani, na maeneo ya ushirikiano ni mapana sana na pia yanaendana na wakati. Wakati huo huo, ufanisi mkubwa wa FOCAC pia unatokana na utaratibu imara wa tathmini na maandalizi. Mkutano wa FOCAC unafanyika kila baada ya miaka mitatu, mkutano wa uratibu unafanyika mwaka mmoja baada ya kumalizika kwa kila mkutano mkuu ili kuangalia utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa na mkutano wa maandalizi unafanyika siku kadhaa kabla ya mkutano mkuu ili kupanga mada za mkutano huo. Mfumo huu endelevu umedumisha mawasiliano ya karibu na uwajibikaji kwa miradi inayopendekezwa wakati wa mkutano, ili ahadi muhimu zinazotolewa kila wakati ziweze kutekelezwa kikweli.

Wakati huohuo FOCAC si tu kwamba imetambuliwa na China na Afrika, lakini pia hatua kwa hatua imekuwa bendera kwenye jukwaa la kimataifa ya kupanua ushirikiano wa kimataifa na Afrika na kuimarisha ushirikiano wa Kusini na Kusini. China daima imekuwa ikiuchukulia ushirikiano na nchi za Afrika kama uhusiano wa kunufaishana kati ya nchi zinazoendelea ndani ya utaratibu wa ushirikiano wa Kusini na Kusini. Mafanikio yanayoendelea ya FOCAC yameonyesha uwezekano wa maendeleo ya ushirikiano wa Kusini na Kusini, ambao sio tu unaongeza sauti na ushawishi wa "Dunia ya Kusini" katika masuala ya kimataifa, lakini pia unafafanua upya hali ya baadaye ya kisiasa na kiuchumi duniani.

Katika Mkutano wa 2024 wa FOCAC, mikataba mipya mfululizo ya ushirikiano inatarajiwa kuathiri zaidi uhusiano kati ya China na Afrika siku zijazo. Kwenye msingi wa mipango iliyofikiwa, inaaminika kuwa mkutano huo utaendelea kuweka kipaumbele katika kupanua ushirikiano wa kiuchumi, biashara na viwanda ili kupanua wigo wa bidhaa za Afrika zinazouzwa nje na uwezo wa uzalishaji viwandani barani humo. Kwa upande wa miundombinu, mkutano huo pia utaimarisha zaidi ushirikiano wa kifedha na kuboresha ufanisi wa uwekezaji wa China barani Afrika. Kuimarisha uhusiano kati ya watu na watu kunaweza pia kuwa jambo kuu katika mkutano wa mwaka huu. Katika Mazungumzo ya Viongozi wa China na Afrika mwaka 2023, China na Afrika zilitangaza kwa pamoja Mpango wa Ushirikiano wa Kuandaa Wataalam wa China na Afrika, ambapo China iliahidi kutoa mafunzo zaidi ya ufundi stadi kwa watu wa Afrika. Zaidi ya hayo, baada ya janga la COVID-19, mawasiliano ya kitamaduni yanatazamiwa kuzingatiwa tena, na kuanzisha tena enzi mpya ya utalii kati ya China na Afrika. Kando na maeneo haya matatu, ajenda kama afya, kilimo na uchumi wa kidijitali pia zitajadiliwa.

Inaaminika kwamba mkutano huo mpya utaenzi mafanikio yaliyopatikana, kutafiti njia mpya za ushirikiano, kuandika sura mpya katika ujenzi wa jumuiya ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja, na kuendelea kuimarisha FOCAC kama "chapa ya dhahabu" ya ushirikiano wa Kusini na Kusini
 

Attachments

  • VCG111437104227.jpg
    VCG111437104227.jpg
    1.4 MB · Views: 1
Back
Top Bottom