Je mamlaka zimeshindwa kabisa kuzuia matumizi ya namba zisizosajiliwa?

pombe kali

JF-Expert Member
Jun 28, 2014
279
554
Salamu wana jukwaa

Nimekuwa nikijiuliza je mamlaka husika zineshindwa kabisa kusitisha matumizi ya namba za simu zisizosajiliwa?

Hizi jumbe za tuma hela kwenye namba hii zimekuwa ni nyingi sana tena hutokea kama umeweka kiasi chochote kwenye simu yako, utaona meseji inasema mfano "mimi ni baba mwenye nyumba yako tuma kodi kwenye namba hii, au mimi ni mwalimu mkuu mwanao ameanguka shuleni,

Huwa najiuliza mamlaka imeshindwa kabisa kudhibiti matumizi ya laini zisizokuwa na usajili halali, zoezi zima la usajili hufanyika kitaalamu sana ambapo kitambulisho cha taifa hutumika na alama za vidole pia ambazo ni utambulisho wa pekee sasa hizi laini za simu zinazotumiwa na hawa jamaa huwa wanazitoa wapi?

kwa nini mitandao husika isiwajibishwe kwa kukubali kuwauzia watu laini bila kufuata sheria kanuni na utaratibu hawa watu wana matusi mabaya pale wanapobaini umewagundua mbinu yao ovu

Mamlaka hapa mnafeli wapi maana wala haihitajiki teknolojia ya juu ni ku disable namba zote zisizo na usajili halali....hata mwanangu anayesoma coding anaweza
 
Salamu wana jukwaa

Nimekuwa nikijiuliza je mamlaka husika zineshindwa kabisa kusitisha matumizi ya namba za simu zisizosajiliwa?

Hizi jumbe za tuma hela kwenye namba hii zimekuwa ni nyingi sana tena hutokea kama umeweka kiasi chochote kwenye simu yako, utaona meseji inasema mfano "mimi ni baba mwenye nyumba yako tuma kodi kwenye namba hii, au mimi ni mwalimu mkuu mwanao ameanguka shuleni,

Huwa najiuliza mamlaka imeshindwa kabisa kudhibiti matumizi ya laini zisizokuwa na usajili halali, zoezi zima la usajili hufanyika kitaalamu sana ambapo kitambulisho cha taifa hutumika na alama za vidole pia ambazo ni utambulisho wa pekee sasa hizi laini za simu zinazotumiwa na hawa jamaa huwa wanazitoa wapi?

kwa nini mitandao husika isiwajibishwe kwa kukubali kuwauzia watu laini bila kufuata sheria kanuni na utaratibu hawa watu wana matusi mabaya pale wanapobaini umewagundua mbinu yao ovu

Mamlaka hapa mnafeli wapi maana wala haihitajiki teknolojia ya juu ni ku disable namba zote zisizo na usajili halali....hata mwanangu anayesoma coding anaweza

Kweli kuna changamoto.
Yaani pamoja na kuja na ile namba maalumu (15040) ya kuripoti hizo ujumbe na namba za utapeli bado hakuna mabadiliko yoyote.

Unakuta namba unairipoti leo lakini baada ya wiki mbili unatumiwa tena ujumbe wa kitapeli kupitia hiyo hiyo namba.
 
Huenda matapeli yanatoa posho kwa wahusika haiwezekani ikawa kimya na hawachukuliwi hatua. Nilidhani hao jamaa hawapati hela kwamba watu wameshawajua utapeli wao asee huwezi amini mke wa jamaa mfanya biashara kapigwa laki6 ambayo alipaswa aitume shule mara msg ikaingia hiyo hela tuma kwa no hii jina fln akatuma baada ya muda akataka apige simu kwa mwalimu,mwalimu akasema hajaona kutaja jina ni mbingu na ardhi
 
Yote Tisa, Kumi ni ule ujumbe wa mwenye nyumba akinilalamikia kwa nini niko kimya ilhali leo ni mwisho wa mwezi na kutishia kunifukuza katika nyumba yake ifikapo jioni. Ila kiukweli mimi pia ni landlord, naishia kucheka tu.
 
Kila mtu atatapeliwa kwa wakati wake ni swala La muda tu
Nchi ishakuwa ya kula usawa wa kamba yako. Unamega kisela unapita hivi
 
@ pombe kali

Nimeona uzi wako huu,nami nilitaka kutoa uzi kama huu juu ya hili janga.
Kama unavyo ona pichani ni meseji nilizopokea kati ya December 2024 na January 2025.
Kuna maswali nilitaka kuuliza kwa:
1.TCRA: uwepo wa hizi namba nyingi zenye kuhusika na utapeli je hazi athiri takwimu mnazotoa za watumiaji wa simu Tanzania?
2.TTCL: kwa nini namba zenu ndio zinatumika Zaidi kwenye hili janga? je hakuna namna ya kuzuia? au uwezo upo ila hakuna ule utashi wa kisiasa?
3.POLISI NA MAHAKAMA: Ni matapeli wangapi walio kamatwa mpaka sasa? Ni wangapi walio kutwa na kesi na kuhukumiwa?
4.KAMPUNI ZA SIMU: hakuna namna ya kusajili namba bila kutumia mawakala?
 

Attachments

  • Screenshot_20241221-204318.jpg
    Screenshot_20241221-204318.jpg
    170.6 KB · Views: 1
  • Screenshot_20241222-164353.jpg
    Screenshot_20241222-164353.jpg
    140.5 KB · Views: 1
  • Screenshot_20241229-113257.jpg
    Screenshot_20241229-113257.jpg
    124 KB · Views: 2
  • Screenshot_20250104-142111.jpg
    Screenshot_20250104-142111.jpg
    148.1 KB · Views: 3
  • Screenshot_20250114-065845.jpg
    Screenshot_20250114-065845.jpg
    174.1 KB · Views: 2
  • Screenshot_20250114-065952.jpg
    Screenshot_20250114-065952.jpg
    178.1 KB · Views: 1
  • Screenshot_20250116-153431.jpg
    Screenshot_20250116-153431.jpg
    221.7 KB · Views: 1
  • Screenshot_20250117-194050.jpg
    Screenshot_20250117-194050.jpg
    191.3 KB · Views: 1
Huenda matapeli yanatoa posho kwa wahusika haiwezekani ikawa kimya na hawachukuliwi hatua. Nilidhani hao jamaa hawapati hela kwamba watu wameshawajua utapeli wao asee huwezi amini mke wa jamaa mfanya biashara kapigwa laki6 ambayo alipaswa aitume shule mara msg ikaingia hiyo hela tuma kwa no hii jina fln akatuma baada ya muda akataka apige simu kwa mwalimu,mwalimu akasema hajaona kutaja jina ni mbingu na ardhi
Wafanyakazi wa TCRA ndo wanamiliki hizo namba, wakiona miamala kwenye simu tuu wanatuma msg.
 
Back
Top Bottom