Ingekuwa ni Kenya, hivi ule muswada uliotokana na pendekezo la Mama Salma Kikwete kuwa "wapenzi" wa viongozi nao walipwe ingekuwaje?

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
14,096
53,131
Mama Salma alipendekeza kuwa wanandoa wa viongozi nao walipwe kama vile ambavyo "wapenzi" wao wanalipwa. Rais Samia Suluhu Hassan akaona hilo ni wazo zuri na akaamua kulifanyia kazi kwa kuunda muswada na kuupeleka bungeni. Sasa hivi, imekuwa sheria. Kwa hiyo, katika nchi hii, tuna wake wa viongozi wanalipwa simply because ni wake wa viongozi.

Siyo kwamba zamani haukuwepo utaratibu wa kuwatunza wajane wa viongozi, la hasha, ulikuwepo. Lakini Mama Salma akaona kwamba yeye anavyomhudumia Mzee Kikwete basi anatufanyia sisi Watanzania favor na kwa hiyo tunastahili kumlipa mpaka siku yake ya mwisho duniani!

Wakati mzee Kikwete anamchumbia, hakutushirikisha, wakati anamtolea mahari hakutushirikisha. Lakini leo Mama Salma anaona kuwa sisi Watanzania tuna deni kwake, kwamba ni lazima tumlipe simply kwa sababu yeye ni mke wa JK, mzee maarufu, muungwana!

Wakati anapendekeza hayo, huyo mama ni mbunge, mumewe ana mijihela kutokana na marupurupu kibao ya urais, mtoto wake ni mbunge. Sijui alikosa nini hadi kutaka apewe kingine juu ya kingi alicho nacho!

Leo nchi inahangaika kukamua wafanyabiashara, kodi zimekuwa mzigo, tozo zimekuwa nyingi. Miongoni mwa hizi pesa zinazotafutwa ni ili ipatikane pesa ya kuwalipa akina mama Salma kwa kuwa tu ni wake wa viongozi!

Najiuliza, mambo haya ya ajabuajabu hivi yagetokea Kenya, Wakenya wangeyaruhusu kweli? Kwamba mke wa rais mstaafu alipwe simply kwa sababu alikuwa mke wa rais? Hivi hawa watu wanatuchukuliaje sisi?

Watawala wa CCM wanadhani kiburi chao cha kutoheshimu hisia na mawazo ya Watanzania hakiwezi kuwa challenged. Lakini wasichokijua ni kuwa Watanzania WANADOCUMENT dharau moja baada ya nyingine, ujinga mmoja baada ya mwingine. Siku WAKIKINUKISHA, hayahaya mambo wanayodhani wamesahau ndiyo watakayowaambia kuwa wamechoshwa nayo. Hayahaya ambayo watawala wanadhani Watanzania wameyasahau na kwa hiyo kudhani kuwa wanaweza ku "go away with," ndiyo yatakayosomwa mbele ya vyombo vya habari siku hiyo kuwa ni sababu ya maamuzi yaliyofikiwa!

CCM wamekuwa too arrogant now. Watawala hawaogopi wala kujali wananchi kabisa! Kikombe cha gadhabu za Mtanzania kinaendelea kujaa polepole. Ole wao siku hiyo ya hasira kali itakapofika. Tanzania si kisiwa!
 
Pasingetosha, pasingekalika.

Woga na ujinga wetu ndio mtaji wa viongozi wetu danganyika.
Wameshajua sisi ni waoga kuliko maelezo. Hakuna kitu tunaweza wafanya

Pamoja na Ujinga wetu lakini mambo haya ya kibaradhuli watu wanayaducument, ndiyo hayohayo yatakayotumika kama sababu siku hiyo ambayo wananchi wataamua kuwanyoosha hawa wasio na aibu wala haya!
 
Watanzania Mungu awape nini? R.I.P JPM. CCM walitupa kiongozi bora kabisa ila wanasiasa wakichagizwa na Chadema hawakupenda uongozi wake. Huwa najiulizaga hivi baadhi ya wanasiasa wa nchi hii wapo kwa ajili ya nchi na wananchi au wapo kwa ajili ya kulinda maslahi yao na wafadhili wao. Naheshimu mawazo ya watu ila nikiona mtu yeyote anampinga JPM huwa namuona ni mtu mbinafsi na ana makando kando kibao.
 
Mama Salma alienda kuongea tu kwasababu anayo nafasi ya kusema.

Waliopanga mipango ni wajane wa hao viongozi, na walishaongea na SSH kuhusu shida zao. Mwenzao akaenda kuwaongelea tu, asipakwe matope tafadhali.
 
Mimi simshangai mtoa hoja bungeni, ninawashangaa walio pitisha, sijui ilikuwa 100%? Sababu tu za uoga wetu au tumelelewa kuwaheshimu sana wakubwa zetu. Lakini ilikuwa kila mbunge akirudi jimboni raia wawe wanamuuliza maswali kama
1. Mnajisikiaje kupitisha nyongeza ya maslahi kwenu tu na kuongeza mzigo kwa wananchi?
2. Hamhisi woga au aibu mbele ya wananchi?
Kwasababu hakuna vitu kama hivyo, waheshimiwa wetu wanajikumbuka wao sana, mwananchi baadaye sana.
Tutafika hivyohivyo.
 
Hako kasalma kameifisadi sana Nchi kupitia ka asasi uchwara kake ka wama.yaani familia nzima Wana asasi Kwa Kodi za wtz halafu Bado anataka Tena pesa za kumtunza kisa mke wa rais?Bahati yake tu ni kuwa watanzania ni waoga hata wakamuliwe vipi lakini hawachukui hatua yeyote zaidi ya kunung'unika tu.wakenya wasingekubali huo upumbavu na ulofa ambao ni vichaa tu wanaoweza kupitisha hiyo sheria
 
Nimeona video moja wabunge wanatoka nduki,spika nayo katiwa kwenye ambulance anatoroshwa
😄

Ova
 
Mama Salma alipendekeza kuwa wanandoa wa viongozi nao walipwe kama vile ambavyo "wapenzi" wao wanalipwa. Samia akaona hilo ni wazo zuri kwelikweli. Akaenda kuliundia muswada, akapeleka bungeni , sasa hivi imeshakuwa sheria. Kwa hiyo nchi hii tuna wake wa viongozi wanalipwa simply because eti ni wake wa viongozi.
Siyo kwamba zamani haukuwepo utaratibu wa kuwatunza wajane wa viongozi, la hasha ulikuwepo. Lakini Mama Salma akaona kwamba yeye anavyomhudumia Mzee Kikiwete basi anatufanyia sisi watanzania favor na kwa hiyo eti tunastahili kumlipa mpaka siku yake ya mwisho duniani!.

Wakati mzee Kikwete anamchumbia hakutushirikisha, wakati anamtolea mahari hakutshirikisha. Lakini leo Mama Salma anaona kuwa sisi Watanzania tuna deni kwake, kwamba ni lazima tumlipe simply kwa sababu yeye ni mke wa JK , Mzee Maarufu, Muungwana!.

Wakati anapendekeza hayo, huyo mama ni mbunge, mumewe ana mijihela kutokana na marupupuru kibao ya urais, mtoto wake ni mbunge. Sijui alikosa nini hadi kutaka apewe kingine juuu ya kingi alicho nacho!.

Leo nchi inahangaika kukamua wafanyabiashara, kodi zimekuwa mzigo, tozo zimekuwa nyingi. Miongoni mwa hizi pesa zinazotafutwa ni ili ipatikane pesa ya kuwalipa akina mama Salma kwa kuwa tu ni wake wa viongozi!.

Najiuliza, mambo haya ya ajabuajabu hivi yagetokea Kenya Wakenya wangeyaruhusu kweli?. Kwamba mke wa rais mstaafu alipwe simply kwa sababu alikuwa mke wa rais?. Hivi hawa watu wanatuchukuliaje sisi?

Watawala wa CCM wanadhani kiburi chao, cha kutoheshimu hisia na mawazo ya watanzania hakiwezi kuwa challenged. Lakini wasichokijua ni kuwa watanzania WANADOCUMENT dharau moja baada ya nyingine, ujinga mmoja baada ya mwingine. Siku WAKIKINUKISHA hayahaya mambo wanayodhani wamesahau ndiyo watakayowaambia kuwa wamechoshwa nayo, hayahaya ambayo watawala wanadhani watanzania wameyasahau na kwa hiyo kudhani kuwa wanaweza ku "go away with" ndiyo yatakayosomwa mbele ya vyombo vya habari siku hiyo kuwa ni sababu ya maamuzi yaliyofikiwa!

CCM wamekuwa too arrogant now. Watawala hawaogopi wala kujali wananchi kabisa!. Kikombe cha ghadahabu za mtanzania kinaendelea kujaa polepole , Ole wao siku hiyo ya hasira kali itakapofika. Tanzania si kisiwa!!
Ni ngumu mwanamke yoyote kuwa na akili na hata akiwa nazo ni ndogo kama chembe .... na ni ngumu mtu anaye penda ccm kuwa na akili timamu...pia nchi yetu inapokuwa chini ya viongozi wa dini ya mudi upumbavu na upuuzi unazidi sana
 
Leo nchi inahangaika kukamua wafanyabiashara, kodi zimekuwa mzigo, tozo zimekuwa nyingi. Miongoni mwa hizi pesa zinazotafutwa ni ili ipatikane pesa ya kuwalipa akina mama Salma kwa kuwa tu ni wake wa viongozi!.
Ni uroho, unyang'anyi na uporaji uliorasimishwa, ila wahenga walishasema:
"Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha"
 
Back
Top Bottom