Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,424
- 1,137
IGUNGA: "UWT TAIFA YAENDELEA KUHAMASISHA MAENDELEO NA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA"
Mjumbe wa Kamati ya Utekekelezaji ya Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mhe. Hawa Ghasia Amefanya Ziara kwenye Kata Nne za Jimbo la Igunga (Itumba, Lugubu, Nguvumoja na Igunga) kwa ajili ya kuhamasisha ;
1. Shughuli za Maendeleo, ikiwa ni utekekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM)
2. Wananchi kushiriki maboresho ya Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na Kujiandikisha kwenye Daftari la Wakazi kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
3. Wananchi kupinga ukatili wa Jinsia, unyanyasi wa Watoto na Ndoa za Jinsia Moja
Mhe. Ghasia Ameambata na Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mhe. Sauda Salum Mtondoo na Mbunge wa Jimbo la Igunga Mhe. Nicholaus George Ngassa, Waheshimiwa Madiwani wa Kata, Waheshimiwa Madiwani wa Viti Maalum, Viongozi wa CCM Wilaya, Kata na Matawi.