DOKEZO Hospitali ya Aga Khan yadaiwa kufunga baadhi ya Vituo vyake Tanzania, Mamia wadaiwa kupoteza Ajira

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

MDAU TZ

Member
Jun 9, 2023
12
53
images (6).jpeg
Kuna ya taarifa za kufungwa kwa baadhi ya vituo vya kutolea huduma ya afya vilivyopo chini ya Taasisi ya Aga Khan, Tanzania kwa sababu za changamoto za kiuendeshashaji.

Fununu hizo zinaeleza kuwa Taarifa zimetokana na mkutano uliofanyika na mtendendaji mkuu wa Taasisi hiyo nchini, kupitia mtandaoni na kuhudhuliwa na baadhi ya wafanyakazi.

Mtendendaji huyo amesema kwamba kutokana na changamoto za kiuendeshaji, Taasisi inalazimika kufunga baadhi ya vituo na kupunguza Wafanyakazi.

Hata hivyo, kwa mujibu ya mmoja wa wafanyakazi wa Taasisi hiyo akizunguumza kwa faragha na Mdau Tanzania, amekili kuwa Taarifa hizo ni za kweli na zoezi la kufunga vituo hivyo limeshaanza na mwisho wa uendeshaji wake inatarajiwa ni mwishoni mwa wiki hii ambapo itakuwa Tarehe 15/8/2024.

Mtoa Taarifa huyo amesema kwamba tayari baadhi ya wafanyakazi waliokuwa wakifanya kazi katika vituo vinavyofungwa na wale wanaopunguzwa kutoka kwenye vituo vinavyosalia wameshapewa barua za mualiko wa majadiliano ya kuachishwa kazi.

MY TAKE

Katika hili waajiri wengi wanatumia udhaifu wa Sheria ya Kazi inayotumiKa nchini katika kuwachisha kazi wafanyakazi wao pindi tu Taasisi inapopitia changamoto kidogo.

Sheria imempa wigo Mpana mwajili wa kufanya maamuzi bila ya kujali hali ya mwajiliwa.

Pia kutokana na urahisi waliopewa katika kipengele cha kupunguza wafanyakazi hasa kwa sababu za kiuendeshaji.

Ni wakati wa mamlala hisika kufikiria kufanya mabadiliko ya sheria hii ili kuwapa ulinzi na uhakika wa ajira kwa wafanyakazi.

IMG-20240724-WA0033.jpg
 
View attachment 3067994
KUNA taarifa za kufungwa Kwa baazi ya vituo vya kutolea huduma ya afya vilivyopo chini ya Taasisi ya Aga Khan,Tanzania kwasababu za changamoto za kiuendeshashaji...
Hawa administration wa Aga Khan ni wabaguzi sana. Nasikia wengi wao ni expatriates. Na hawa wanakula mishahara mikubwa na PAYE hawakatwi.

Nasikio wafanyakazi wazawa ndiyo wanaachishwa. Ma expatriates hawajaguswa.

Ingekuwa vizuri wizara husika ziangalie kinachoendelaea hapo Aga Khan.
 
kwa kweli sijapenda nilikuwa nawaza kwenda kufanya checkup kwao nimemeza mwiba wa mfupa...ntataabika kwa kweli..pamoja ya kuwa ni gharama kufanya matibabu kwao ila ni rahisi na haraka kuliko serikalini wanajali mazingira ya afya na ya kutolea huduma..pole kwa taasisi serikali ilitakiwa ibane fungu moja linalopigwa hovyo kuwapa watoa huduma kama hawa huku ikiwasimamia...
 
Back
Top Bottom