Joseph Nyoni
Member
- Apr 21, 2024
- 5
- 2
TABIA ZA MTU MZALENDO
Na Joseph Nyoni
Uzalendo nini? Uzalendo ni ibada ya kulipenda, kulitumikia na kulitetea taifa katika hali yoyote pamoja na kutanguliza maslahi ya taifa.
Zifuatazo ni tabia za mtu mzalendo
1. Analipenda taifa lake na hawi tayari kuliona taifa lake linaingia kwenye shida, matatizo au linaonewa, linaaibika na kunyanyasika, muda wote anaangalia faida/ maslahi ya taifa lake.
2. Kulipigania taifa linapoingia katika dhiki, shida, na kila hali
3. Mzalendo si mbinafsi! Hatangulizi mambo yake bali ya taifa. Taifa lifaidike kwanza yeye baadaye. Tuliwaona akina Hayati J.K Nyerere, Karume, na Sokoine.
4. Popote akiwa ndani au nje ya taifa atasimama kulitangaza taifa lake akijisikia fahari hata katika aibu atakubali kuibeba kwaajili ya taifa lake.
5. Mzalendo si mbaguzi, havai vazi la udini wala ukabila, anavaa vazi la taifa. Hawezi kubagua ngozi wala jinsia.
6. Anajivunia taifa lake
7. Atafundisha watu kulitumikia taifa
8 Ataheshimu maoni chanya ya kila mmoja katika kujenga na kulitumikia taifa
9. Atapenda na kuheshimu haki za wengine katika taifa
10. Mzalendo lazima atalitumikia taifa kwa kufanya kazi fulani katika taifa lake.
11. Atafichua wezi, wala rushwa na mafisadi katika eneo lake analoishi au analoongoza.
12. Atakuwa jasiri (Ili uwe ngao ya kulitetea taifa sharti uwe jasiri)
13. Ataandaa/ atafundisha watoto na vijana kutetea taifa
14. Ataweka mbele utamaduni wa taifa lake
15. Atalitangaza taifa lake mbele ya mataifa mengine
16. Atatetea rasilimali za nchi
17. Atapinga unyonyaji na ukupe (Uchawa) kwani ni chembe ya unafiki na kula kwa kutegemea unyonyaji na unafiki.
18. Atahamasisha jamii yake kuelekea maendeleo makubwa
19. Atatoa mawazo ya kulijenga taifa.
20. Hatokubali kuwa tegemezi wa mtu au kitu bali kujitengenezea nafasi ya kujitegemea mwenyewe.
21. Atafikiria kizazi kijacho cha taifa kuliko anavyofikiria vizazi vya familia yake.
Na Joseph Nyoni
0766875334
Na Joseph Nyoni
Uzalendo nini? Uzalendo ni ibada ya kulipenda, kulitumikia na kulitetea taifa katika hali yoyote pamoja na kutanguliza maslahi ya taifa.
Zifuatazo ni tabia za mtu mzalendo
1. Analipenda taifa lake na hawi tayari kuliona taifa lake linaingia kwenye shida, matatizo au linaonewa, linaaibika na kunyanyasika, muda wote anaangalia faida/ maslahi ya taifa lake.
2. Kulipigania taifa linapoingia katika dhiki, shida, na kila hali
3. Mzalendo si mbinafsi! Hatangulizi mambo yake bali ya taifa. Taifa lifaidike kwanza yeye baadaye. Tuliwaona akina Hayati J.K Nyerere, Karume, na Sokoine.
4. Popote akiwa ndani au nje ya taifa atasimama kulitangaza taifa lake akijisikia fahari hata katika aibu atakubali kuibeba kwaajili ya taifa lake.
5. Mzalendo si mbaguzi, havai vazi la udini wala ukabila, anavaa vazi la taifa. Hawezi kubagua ngozi wala jinsia.
6. Anajivunia taifa lake
7. Atafundisha watu kulitumikia taifa
8 Ataheshimu maoni chanya ya kila mmoja katika kujenga na kulitumikia taifa
9. Atapenda na kuheshimu haki za wengine katika taifa
10. Mzalendo lazima atalitumikia taifa kwa kufanya kazi fulani katika taifa lake.
11. Atafichua wezi, wala rushwa na mafisadi katika eneo lake analoishi au analoongoza.
12. Atakuwa jasiri (Ili uwe ngao ya kulitetea taifa sharti uwe jasiri)
13. Ataandaa/ atafundisha watoto na vijana kutetea taifa
14. Ataweka mbele utamaduni wa taifa lake
15. Atalitangaza taifa lake mbele ya mataifa mengine
16. Atatetea rasilimali za nchi
17. Atapinga unyonyaji na ukupe (Uchawa) kwani ni chembe ya unafiki na kula kwa kutegemea unyonyaji na unafiki.
18. Atahamasisha jamii yake kuelekea maendeleo makubwa
19. Atatoa mawazo ya kulijenga taifa.
20. Hatokubali kuwa tegemezi wa mtu au kitu bali kujitengenezea nafasi ya kujitegemea mwenyewe.
21. Atafikiria kizazi kijacho cha taifa kuliko anavyofikiria vizazi vya familia yake.
Na Joseph Nyoni
0766875334