Hivi Mkuu wa Wilaya Ubungo atathibitishaje ukahaba wa hawa watu?

Bashir Yakub

Member
May 27, 2013
91
1,669
Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241.

1. Pengine utasema ni kahaba kwasababu kavaa nguo fupi sana dizaini ya chupi au nyinginezo.

Lakini hii sio ushahidi wa mtu kuwa kahaba. Tanzania hatuna Sheria inayoelekeza(regulate) mavazi. Mtu anaweza kuvaa vyovyote vile. Na pia hakuna mavazi mtu akivaa anahesabika kahaba kwa mujibu wa sheria.

2. Pengine utasema nimemkuta amesimama sehemu fulani usiku wa manane.

Kusimama nje usiku wa manane sio ushahidi wa ukahaba/ biashara ya ngono. Wengi wetu husimama na hatufanyi hizo biashara.

Pia Tanzania hakuna kosa mtu kusimama sehemu yoyote usiku wa manane labda sehemu hiyo pawe panazuiwa kusimama na mmiliki wa pale.

Na kama mmiliki wa pale ndio hapendi mtu asimame basi hiyo sio kesi ya mkuu wa wilaya bali ya mmiliki dhidi ya aliyesimama pale. Na so far sio kesi ya ukahaba bali uvamizi wa eneo(trespass).

Kusimama nje ya Baa, nje klabu, nje ya kituo cha mabasi kama Riverside, au kurandaranda nje tu, au kuwa popote nje usiku sio kosa na sio ushahidi wa kufanya biashara ya ngono. Watu kada zote husimama maeneo hayo.

3. Pengine utasema nimemkuta lodge, guest nk. Tena akiwa na mwanaume au wanaume.

Kuwa lodge,guest na mwanaume, wanaume, au peke yako sio ushahidi wa ukahaba.

Hope hata huyo mkamataji amewahi mara kadhaa kuwa maeneo kama hayo na hakukamatwa kwa kushiriki ukahaba.

Na zaidi, mwanamke kuwa ndani ya lodge au guest peke yake au na mwanaume au wanaume(3 au 4s..me) nalo sio kosa Tanzania, na hata iwe usiku wa manane ama mchana kweupe.

4. Pengine utasema nimemkuta kwenye vile vijumba wanavyopanga vya uwanja wa fisi na mwananyamala.

Si atasema mi naishi hapo. Na hata kama umemkuta na mwanaume au wanaume atasema ndio nilikuwa nao sasa kosa liko wapi. Kuwa na mwanaume au wanaume nyumbani kwangu linakuwaje kosa nchi hii. Hata ukiwakuta wanafanya kosa liko wapi, si nchi nzima ingeishia jela kama ni hivyo.

5. Ushahidi wa Ukahaba/biashara ya ngono.

Kitu pekee kinachoweza kuthibitisha kuwa mtu fulani anafanya biashara ya ngono na mtuhumiwa akapatikana na hatia bila wasiwasi ni kimoja tu. Ni mtuhumiwa mwenyewe kukubali kuwa ni kweli anafanya biashara hiyo.

Anyway, tusiseme sana lakini hili jambo ni gumu .

Namuona Mkuu wa Wilaya akiwalipa fidia ya udhalilishaji hawa viumbe.

Tunaongelea SHERIA hatutetei wala kumkandamiza yeyote.

PIA SOMA
- Vita ya DC Ubungo na Makahaba: Mgongano wa sheria, haki na maadili

- Mkuu wa Wilaya ya Ubungo adhamiria kutokomeza biashara ya ukahaba
 
Pia katiba yetu au sheria na kanuni sina imani kama zimemtaja kahaba kuwa ni kosa la madai au kosa la jinai.

Vilevile; Mkuu wa mkoa, wilaya na vongozi wengine maandamizi kuna vitu vingi vya kudeal navyo, ambavyo vina impact ya moja kwa moja kwa wananchi.

Mnapata wapi muda wa kudeal na issues kama hiz?

MyCountry
 
Ulichoandika kina mantiki. Haya mambo ya kuacha shughuli zako za msingi, na kuzunguka usiku kukamata hovyo watu waliovaa nguo fupi, waliosimama nje ya nyumba za starehe, au uliowakuta kwenye nyumba za wageni; ni upumbavu na pia dalili ya watu waliokosa kazi za kufanya.
 
Kwahiyo kero ya wananchi wa ubungo ni ukahaba. Vipi suala la maji, umeme, Barabara, Wizi na ajira kwa vijana. Mkuu wa wilaya amepewa ofisi kwa kodi za wananchi, Gari kwa kodi za wananchi, Nyumba kwa kodi za wananchi na mshahara juu bado ameona kipaumbele chake ni kukomesha ngono baina ya waliokubaliana. Kwanini wasianze na jamaa wa simuyu mkuu wa mkoa aloshtumiwa kumwingilia kinyume mwanafunzi
 
Mwanamke asiye kahaba hana vielelezo hivyo ulivyovitaja.

Mavazi ya kikahaba, usiku wa manaane, lodge ni vihashiria vya watu wa aina fulani
 
HIVI MKUU WA WILAYA UBUNGO ATATHIBITISHAJE UKAHABA WA HAWA WATU

Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241.

1. Pengine utasema ni kahaba kwasababu kavaa nguo fupi sana dizaini ya chupi au nyinginezo.

Lakini hii sio ushahidi wa mtu kuwa kahaba. Tanzania hatuna Sheria inayoelekeza(regulate) mavazi. Mtu anaweza kuvaa vyovyote vile. Na pia hakuna mavazi mtu akivaa anahesabika kahaba kwa mujibu wa sheria.

2. Pengine utasema nimemkuta amesimama sehemu fulani usiku wa manane.

Kusimama nje usiku wa manane sio ushahidi wa ukahaba/ biashara ya ngono. Wengi wetu husimama na hatufanyi hizo biashara.

Pia Tanzania hakuna kosa mtu kusimama sehemu yoyote usiku wa manane labda sehemu hiyo pawe panazuiwa kusimama na mmiliki wa pale.

Na kama mmiliki wa pale ndio hapendi mtu asimame basi hiyo sio kesi ya mkuu wa wilaya bali ya mmiliki dhidi ya aliyesimama pale. Na so far sio kesi ya ukahaba bali uvamizi wa eneo(trespass).

Kusimama nje ya Baa, nje klabu, nje ya kituo cha mabasi kama Riverside, au kurandaranda nje tu, au kuwa popote nje usiku sio kosa na sio ushahidi wa kufanya biashara ya ngono. Watu kada zote husimama maeneo hayo.

3. Pengine utasema nimemkuta lodge, guest nk. Tena akiwa na mwanaume au wanaume.

Kuwa lodge,guest na mwanaume, wanaume, au peke yako sio ushahidi wa ukahaba.

Hope hata huyo mkamataji amewahi mara kadhaa kuwa maeneo kama hayo na hakukamatwa kwa kushiriki ukahaba.

Na zaidi, mwanamke kuwa ndani ya lodge au guest peke yake au na mwanaume au wanaume(3 au 4s..me) nalo sio kosa Tanzania, na hata iwe usiku wa manane ama mchana kweupe.

4. Pengine utasema nimemkuta kwenye vile vijumba wanavyopanga vya uwanja wa fisi na mwananyamala.

Si atasema mi naishi hapo. Na hata kama umemkuta na mwanaume au wanaume atasema ndio nilikuwa nao sasa kosa liko wapi. Kuwa na mwanaume au wanaume nyumbani kwangu linakuwaje kosa nchi hii. Hata ukiwakuta wanafanya kosa liko wapi, si nchi nzima ingeishia jela kama ni hivyo.

5. Ushahidi wa Ukahaba/biashara ya ngono.

Kitu pekee kinachoweza kuthibitisha kuwa mtu fulani anafanya biashara ya ngono na mtuhumiwa akapatikana na hatia bila wasiwasi ni kimoja tu. Ni mtuhumiwa mwenyewe kukubali kuwa ni kweli anafanya biashara hiyo.

Anyway, tusiseme sana lakini hili jambo ni gumu .

Namuona Mkuu wa Wilaya akiwalipa fidia ya udhalilishaji hawa viumbe.

Tunaongelea SHERIA hatutetei wala kumkandamiza yeyote.
Bila shaka wewe ni kahaba uliyekubuhu.
 
Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241.

1. Pengine utasema ni kahaba kwasababu kavaa nguo fupi sana dizaini ya chupi au nyinginezo.

Lakini hii sio ushahidi wa mtu kuwa kahaba. Tanzania hatuna Sheria inayoelekeza(regulate) mavazi. Mtu anaweza kuvaa vyovyote vile. Na pia hakuna mavazi mtu akivaa anahesabika kahaba kwa mujibu wa sheria.

2. Pengine utasema nimemkuta amesimama sehemu fulani usiku wa manane.

Kusimama nje usiku wa manane sio ushahidi wa ukahaba/ biashara ya ngono. Wengi wetu husimama na hatufanyi hizo biashara.

Pia Tanzania hakuna kosa mtu kusimama sehemu yoyote usiku wa manane labda sehemu hiyo pawe panazuiwa kusimama na mmiliki wa pale.

Na kama mmiliki wa pale ndio hapendi mtu asimame basi hiyo sio kesi ya mkuu wa wilaya bali ya mmiliki dhidi ya aliyesimama pale. Na so far sio kesi ya ukahaba bali uvamizi wa eneo(trespass).

Kusimama nje ya Baa, nje klabu, nje ya kituo cha mabasi kama Riverside, au kurandaranda nje tu, au kuwa popote nje usiku sio kosa na sio ushahidi wa kufanya biashara ya ngono. Watu kada zote husimama maeneo hayo.

3. Pengine utasema nimemkuta lodge, guest nk. Tena akiwa na mwanaume au wanaume.

Kuwa lodge,guest na mwanaume, wanaume, au peke yako sio ushahidi wa ukahaba.

Hope hata huyo mkamataji amewahi mara kadhaa kuwa maeneo kama hayo na hakukamatwa kwa kushiriki ukahaba.

Na zaidi, mwanamke kuwa ndani ya lodge au guest peke yake au na mwanaume au wanaume(3 au 4s..me) nalo sio kosa Tanzania, na hata iwe usiku wa manane ama mchana kweupe.

4. Pengine utasema nimemkuta kwenye vile vijumba wanavyopanga vya uwanja wa fisi na mwananyamala.

Si atasema mi naishi hapo. Na hata kama umemkuta na mwanaume au wanaume atasema ndio nilikuwa nao sasa kosa liko wapi. Kuwa na mwanaume au wanaume nyumbani kwangu linakuwaje kosa nchi hii. Hata ukiwakuta wanafanya kosa liko wapi, si nchi nzima ingeishia jela kama ni hivyo.

5. Ushahidi wa Ukahaba/biashara ya ngono.

Kitu pekee kinachoweza kuthibitisha kuwa mtu fulani anafanya biashara ya ngono na mtuhumiwa akapatikana na hatia bila wasiwasi ni kimoja tu. Ni mtuhumiwa mwenyewe kukubali kuwa ni kweli anafanya biashara hiyo.

Anyway, tusiseme sana lakini hili jambo ni gumu .

Namuona Mkuu wa Wilaya akiwalipa fidia ya udhalilishaji hawa viumbe.

Tunaongelea SHERIA hatutetei wala kumkandamiza yeyote.

PIA SOMA
- Vita ya DC Ubungo na Makahaba: Mgongano wa sheria, haki na maadili

- Mkuu wa Wilaya ya Ubungo adhamiria kutokomeza biashara ya ukahaba
Waambie ukweli haya majinga!
 
Back
Top Bottom