Hii ndio sensor kuu katika gari (master sensor)

JituMirabaMinne

JF-Expert Member
May 4, 2020
3,381
9,740
Gari ina sensor nyingi sana kama MAF sensor, MAP sensor, A/F sensor, IAT sensor, ECT sensor, TPS sensor, CPS, VSS n.k.

Lakini katika hizo sensor zote kuna sensor moja tu ambayo ndio sensor kuu (master sensor). Ukuu wake unatokana na sababu kwamba sensor hiyo hutumika katika operations nyingi sana kwenye engine na baadhi kwenye automatic gearbox.

Sensor hiyo ni Engine Coolant temperature sensor (ECT sensor). Kazi ya sensor hii ni kupeleka signal ya joto la coolant kwenye control Module(PCM). Kwanza kabisa hii ndio sensor ambayo inaamua engine ioperate vipi(Yaani operating strategy ya engine). Hebu tuone baadhi ya operations ambazo zinaamuliwa na signal kutoka kwenye hii sensor.

Huenda hizo points nmezipanga vibaya lakini ni muhimu ukazisoma zote.

1. Cold start fuel enrichment

Unapowasha gari asubuhi sensor hii hupeleka signal kwenye Control module kwamba coolant ni ya baridi hivyo control module huamuru kwamba mafuta yaingie mengi kwenye engine kwa kuongeza muda wa injector nozzle kuwa wazi (Pulse width). Kama sensor hii itaharibika na ikawa inatoa signal ya cold tu basi itapelekea engine kutumia mafuta mengi sana pia kama itaharibika na ikawa inapeleka signal ya hot tu basi itapelekea misi, kuzimazima au rough idle wakati wa kuwasha gari asubuhi au wakati engine imepoa.

2. Spark advance and retard
Hii spark advance maana yake spark inakuwa released degrees chache kabla piston haijafika juu ya cylinder( yaani Top dead centre). Inasaidia sana katika performance ya engine na mambo ya emission. Kama joto ambalo engine inatakiwa kuoperate halijafikiwa basi spark advance itakuwa limited kufanya kazi.

3. Exhaust gas recirculation (EGR)
Control module ya gari haitaruhusu EGR valve kuwa wazi mpaka engine ipate joto la kutosha. Na kama ikiwa wazi wakati engine ni ya baridi inaweza kupelekea gari kumisi, rough idle au hata kuzima. Na kama ikifungwa wakati imeshapata joto inaweza kuathiri performance ya engine.

4. Open/closed loop feedbackh control of A/F ratio
Control module ya gari(PCM) inaweza kuignore signal kutoka kwenye Oxygen sensor kwamba Air/fuel ratio ni rich/lean mpaka pale engine itakapofikia joto fulani. Unapowasha gari asubuhi au muda wowote ambapo engine ni ya baridi PCM itabakia kwenye open loop na itaamuru mafuta mengi yaende kwenye engine kwa ajili ya kuboresha idle speed quality na cold driverbility. Kama PCM itashindwa kuingia kwenye closed loop pale engine itakapokuwa ya moto basi itapelekea gari kutumia mafuta mengi na kuchafua mazingira.

5. Idle speed(Silencer wakati wa baridi)
Control module ya gari itaongeza RPM wakati umewasha gari engine ikiwa ya baridi ili kuifanya engine isizime na kuboresha idle speed quality.

6. Lock up mechanism ya torque converter kwenye Automatic gearbox
Hii lock up hutokea ikiwa speed ya engine na speed ya gearbox zinafanana au zimekaribiana, yaani maana ya lock up ni kunakuwa na direct drive kati ya engine na gearbox, hii kupelekea kutokuwepo kwa joto jingi linalozalishwa kwenye torque converter na hivyo kuifanya gearbox yako iishi maisha marefu. Sasa hii lock up haitatokea ikiwa joto la engine linalohitajika halijafikiwa. Kama sensor yako ni mbovu, au umeng'oa thermostat au umeunga direct fan basi operating temperature ya engine haitafikiwa na unapunguza maisha ya gearbox yako.

7. Radiator fan(Feni ya rejeta)
Hii ndio sensor inaamua kwamba sasa feni ya rejeta iwake au izime(ukiondoa gari za zamani sana ambazo hutumia temperature switch). Hivyo kama sensor hii ikiwa mbovu feni yako inaweza isiwake kabisa au ikawaka muda wote kutegemea na signal inayopeleka kwenye control module. Kama isipowaka kabisa engine itaoverheat na kama ikiwaka muda wote engine itaoperate chini ya joto lake.

Hizo ni baadhi tu ya operations za muhimu ambazo zinafanywa na sensor hii. Hivyo unaweza kuona ni jinsi gani sensor hii ilivokuwa ina umuhimu mkubwa katika gari yako.

Kwa leo tuishie hapo.
 
Sasa hebu tushaur kuhusu service ya cvt gearbox maana mafund wanatukoroga Sana kwenye service

Mfano kama Nissan ambao ndio watumiaji wakubwa wa CVT wanashauri kubadili ATF kila baada ya 25,000 miles ambazo ni sawa na around 48,000 km. Pia asilimia kubwa ya manufacturers ambao wanamefunga CVT transmission kwenye gari zao wanashauri kubadili ATF baada ya kati ya 30,000 miles mpaka 50,000 miles ambayo ni sawa na around 48,000km mpaka 80,000km.

Hata kwa gearbox za kawaida huwa ni 15,000 miles mpaka 30,000 miles ambayo ni around 24,000km mpaka 40,000km ingawa wenye magari mengi hubadili ATF around 10,000km tu.

Lakini njia nzuri ambayo mimi ninaifahamu ni kuangalia mwonekano wa ATF ukichomoa dipstick. Na hii ni kwa automatic gearbox za aina zote.

1. Kama ni Pink basi ipo katika hali nzuri bado.

2. Kama ni brown basi itafanya kazi bila shida ila itahitaji kubadilishwa.

3. Kama ni nyeusi kimbia haraka sana ukamwage ATF uweke nyingine.
 
Sasa hebu tushaur kuhusu service ya cvt gearbox maana mafund wanatukoroga Sana kwenye service
Weka CVT fluid ya kiwanda cha gari lako. Usije ukarogwa ukaweka ATF fluid. Kama gari ni nissan weka CVT fluid ya nissan na mara nyingi dipstick ya transmission imeandikwa aina ya fluid unayotakiwa kuweka.
 
Mfano kama Nissan ambao ndio watumiaji wakubwa wa CVT wanashauri kubadili ATF kila baada ya 25,000 miles ambazo ni sawa na around 48,000 km. Pia asilimia kubwa ya manufacturers ambao wanamefunga CVT transmission kwenye gari zao wanashauri kubadili ATF baada ya kati ya 30,000 miles mpaka 50,000 miles ambayo ni sawa na around 48,000km mpaka 80,000km.

Hata kwa gearbox za kawaida huwa ni 15,000 miles mpaka 30,000 miles ambayo ni around 24,000km mpaka 40,000km ingawa wenye magari mengi hubadili ATF around 10,000km tu...
Brother, naomba uelewe kitu kimoja.

1. ATF fluid ni tofauti na CVT fluid.
2. Sio lazima CVT fluid iwe pink, kwa mfano CVT fluid na hasa ya Nissan magari madogo (NS2) huwa ina rangi ya maji ya kunywa. Na ukiweka hiyo ATF ya pink utaua gearbox.

Chonde chonde, kwenye magari ya kisasa, dip stick ya transmission huwa inaelekeza aina ya CVT au ATF fluid ya kuweka.
 
Nitakupigia pia sim lakini shidayangu ni; 1. Gari yangu ni Subaru auto gea inang,ang,ania kwenye namba 2 tu. Nimebadili CVT lakini bado. Pia taa ya check engine inawaka na mafundi wameniambia ni Oxygen sensor imekufa. Nifanye nini kurekebisha matatizo hayo? Nipo Moshi
 
Nitakupigia pia sim lakini shidayangu ni; 1. Gari yangu ni Subaru auto gea inang,ang,ania kwenye namba 2 tu. Nimebadili CVT lakini bado. Pia taa ya check engine inawaka na mafundi wameniambia ni Oxygen sensor imekufa. Nifanye nini kurekebisha matatizo hayo? Nipo Moshi
Subaru yako ipo Kwenye mfumo huu?
BG471347_c7471c.jpg
 
Brother, naomba uelewe kitu kimoja.

1. ATF fluid ni tofauti na CVT fluid.
2. Sio lazima CVT fluid iwe pink, kwa mfano CVT fluid na hasa ya Nissan magari madogo (NS2) huwa ina rangi ya maji ya kunywa. Na ukiweka hiyo ATF ya pink utaua gearbox.

Chonde chonde, kwenye magari ya kisasa, dip stick ya transmission huwa inaelekeza aina ya CVT au ATF fluid ya kuweka.


1. Mkuu nmetumia ATF tu kama general term ila ninaelewa kwamba CVT transmission zinahitaji CVT fluid. Na hata kwenye uzi wangu kabla ya huu nilishawapa watu warning kwamba ni vizuri ukajua kwamba gearbox yako inahitaji fluid ya aina gani sababu hizi transmission fluid siyo kama engine oil. Ukimess up kidogo tu biashara lazima ikukate.

20200710_221231.jpg


2. Asilimia kubwa ya hizi Transmission fluids zimetengenezwa kwa rangi ya red/pink. Ingawa nakubaliana pia na unachosema kwamba zinaweza kuwa katika rangi nyingine. Lakini suala la kuchagua rangi unayotumia bado linabakia kwako ww mtumiaji. Mfano hii picha niliyoambatanisha hapa hawa jamaa wanazalisha CVT fluid ambazo zina rangi ya green na red.

CTV-colors.png
 
1. Mkuu nmetumia ATF tu kama general term ila ninaelewa kwamba CVT transmission zinahitaji CVT fluid. Na hata kwenye uzi wangu kabla ya huu nilishawapa watu warning kwamba ni vizuri ukajua kwamba gearbox yako inahitaji fluid ya aina gani sababu hizi transmission fluid siyo kama engine oil. Ukimess up kidogo tu biashara lazima ikukate..

Nimekuelewa sana brother.

Tufikie mwafaka kwamba mwenye gari atizame CVT na ATF fluid inayotakiwa kwenye dipstick ya transimission kwenye gari lake.
 
Sasa hebu tushaur kuhusu service ya cvt gearbox maana mafund wanatukoroga Sana kwenye service
Mkuu kwenye suala la cvt transmission usiwasikize wale mwafundi wetu waliorithishana ufundi.

Hapa anagalia deep stick ya gari lako utakuta wamekuandikia.

Kama hawajakuandikia chukua Aina ya gari mafano Toyota au Nissan, chassis number, mwaka wa kutengenezwa ingia google utapata full specifications za gari yako..

Kwa wenye Nissan Note, Tiida, Wingroad, Bluebird syliph ile ya cc 1500 na nyingine nyiingi za miaka ya 2005 kuja mbele, fluid yake ni CVT FLUID NS 2 na si vinginevyo..

Bei yake ni 120000/ mpaka 140000/ kwa lita 4 kulingana unaishi wapi...Nimebadilisha mwezi uliopolita kwa 120000/-
 
Nitakupigia pia sim lakini shidayangu ni; 1. Gari yangu ni Subaru auto gea inang,ang,ania kwenye namba 2 tu. Nimebadili CVT lakini bado. Pia taa ya check engine inawaka na mafundi wameniambia ni Oxygen sensor imekufa. Nifanye nini kurekebisha matatizo hayo? Nipo Moshi

Mkuu sorry mara ya kwanza nilisoma juujuu uliposema umebadili CVT nikajua ulifunga gearbox mpya. Sasa nilipokuja kusoma vizuri baadae nikaona kwamba kumbe nilikosea.

1. Suala la gari yako kung'ang'ania kwenye gear namba mbili inaweza kuwa inasababishwa na shida kwenye primary up solenoid, valve zake au return spring yake. Hapo mpaka nifungue valve body ya hiyo gearbox nikague hivyo vitu nilivyokutajia.

2. Umesema taa ya check engine imekuwakia, Taa ya check engine inaonesha ama kuna tatizo kwenye engine au gearbox yako. Mara nyingi shida huwa ni oxygen sensor lakini kuna matatizo zaidi ya 10 ambayo yanaweza kukuwashia taa ya check engine. Na baadhi ya matatizo huwa yanapelekea gari kuingia kwenye LIMP MODE.

Gari ikiingia kwenye Limp mode baadhi ya vitu kwenye gari huwa vinazimwa ili matatizo yasiwe makubwa zaidi. Na moja ya changamoto ambayo huwa inatokea gari ikiingia kwenye limp mode ni kupata tu gear za chini yaani 1 na 2. Awe kwa gearbox yenye gear nyingi unakuta mtu anapata tu 1 mpaka 3.

Karibu sana.
 
Back
Top Bottom