KERO Headmaster shule ya Sekondari Maji ya Chai-Arumeru hafiki kazini. Walimu wengine nao hawafundishi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Sangamwalogesha

JF-Expert Member
Mar 10, 2025
557
468
Shule ya sekondari Maji ya Chai iko Halmashauri ya wilaya ya Meru, wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha.

Tusilaumu hizi shule, mazingira wala wanafunzi, mchawi mkubwa ni walimu na viongozi wao.

Shule hizi zimetelekezwa, walimu wanafanya shughuli zao binafsi, wengine wana vipindi shule binafsi. Hii shule tajwa hapo juu iko karibu kabisa na barabara kuu ya Arusha-Moshi, ni kilometa moja tu kutoka barabara kuu.

Headmaster wa hii shule haonekani shuleni, tunaambiwa ana shule yake binafsi, ni kwa nadra sana kufika kazini, ni mtoro wa kudumu.

Hii imefanya mpaka leo walimu hawajaanza kufundisha. Kwa mfano, mwalimu wa Physics wa kidato cha kwanza ameingia darasani mara moja tu na kafundisha "What is Physics" tu mpaka leo tunaenda mwezi wa nne.

Halafu tunakuja kutukana watoto wetu hawana akili? Physics kidato cha kwanza ina mada (topics) karibu kumi mpaka leo hawajafundishwa, kwanini watoto wasifeli?

Kwanini wasichukie masomo ya Sayansi? Headmaster wa hii shule na huyo mwalimu wake wa Physics ni wachawi wa watoto wetu.

Tunajua ndani ya Halmashauri kuna Afisa Elimu Sekondari, kuna wadhibiti ubora, kuna mkurugenzi. Wako wapi wasijue uhuni wote huu unafanyika?

Inawezekana tatizo limeanzia juu kwa waziri. Rais, mpeleke Dr. Dorothy Onesphory Gwajima Wizara ya Elimu, yule mama ni mwajibikaji. Prof. Mkenda anachojua ni kubadili mitaala na kutunga sera mpya, hayo ni makaratasi tu hayatasaidia kitu kama hakuna uwajibikaji.

Mtazamo na ushauri wangu, yule headmaster ashushwe, anyang'anywe ukuu, na mwalimu wa Physics wa kidato cha kwanza apewe onyo. Kama hataki kazi apishe, tuko wengi tunaojua Physics zaidi yake. Atupishe tusaidie watoto wetu kufikia ndoto zao.

Afisa Elimu wa pale Meru ni jamaa moja yuko na makogo tu, anafikiri cheo ni egoism, siyo kazi. Yule jamaa hajitambui, apelekwe DEO mwingine anayejua wajibu wake. Wale wadhibiti ubora waondolewe pale, kazi yao ni umbea na kusubiri muda wa chai na lunch.

Hawa viongozi wote niliowataja watoto wao wako private huku wanakula kodi zetu. Wawafuate watoto wao waliko, wafanye kazi huko.
 
Second Master si yupo? Labda Headmaster ana dharura, mi nikiwa shule fulani hapahapa Arusha Olevel kwanzia Form 1 hadi 3 nilikua sijawahi kumuona Headmistress shuleni hata sura yake nilikua siijui kumbe yule Mama alikua anamuuguza mume wake huko India kwa miaka yote alirudi tuko form 4 ndo namuona kwa mara ya kwanza, shughuli zote za utawala akawa anafanya Msaidizi wake.

Alafu hao ni watawala siyo kila siku anakua shuleni siku zingine ataenda kwenye vikao au seminar mbalimbali , sidhani Headmaster wa shule iliyo mjini kama hiyo anaweza kujiamulia tu kutokwenda shule.
 
Wakikaa mda wote shule na kuwafundisha watoto zenu mnakuja JF kuwasema wana maisha magumu wanatia aibu.

Na kwa kuwa shule hakuna cha kuiba(kupiga dili)sasa na wao wanaamua kuingia mtaani kutafuta pesa ili msiwasakame.

Na hii ni kwa shule nyingi sio hiyo tu.
 
Shule ya sekondari Maji ya Chai iko Halmashauri ya wilaya ya Meru, wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha.

Tusilaumu hizi shule, mazingira wala wanafunzi, mchawi mkubwa ni walimu na viongozi wao.

Shule hizi zimetelekezwa, walimu wanafanya shughuli zao binafsi, wengine wana vipindi shule binafsi. Hii shule tajwa hapo juu iko karibu kabisa na barabara kuu ya Arusha-Moshi, ni kilometa moja tu kutoka barabara kuu.

Headmaster wa hii shule haonekani shuleni, tunaambiwa ana shule yake binafsi, ni kwa nadra sana kufika kazini, ni mtoro wa kudumu.

Hii imefanya mpaka leo walimu hawajaanza kufundisha. Kwa mfano, mwalimu wa Physics wa kidato cha kwanza ameingia darasani mara moja tu na kafundisha "What is Physics" tu mpaka leo tunaenda mwezi wa nne.

Halafu tunakuja kutukana watoto wetu hawana akili? Physics kidato cha kwanza ina mada (topics) karibu kumi mpaka leo hawajafundishwa, kwanini watoto wasifeli?

Kwanini wasichukie masomo ya Sayansi? Headmaster wa hii shule na huyo mwalimu wake wa Physics ni wachawi wa watoto wetu.

Tunajua ndani ya Halmashauri kuna Afisa Elimu Sekondari, kuna wadhibiti ubora, kuna mkurugenzi. Wako wapi wasijue uhuni wote huu unafanyika?

Inawezekana tatizo limeanzia juu kwa waziri. Rais, mpeleke Dr. Dorothy Onesphory Gwajima Wizara ya Elimu, yule mama ni mwajibikaji. Prof. Mkenda anachojua ni kubadili mitaala na kutunga sera mpya, hayo ni makaratasi tu hayatasaidia kitu kama hakuna uwajibikaji.

Mtazamo na ushauri wangu, yule headmaster ashushwe, anyang'anywe ukuu, na mwalimu wa Physics wa kidato cha kwanza apewe onyo. Kama hataki kazi apishe, tuko wengi tunaojua Physics zaidi yake. Atupishe tusaidie watoto wetu kufikia ndoto zao.

Afisa Elimu wa pale Meru ni jamaa moja yuko na makogo tu, anafikiri cheo ni egoism, siyo kazi. Yule jamaa hajitambui, apelekwe DEO mwingine anayejua wajibu wake. Wale wadhibiti ubora waondolewe pale, kazi yao ni umbea na kusubiri muda wa chai na lunch.

Hawa viongozi wote niliowataja watoto wao wako private huku wanakula kodi zetu. Wawafuate watoto wao waliko, wafanye kazi huko.
Mind your Business ndugu.
Huu ni umbea na hauna masirahi zaidi utakufa mda si mrefu kwa kubeba mizigo isiyo yako
 
Shule ya sekondari Maji ya Chai iko Halmashauri ya wilaya ya Meru, wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha.

Tusilaumu hizi shule, mazingira wala wanafunzi, mchawi mkubwa ni walimu na viongozi wao.

Shule hizi zimetelekezwa, walimu wanafanya shughuli zao binafsi, wengine wana vipindi shule binafsi. Hii shule tajwa hapo juu iko karibu kabisa na barabara kuu ya Arusha-Moshi, ni kilometa moja tu kutoka barabara kuu.

Headmaster wa hii shule haonekani shuleni, tunaambiwa ana shule yake binafsi, ni kwa nadra sana kufika kazini, ni mtoro wa kudumu.

Hii imefanya mpaka leo walimu hawajaanza kufundisha. Kwa mfano, mwalimu wa Physics wa kidato cha kwanza ameingia darasani mara moja tu na kafundisha "What is Physics" tu mpaka leo tunaenda mwezi wa nne.

Halafu tunakuja kutukana watoto wetu hawana akili? Physics kidato cha kwanza ina mada (topics) karibu kumi mpaka leo hawajafundishwa, kwanini watoto wasifeli?

Kwanini wasichukie masomo ya Sayansi? Headmaster wa hii shule na huyo mwalimu wake wa Physics ni wachawi wa watoto wetu.

Tunajua ndani ya Halmashauri kuna Afisa Elimu Sekondari, kuna wadhibiti ubora, kuna mkurugenzi. Wako wapi wasijue uhuni wote huu unafanyika?

Inawezekana tatizo limeanzia juu kwa waziri. Rais, mpeleke Dr. Dorothy Onesphory Gwajima Wizara ya Elimu, yule mama ni mwajibikaji. Prof. Mkenda anachojua ni kubadili mitaala na kutunga sera mpya, hayo ni makaratasi tu hayatasaidia kitu kama hakuna uwajibikaji.

Mtazamo na ushauri wangu, yule headmaster ashushwe, anyang'anywe ukuu, na mwalimu wa Physics wa kidato cha kwanza apewe onyo. Kama hataki kazi apishe, tuko wengi tunaojua Physics zaidi yake. Atupishe tusaidie watoto wetu kufikia ndoto zao.

Afisa Elimu wa pale Meru ni jamaa moja yuko na makogo tu, anafikiri cheo ni egoism, siyo kazi. Yule jamaa hajitambui, apelekwe DEO mwingine anayejua wajibu wake. Wale wadhibiti ubora waondolewe pale, kazi yao ni umbea na kusubiri muda wa chai na lunch.

Hawa viongozi wote niliowataja watoto wao wako private huku wanakula kodi zetu. Wawafuate watoto wao waliko, wafanye kazi huko.
Bila shaka utakua mwalimu tu wewe mna roho za chuki sana nyie wapumbavu
 
% kubwa ya wafanyakazi wa serikali hawafiki kazini na hata wakifika either wanachelewa na pia hawafanyi kilichowapeleka.

Huo ndiyo ukweli mchungu.
 
Kila siku ni walimu tu
Kwa sababu wao ndio wametufikisha hapa tulipo tukianza na aliyeingiza nchi kwenye chaka tangia ile 1961 ni alikuwa mwalimu, anayesimamia chaguzi/kuandikisha wapiga kura na kupendelea CCM ni walimu, na aliyesema wahitimu wa vyuo vikuu wakimaliza degree zao waende VETA ni mwalimu
 
Serikali iwalipe vizuri walimu kuliko fani nyingine yoyote.

Binasfi ningekuwa sihudhurii kazini kama maslahi sio mazuri.
 
Kuna wahusika uliowataja hapo ndio uliopaswa uwafikishe hizo tuhuma zako ili waweze kufanya ufuatiliaji na sio kuja kubwaga mitandaoni hapa
 
Kama una mtoto pale we fanya kumtafutia shule nyingine man ikiwa bado mapema.Sema si kiongozi mkuu alisema kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake,sasa huu ndio urefu wa kamba zao.

Pesa wanayowalipa ndogo acha kama wanajitafutia sehemu nyingine kipato wafanye hivyo.Japo wanasema kazi ya walimu ni wito
 
Shule ya sekondari Maji ya Chai iko Halmashauri ya wilaya ya Meru, wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha.

Tusilaumu hizi shule, mazingira wala wanafunzi, mchawi mkubwa ni walimu na viongozi wao.

Shule hizi zimetelekezwa, walimu wanafanya shughuli zao binafsi, wengine wana vipindi shule binafsi. Hii shule tajwa hapo juu iko karibu kabisa na barabara kuu ya Arusha-Moshi, ni kilometa moja tu kutoka barabara kuu.

Headmaster wa hii shule haonekani shuleni, tunaambiwa ana shule yake binafsi, ni kwa nadra sana kufika kazini, ni mtoro wa kudumu.

Hii imefanya mpaka leo walimu hawajaanza kufundisha. Kwa mfano, mwalimu wa Physics wa kidato cha kwanza ameingia darasani mara moja tu na kafundisha "What is Physics" tu mpaka leo tunaenda mwezi wa nne.

Halafu tunakuja kutukana watoto wetu hawana akili? Physics kidato cha kwanza ina mada (topics) karibu kumi mpaka leo hawajafundishwa, kwanini watoto wasifeli?

Kwanini wasichukie masomo ya Sayansi? Headmaster wa hii shule na huyo mwalimu wake wa Physics ni wachawi wa watoto wetu.

Tunajua ndani ya Halmashauri kuna Afisa Elimu Sekondari, kuna wadhibiti ubora, kuna mkurugenzi. Wako wapi wasijue uhuni wote huu unafanyika?

Inawezekana tatizo limeanzia juu kwa waziri. Rais, mpeleke Dr. Dorothy Onesphory Gwajima Wizara ya Elimu, yule mama ni mwajibikaji. Prof. Mkenda anachojua ni kubadili mitaala na kutunga sera mpya, hayo ni makaratasi tu hayatasaidia kitu kama hakuna uwajibikaji.

Mtazamo na ushauri wangu, yule headmaster ashushwe, anyang'anywe ukuu, na mwalimu wa Physics wa kidato cha kwanza apewe onyo. Kama hataki kazi apishe, tuko wengi tunaojua Physics zaidi yake. Atupishe tusaidie watoto wetu kufikia ndoto zao.

Afisa Elimu wa pale Meru ni jamaa moja yuko na makogo tu, anafikiri cheo ni egoism, siyo kazi. Yule jamaa hajitambui, apelekwe DEO mwingine anayejua wajibu wake. Wale wadhibiti ubora waondolewe pale, kazi yao ni umbea na kusubiri muda wa chai na lunch.

Hawa viongozi wote niliowataja watoto wao wako private huku wanakula kodi zetu. Wawafuate watoto wao waliko, wafanye kazi huko.
Watu km hao ndio wanafanya shule za serikali kuonekana vioja, hao wapuuzi washughulikiwe ipasavyo. Mh. Rais abadilishe uongozi hasa waziri, waziri ajaye afanye overhaul. Ndio wanafunzi wameanza mtaala mpya lakini walimu hawaingii darasani? Km mtu hataki kazi aondoke au aondolewe aendelee na mambo yake huko mitaani. Mtoto wangu yuko private form one somo hilo la Physics wameshasoma Introduction to Physics, Measurement, Introduction to Force na sasa hivi wako wanasoma Density and Relative Density, Form One kuna Chapters 9. Kwa hali hiyo kila mzazi mwenye uwezo hawezi kumpeleka mtoto wake shule ya serikali, shule za serikali zitabaki kuwa za walalahoi, hii ni laana kubwa kwa nchi yetu
 
Back
Top Bottom