Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,752
- 121,800
Wanabodi
Leo naendelea na zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa". Sisi watu sekta binafsi, tunaotegemea tenders, kuna siku unaamka asubuhi, huna tenda, huna kazi, huna hili wala lile, uko kitandani, ndipo unaamua kuamka na Jf, wakati ukisubiri saa 12:00 asubuhi uanze kusikiliza morning news.
Kuna msemo "beggars cannot be choosers" kumaanisha ukiwa omba omba, huwezi kuchagua usaidiwe na nani na usaidiwe nini, wewe kazi yako ni kutembeza tuu bakuli kuomba tuu, chochote utakachopewa au kusaidiwa unapokea na kazi yako ni kusema tuu "hewala*, " asante". Hivyo Tanzania as beggars as we were, we had no choice but to bow down to IMF and World Bank and beg for mercy.
That was then, Nyerere aliwahi kuwakatalia Waingereza kutuingilia, wakati wa mgogoro wa Jimbo la Biafra nchini Nigeria, na akarejesha misaada yao, na kuvunja uhusiano wetu na wao wa kibalozi.
Pia Nyerere aliwahi kuwakatalia Wajerumani walipotaka kutuchagulia marafiki. Kabla ya Muungano, Tanzania ilikuwa na Ubalozi wa Ujerumani Magharibi, na Zanzibar ilikuwa na ubalozi wa Ujerumani Mashariki. Kutokana na ugomvi wao, hadi kujenga ukuta jiji la Berlin, kila watu na upande wao, nchi ikiwa na ubalozi wa nchi moja nyingine inajitoa. Hiyo tulipoungana na Zanzibar, Tanzania tukawa na balozi zote mbili, Ujerumani Magharibu wakatulazimisha kuwafukuza Ujerumani Mashariki, Nyerere aliwagomea, akawarudishia misaada yao na kuwaambia kama hawataki wao ndio waondoke.
Hata mashirika ya kibeberu ya IMF na WB, aliwakatalia kutokana na masharti yao, ila kibano kilipozidi akaamua, kuliko kugeuka nyuma akageuka jiwe la chumvi, bora ang'atuke na kupisha wengine, Mwinyi alipoingia, Ali bow down kwa kufungulia ruhsa zote.
Mambo ya Nyerere na Mashirika ya kimataifa kama World Bank, sasa yanataka kurejeshwa kiaina. Rais Magufuli tangu ameingia, amebana mianya yote ya upigaji hadi vyuma vimekaza, sasa haya mashirika kwa kuanzia na WB wanataka kuleta za kuleta kwa kutishia nyau watu wazima. Baada ya kukosa mahali popote pa kumshikia bango rais Magufuli, sasa wanataka kuzitumia baadhi ya kauli zake kama bangusilo la kutunyima mikopo.
Kama hii taarifa ya CNN eti World Bank wanatunyima mkopo wa dola Milioni 300 kuboresha elimu, kwa sababu Rais Magufuli alisema mwanafunzi atakaeshika ujauzito akiwa shule, masomo basi. Serikali yake haitasomesha.
Kwa mambo kama haya ya nchi yetu kuadhibiwa kwa kauli za ukweli za rais wetu, jee kuna haja ya washauri wa rais, wamshauri rais wetu kutafakari baadhi ya kauli zake, ili kuepusha hizi sintofahamu za kimataifa ambazo baadhi zinaanza kutugharimu kama hivi, au kwa vile Tanzania ni nchi huru, a sovereign state, kulinda uhuru wetu na heshima ya nchi yetu, tusikubali nchi yetu inyanyaswe kwa kunyimwa mikopo na misaada yenye masharti magumu ya kuingilia uhuru wetu na uhuru wa rais wetu ambaye ni mkweli daima, aendelee kuwa huru kusema chochote popote regardless of the consequences?.
Hili rais Magufuli kusema chochote popote, pia niliwahi kushauri
Jee Aachwe Aseme Tuu, By "Taking The Bitter With The Sweet", Or Atumie Busara?!. - JamiiForums
Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake! . - JamiiForums
Jumatano Njema.
Paskali
Leo naendelea na zile makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa". Sisi watu sekta binafsi, tunaotegemea tenders, kuna siku unaamka asubuhi, huna tenda, huna kazi, huna hili wala lile, uko kitandani, ndipo unaamua kuamka na Jf, wakati ukisubiri saa 12:00 asubuhi uanze kusikiliza morning news.
Kuna msemo "beggars cannot be choosers" kumaanisha ukiwa omba omba, huwezi kuchagua usaidiwe na nani na usaidiwe nini, wewe kazi yako ni kutembeza tuu bakuli kuomba tuu, chochote utakachopewa au kusaidiwa unapokea na kazi yako ni kusema tuu "hewala*, " asante". Hivyo Tanzania as beggars as we were, we had no choice but to bow down to IMF and World Bank and beg for mercy.
That was then, Nyerere aliwahi kuwakatalia Waingereza kutuingilia, wakati wa mgogoro wa Jimbo la Biafra nchini Nigeria, na akarejesha misaada yao, na kuvunja uhusiano wetu na wao wa kibalozi.
Pia Nyerere aliwahi kuwakatalia Wajerumani walipotaka kutuchagulia marafiki. Kabla ya Muungano, Tanzania ilikuwa na Ubalozi wa Ujerumani Magharibi, na Zanzibar ilikuwa na ubalozi wa Ujerumani Mashariki. Kutokana na ugomvi wao, hadi kujenga ukuta jiji la Berlin, kila watu na upande wao, nchi ikiwa na ubalozi wa nchi moja nyingine inajitoa. Hiyo tulipoungana na Zanzibar, Tanzania tukawa na balozi zote mbili, Ujerumani Magharibu wakatulazimisha kuwafukuza Ujerumani Mashariki, Nyerere aliwagomea, akawarudishia misaada yao na kuwaambia kama hawataki wao ndio waondoke.
Hata mashirika ya kibeberu ya IMF na WB, aliwakatalia kutokana na masharti yao, ila kibano kilipozidi akaamua, kuliko kugeuka nyuma akageuka jiwe la chumvi, bora ang'atuke na kupisha wengine, Mwinyi alipoingia, Ali bow down kwa kufungulia ruhsa zote.
Mambo ya Nyerere na Mashirika ya kimataifa kama World Bank, sasa yanataka kurejeshwa kiaina. Rais Magufuli tangu ameingia, amebana mianya yote ya upigaji hadi vyuma vimekaza, sasa haya mashirika kwa kuanzia na WB wanataka kuleta za kuleta kwa kutishia nyau watu wazima. Baada ya kukosa mahali popote pa kumshikia bango rais Magufuli, sasa wanataka kuzitumia baadhi ya kauli zake kama bangusilo la kutunyima mikopo.
Kama hii taarifa ya CNN eti World Bank wanatunyima mkopo wa dola Milioni 300 kuboresha elimu, kwa sababu Rais Magufuli alisema mwanafunzi atakaeshika ujauzito akiwa shule, masomo basi. Serikali yake haitasomesha.
Tena hizo $ Milioni 300 ambazo WB wanataka kutunyanyasia, sisi tunazipata kwa siku moja tuu, kwa rais Magufuli kumkumbusha tuu Prof Richard Thornton atimize ile ahadi yake.Baadhi ya kauli za rais wetu, Dr. John Pombe Joseph Magufuli zimeanza kutu cost kama taifa, kwa baadhi ya kauli hizo kutumika kama bangusilo la kutunyima mikopo, hivyo kuti cost na kulicost taifa. moja vya cost hizo ni hii
CNN: Tanzania loses $300m World Bank loan amid crackdown concerns - JamiiForums
Ya Mkuu Tang Zhou,
Hawa WB kama wana yao, nao ikibidi, waende zao tuu, hawawezi kutunyima mkopo wa elimu kwa kisingizio cha kauli ya Rais Magufuli kukataa mimba za utotoni. Tanzania tangu tumepata uhuru, hatujawahi kuruhusu pregnant girls kuendelea na masomo shule zile zile, alichokisema rais Magufuli sio kitu kipya, ni kuusisitiza tuu kitu kile kile kilichokuwepo miaka yote, sasa iweje hawa WB, wazuie mkopo huo muhimu sana wa elimu kwa kisingizio cha sababu hizo?!, hawa nao wana yao, kama wana yao waseme tuu, vinginevyo nao tuwafungulie tuu milango, kuwaonyesha njia ya kutokea na ikibidi kuondoka, nao waondoke tuu, kama Nyerere aliweza nchi ikiwa with nothing, Magufuli atashindwaje sasa nchi ina everything?.
Mwalimu Nyerere aliwahi kuwagomea mabeberu hawa na Mashirika yao ya kimataifa, IMF na WB, japo tuliteseka, bora tuteseke huru kuliko kulishwa tukashibishwa utumwani.
Watanzania tusimame na rais wetu, kamwe tusikubali, nchi yetu na
rais wetu kupangiwa nini aseme na nini asiseme kisa kuogopa kunyimwa mikopo na misaada yenye masharti.
Japo katika hili la pregnant girls kunyimwa fursa za kuendelea na masomo, mimi siliungi mkono kauli ya Rais Magufuli, naiunga mkono ilani ya uchaguzi ya CCM na niliuliza hapa
Jee Kitendo Cha Kukiuka Ilani ya CCM Bila Kikao Chochote, Sio Udikiteta?. - JamiiForums
Lakini pamoja na kutomuunga mkono rais Magufuli kwenye hili, ila ninamwelewa ana maanisha nini, hivyo kupinga media za nje zinazo shadadia sana mimba za utotoni na hapa nimewapinga,
Huku sio kudhalilishwa kwa Rais wetu na Media za Nje? Je, watanzania tukubali, Tukae kimya? - JamiiForums
Lakini hili la rais wetu kupangiwa nini cha kusema ili asiwaudhi wakubwa hawa, nasimama na rais Magufuli.
Mwalimu Nyerere alipowagomea IMF na World Bank, enzi zile, Tanzania tuliteseka kwa sababu tulikuwa nchi changa, nchi masikini with nothing, lakini sasa Tanzania sio changa tena, sasa Tanzania ni nchi tajiri with everything, madini, gesi asili, ardhi yenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, maliasli za kutosha, watu tunao etc, hivyo hatuwezi kutishwa na yeyote kwa rais wetu kupangiwa cha kuongea.
Kwa mambo kama haya ya nchi yetu kuadhibiwa kwa kauli za ukweli za rais wetu, jee kuna haja ya washauri wa rais, wamshauri rais wetu kutafakari baadhi ya kauli zake, ili kuepusha hizi sintofahamu za kimataifa ambazo baadhi zinaanza kutugharimu kama hivi, au kwa vile Tanzania ni nchi huru, a sovereign state, kulinda uhuru wetu na heshima ya nchi yetu, tusikubali nchi yetu inyanyaswe kwa kunyimwa mikopo na misaada yenye masharti magumu ya kuingilia uhuru wetu na uhuru wa rais wetu ambaye ni mkweli daima, aendelee kuwa huru kusema chochote popote regardless of the consequences?.
Hili rais Magufuli kusema chochote popote, pia niliwahi kushauri
Jee Aachwe Aseme Tuu, By "Taking The Bitter With The Sweet", Or Atumie Busara?!. - JamiiForums
Wasaidizi wa Rais, Please Msaidieni Rais Wetu Kwenye Public . Msimuachie Kila Kitu Peke Yake! . - JamiiForums
Jumatano Njema.
Paskali