Hata makondakta wa daladala wana D2, na kwa hili wamesomea CUBA

RIGHT MARKER

Member
Apr 30, 2018
50
236
Mhadhara 31:
Leo naomba niwajuze abiria wa daladala jambo ambalo makondakta wamesomea CUBA, na jinsi ambavyo wanatumia vizuri D2 za shuleni.

1. Matumizi ya D2:
Kumbukumbu walizonazo makondakta (tingo) za kuwakumbuka abiria wote ambao tayari wamewatoza nauli, na abiria ambao bado hawajawatoza nauli. Kwenye hili naamini makondakta wote wana D2 za Historia na Hisabati. Kwasababu si rahisi kondakta kumsahau kumdai abiria nauli hata kama abiria ataingia kupitia dirishani.

2. Walichosomea CUBA:
Kuna hiki kitu ambacho makondakta wamekisomea CUBA na huenda baadhi ya abiria hawajakigundua hasa kwa wale abiria wa mabus madogo ya mikoani. Kondakta (Tingo) anapochukua nauli ya abiria ambayo inahitaji kurudishwa chenji huwa anajichelewesha kurudisha chenji.

Kwa mfano nauli ya safari ni Tsh 1,000, wewe umempa Tsh 5,000 au 10,000; hata kama chenji anazo mkononi kamwe hawezi kukurudishia papo hapo mpaka wewe mwenyewe umkumbushe kondakta, hii ipo sana kwa makondakta wa mikoani tofauti na hapa DSM.

Hapa niwajuze abiria kuwa si kwamba kondakta amesahau kukurudishia chenji yako, bali ile ni mbinu waliosomea makondakta huko CUBA. Unaweza kudhani amesahau kumbe yeye ndo anataka wewe usahau ili iwe faida kwake.

Right Marker
Dar es salaam
 
Mh wapi hiyo!! huku kwetu makondakta ikiwa wameelemewa wakifika mwisho hua wanatangaza kabisa anaedai chenji ni nani?
 
Kondakta huwa wanaamini abiria wote ni masikini ndio maana huwa wanajibu ovyo
Wako sahihi hakuna tajiri anapanda daladala,au kiongozi mkubwa anayepanda daladala
Usafiri wadaladala kwa DSM,panoja na mwendokasini kwa DSM ni kwa masikinj
 
Kondakta huwa wanaamini abiria wote ni masikini ndio maana huwa wanajibu ovyo
Wako sahihi hakuna tajiri anapanda daladala,au kiongozi mkubwa anayepanda daladala
Usafiri wadaladala kwa DSM,panoja na mwendokasini kwa DSM ni kwa masikinj
daah,
nimelia sana mkuu.
 
Mhadhara 31:
Leo naomba niwajuze abiria wa daladala jambo ambalo makondakta wamesomea CUBA, na jinsi ambavyo wanatumia vizuri D2 za shuleni.

1. Matumizi ya D2:
Kumbukumbu walizonazo makondakta (tingo) za kuwakumbuka abiria wote ambao tayari wamewatoza nauli, na abiria ambao bado hawajawatoza nauli. Kwenye hili naamini makondakta wote wana D2 za Historia na Hisabati. Kwasababu si rahisi kondakta kumsahau kumdai abiria nauli hata kama abiria ataingia kupitia dirishani.

2. Walichosomea CUBA:
Kuna hiki kitu ambacho makondakta wamekisomea CUBA na huenda baadhi ya abiria hawajakigundua hasa kwa wale abiria wa mabus madogo ya mikoani. Kondakta (Tingo) anapochukua nauli ya abiria ambayo inahitaji kurudishwa chenji huwa anajichelewesha kurudisha chenji.

Kwa mfano nauli ya safari ni Tsh 1,000, wewe umempa Tsh 5,000 au 10,000; hata kama chenji anazo mkononi kamwe hawezi kukurudishia papo hapo mpaka wewe mwenyewe umkumbushe kondakta, hii ipo sana kwa makondakta wa mikoani tofauti na hapa DSM.

Hapa niwajuze abiria kuwa si kwamba kondakta amesahau kukurudishia chenji yako, bali ile ni mbinu waliosomea makondakta huko CUBA. Unaweza kudhani amesahau kumbe yeye ndo anataka wewe usahau ili iwe faida kwake.

Right Marker
Dar es salaam
Makondakta wengi hawana heshima kabisa walimdhalilisha baba mmoja wa makamo kwenye daladala ila nikama alitutukana wote mule ndani..

Ilikuwa hivi,
mzee:
alimwambia konda kwa kufoka mbona umenipitiliza kituo na mbona utangazi vituo we konda gani wewe,
Konda:
Kwani mzee kituo chako ukikiona si ungesema alafu maisha yako yenyewe ni ya mia sita alafu unataka kuniendesha hapa..

Yule mzee alinyamaza kimya..ila ni kama alitusimanga wote kweny ile daladala..toka siku ile niliapa ata kukopa nitakopa ili nimiliki gari kudharirishana vile isee.
 
Makondakta wengi hawana heshima kabisa walimdhalilisha baba mmoja wa makamo kwenye daladala ila nikama alitutukana wote mule ndani..

Ilikuwa hivi,
mzee:
alimwambia konda kwa kufoka mbona umenipitiliza kituo na mbona utangazi vituo we konda gani wewe,
Konda:
Kwani mzee kituo chako ukikiona si ungesema alafu maisha yako yenyewe ni ya mia sita alafu unataka kuniendesha hapa..

Yule mzee alinyamaza kimya..ila ni kama alitusimanga wote kweny ile daladala..toka siku ile niliapa ata kukopa nitakopa ili nimiliki gari kudharirishana vile isee.
😀😀
 
Makondakta wengi hawana heshima kabisa walimdhalilisha baba mmoja wa makamo kwenye daladala ila nikama alitutukana wote mule ndani..

Ilikuwa hivi,
mzee:
alimwambia konda kwa kufoka mbona umenipitiliza kituo na mbona utangazi vituo we konda gani wewe,
Konda:
Kwani mzee kituo chako ukikiona si ungesema alafu maisha yako yenyewe ni ya mia sita alafu unataka kuniendesha hapa..

Yule mzee alinyamaza kimya..ila ni kama alitusimanga wote kweny ile daladala..toka siku ile niliapa ata kukopa nitakopa ili nimiliki gari kudharirishana vile isee.
Konda yuko sahihi,tumieni ujana vizuri,unafikishaje miaja 60 huna hata pikipiki boxer used milioni moja,au kamkweche ka milioni nne,konda yuko sahihi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom