Gonjwa ripoti za CAG linataka operesheni

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,160
Sunday, April 16, 2017
Gonjwa ripoti za CAG linataka operesheni




Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Juma Assad

By Mwananchi


Mwaka jana, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Juma Assad alipotoa ripoti yake ikionyesha udhaifu mkubwa katika matumizi ya fedha na mali za umma, tuliandika maoni hapa tukisema “Tunataka kuona mabadiliko katika ripoti za CAG”.

Juzi, Profesa Assad aliwasilisha bungeni ripoti yake nyingine ya mwaka, ambayo kama ile iliyotangulia na nyingine za awali, mambo bado ni yale yale au pengine yamekuwa makubwa zaidi.

Kinyume na matarajio yetu kwamba katika awamu hii ambayo Rais amejipambanua kwa kupambana na rushwa, ubadhirifu na kupiga ‘dili’ serikalini mambo yangebadilika, CAG Assad amesema mambo bado na kuwa kati ya mapendekezo 234 yaliyotolewa, 32 pekee (asilimia 14) ndiyo yametekelezwa kikamilifu.

Miongoni mwa kasoro zinazobainishwa katika ripoti hiyo ni kukua kwa Deni la Taifa kwa asilimia 20 na kufikia Sh41 trilioni, ambalo CAG ameonya iwapo hakutakuwa na udhibiti, litaathiri uwezo wa Serikali kwenye matumizi ya maendeleo kwa miaka ijayo.

Licha ya ukuaji wake, deni hilo halijajumuisha Sh3.2 trilioni ambazo ni madeni ya mifuko ya hifadhi ya jamii na madeni mengine ya Sh225.6 bilioni ambayo hayajalipwa na yana dhamana ya Serikali.

Vilevile, CAG amebainisha pia matumizi mabaya ya misamaha ya kodi, kuyeyuka mapato ya ushuru, ufisadi katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa na malipo ya Sh7.3 bilioni kwa wafanyakazi hewa.

Ripoti hiyo pia kati ya mengi inaonyesha ukata katika ofisi za ubalozi, kushuka kwa uwekezaji kwa mifuko ya hifadhi ya jamii, udhaifu katika usimamizi wa fedha za Serikali na Serikali kuwa mdaiwa mkubwa wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa).

Vilevile, CAG amebainisha jambo ambalo wabunge wamekuwa wakilisema kuhusu uhalisia wa Bajeti ya Serikali na ameishauri Serikali kuwa na bajeti inayoakisi uhalisia kuliko ilivyo sasa, ili kupunguza nakisi ya bajeti na madeni.

Mathalani, Bajeti ya Serikali ya mwaka 2016/17 ilipanda hadi Sh29.5 trilioni kutoka Sh22.5 trilioni ya mwaka 2015/16 huku wabunge wakisema fedha zilizotolewa kwenye shughuli za maendeleo ni chini ya nusu ya zilizotengwa.

Kinachoshangaza katika ripoti hii ni hali kuendelea licha ya mapambano ya Rais John Magufuli dhidi ya uozo huo tangu aingie madarakani.

Nani asiyejua kuwa hadi sasa Rais amekuwa akitengua uteuzi au kusimamisha watumishi wa Serikali wanaobainika kuhusika katika ubadhirifu wa fedha za umma, wazembe, wafanyakazi hewa na kuchukua hatua kupunguza Deni la Taifa?

Na haya yanatokea kipindi ambacho tunaelezwa kuwa bajeti ya ofisi ya CAG imepungua na hivyo kushindwa kuyafikia baadhi ya maeneo ya ukaguzi, pengine yangefikiwa tungeona makubwa zaidi.

Tunadhani hatua za ziada zitatakiwa kufanyika kwa operesheni maalumu ili kukomesha upungufu unaojitokeza katika kila uchao.

Miongoni mwa hatua hizo ni kuwekeza katika maadili ya mtu mmoja mmoja na maadili ya Taifa, kuhakikisha watumishi wanalipwa kiwango kinachostahili kulingana na gharama za maisha, huku Serikali ikifanya kila linalowezekana kudhibiti mfumuko wa bei na kuwezesha upatikanaji wa hudumu muhimu kwa gharama nafuu.

Endapo hayo yatafanyiwa kazi tunaweza kuondokana na uozo huo kwa kudhibiti rushwa, ufisadi na kusimamia vizuri mikataba ya uwekezaji.
 
Kweli Stomatollogia, najiuliza ksbb EL alisemwa ndiye mhusika wa kila ufisadi. Sasa ni takriban miaka 10 nje ya ccm na serikali yake lkn madudu yanaongezeka kila kukucha.

Raisi awamu hii aliahidi pesa ya umma hiitapotea hata shilingi moja sasa yako wapI?. Tukaaminishwa nidhamu serikalini imerejeshwa, je ni nidhamu ipi?. Nyie CCM nyie, kama madudu yameanza mapema hiv ,itakuwaje mwaka 2018/2019 wakati chama kinatafuta fedha za uchaguzi mkuu 2020?.

Pole sana ndg EL kwa kufanywa mbuzi wa kafara na awamu ya nne pia kamati ya Mwakyembe ambayo haikutaka hata kukihoji magogoni ingawa ilikwenda hadi ulaya kukusanya data.
 
Kwanini unashangaa mkuu??
Kwani report ya CAG ya ukaguzi wa hesabu Za mapato Na matumizi ya CDM nayo imekushangaza pia??
 
Ile mahakama nafikiri ilianzishwa kwa nia njema lkn baadaye DPP kawambia itawafunga CCM wote mpk aliyeiasisi akiwemo yeye DPP, kufikia hapo utakuwa umejua kwnn Mwakiembe alisema imekosa mshitakiwa.
 
THEGAME inanishangaza kwsbb ccm ndio chama dola. Hivo kikijiwajibisha kwanza chenyewe nirahisi kumwajibisha CDM na chama chochote kipatacho ruzuku toka sserikalini .
 
Kwani waliomsema ni CCM au CHADEMA?
 
Kazi nzuri ya CAG, Wahusika wajiangalie na Kujirekebisha.
Kwa sababu Mkuu alisema Kipindi kijacho anataka mavitabu ya REPORTS za CAG yapungue, Ngoja tuone nini kitafanyika...
 
Kilio ukata wiki ya tatu bungeni
www.ippmedia.com/sw/habari/kilio-ukata-wiki-ya-tatu-bungeni


Hata hivyo, wakati hali ikionekana kuwa kero kwa chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) hadi kulazimika kuwazuia wabunge wake kuibua na kuachangia kwa kuiunga mkono hoja hiyo na nyingine zenye kufanana nayo, ilifichuka kuwa hali ya Bunge kifedha ni mbaya.

Aidha, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad, ameweka wazi kuwa hali ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NOAT) ambayo yeye ndiye mkuu wake, nayo si nzuri kifedha.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti ndiyo iliyofichua ukata unaolikabili Bunge wakati wa mjadala wa bajeti ya Ofisi Waziri Mkuu wiki juzi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Hawa Ghasia anasema kuwa katika mwaka huu wa fedha (2016/17), Mfuko wa Bunge (Fungu 42) uliidhinishiwa jumla ya Sh. bilioni 99.066 na hadi kufikia Machi 31, ulikuwa umepokea Sh. bilioni 77.479 (Sh. bilioni 59.929 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo na Sh. bilioni 17.479 kwa ajili ya mishahara).

”Hata hivyo, pamoja na kupokea fedha hizo, bado kunaonekana kuna changamoto kubwa ya kutolewa fedha kwa wakati kwa fungu husika na hivyo kuathiri utekelrezaji wa baadhi ya majukumu ya Mfuko wa Bunge,” anasema Ghasia.

Anasema hadi sasa mfuko huo una bakaa ya bajeti ya matumizi mengineyo ya kiasi cha Sh. bilioni 8.338 kulingana na bajeti iliyoidhinishwa, lakini bakaa hiyo haitoshi kutekeleza shughuli zilizobaki katika kipindi cha Aprili hadi Juni mwaka huu.

Anasema kamati yake imebaini mfuko una upungufu wa Sh. bilioni 21.196 ambao utaathiri utekelezaji wa shughuli za Bunge kwa kipindi cha robo ya nne, changamoto Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema wataitua kwa kulipatia Bunge kiasi hicho cha fedha.

Ghasia ambaye pia ni Mbunge wa Mtwara Vijijini (CCM), anasema kamati yake imethibitisha kuwapo kwa changamoto ya mgawo wa fedha kutoka Hazina kutoendana na ratiba ya shughuli za ofisi hivyo, Ofisi ya Bunge imejikuta ikiingia katika madeni ya kiasi cha Sh. bilioni 5.7 huku Spika Job Ndugai akikiri kuwa hali ni mbaya na imefikia kipindi wanachelewa kulipa mishahara na posho za wabunge.

Wakati wabunge wakilia ukata, CAG Assad naye ameweka wazi kwamba ofisi yake imeshindwa kutekeleza majukumu yake kwa wakati kutokana na kutopewa fedha na serikali.

Prof. Assad aliwaambia waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari ya Bunge mjini hapa wiki iliyopita kuwa hadi Oktoba mwaka jana, alikuwa hajapewa hata senti moja kwa ajili ya ukaguzi.

Kutokana na changamoto hiyo, Prof. Assad alisema anashindwa kufanya kazi kwa kufikia kiwango cha kitaifa na kimataifa cha ukaguzi kama inavyotakiwa licha ya kuwa na watumishi wenye ari ya kufanya kazi kwa muda mrefu.

Pia, Prof. Assad aliwaambia waaandishi wa habari mjini hapa Machi 14, kuwa anashindwa kukaa ofisini kwa utulivu kutokana na madeni makubwa ya makandarasi ambao wanajenga majengo yetu.

UTATA WA WAZIRI MPANGO

Fungu la NOAT lilikuwa miongoni mwa mafungu manne yaliyoibua mjadala mzito bungeni wakati wa vikao vya Bunge la Bajeti mwaka jana baada ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kubaini kuwa kiwango cha fedha kilichopangwa kwa ajili ya ofisi hiyo kilikuwa pungufu kwa asilimia 60 kulinganishwa na makadirio yake kwa mwaka huu wa fedha.

Mafungu mengine yaliyolalamikiwa kwa kiasi kikubwa na watunga sheria hao ni ya Mfuko wa Bunge, Mahakama na Maji.

Wakati wa mjadala wa makadirio ya bajeti ya Wizara ya Fedha na Mipango kwa mwaka huu wa fedha, Naibu Waziri Kivuli wa wizara hiyo aliliambia Bunge kuwa walibaini bajeti ya NOAT ilikuwa imefyekwa kwa asilimia 60 ikilinganishwa na makadirio ya ofisi hiyo.

Alisema ofisi hiyo iliomba kuidhinishiwa Sh. bilioni 68.839 ili itekeleze majukumu yake kwa ufanisi, lakini serikali ilitengea Sh. bilioni 32.3. Kati ya fedha hizo zilizotengwa na serikali, Sh. bilioni 28.3 ni za matumizi ya kawaida na Sh. bilioni nne ni za utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aidha, Silinde ambaye alilazimika kusoma bajeti ya upinzani kutokana na kutokuwapo bungeni kwa Waziri Kivuli wa Fedha na Mipango, Halima Mdee, alifichua kuwa mafungu ya Mahakama, Bunge na Maji yalikuwa yamefyekwa kulinganishwa na mwaka wa fedha 2015/16 na pia huku akimshukia Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango kwa madai ya kupanga bajeti bila kuzingatiwa uhalisia na umuhimu wa mafungu husika.

Hata hivyo, katika kile ambacho baadhi ya wabunge wamekuwa wakikiita 'ubishi', Dk. Mpango alikaa kuongeza mafungu hayo, uamuzi ambao madhara yake yanaonekana sasa.

Wakati Dk. Mpango alikataa kuyaongeza fedha mafungu hayo, Waziri Mkuu anasema serikali italiongeza Bunge zaidi ya Sh. bilioni 21 ambazo kimsingi ndicho kiasi cha fedha ambacho Waziri Mpango alikataa kukiongeza katika mjadala wa makadirio ya bajeti ya serikali mwaka jana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…