Gen z wapanga kuharibu nchi yao wenyewe

Tlaatlaah

JF-Expert Member
May 18, 2023
17,415
19,466
vuguvugu la mabadiliko linalochochewa na vijana hususan Africa Mashariki, yaani katika nchi za Kenya, Tanazania, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Sudani Kusini, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, limechukua sura mpya hivi sasa....

mathalani,
kuibuka kwa gen z wa Kenya kulichochewa zaidi na hali ngumu ya maisha, ikiambatana na ukosefu wa ajira, rushwa iliyokithiri, kodi, tozo na ushuru ambao uliongezwa maradufu na kuboreshwa zaidi kwenye musuada wa fedha kwa mwaka 2024/2025 kitu ambacho kiliwaunganisha vijana wa kenya bila kujali ukabila wao na kuupinga kwa maandamano ya amani, kushinikiza muswada huo tata kurekibishwa...

na hata baada ya sauti, maoni, mahitaji na matakwa yao kuskizwa,
na hatimae Rais wa Jamuhiri ya Kenya kulazimika kuufutilia mbali musuada huo muhimu wa kikatiba, na majuzi kuwafuta kazi mawaziri wake wote na kumfuta kazi mkuu wa jeshi la polisi Kenya. hivi sasa Dr. William Ruto yuko mbioni kuunda baraza ka mawaziri, huenda likawa na sura ya umoja wa kitaifa likijumuisha wapinzani na vijana....

bado gen z wanapanga kuendelea kuandamana, huku wakiibua madai mengine mapya kabisa, kama vile kumtaka na kumshinikiza Rais William Ruto, waliemchagua wenyewe kihalali kikatiba katika uchagizi mkuu wa kidemokrasia uliyofanyika Aug.2022, na kuthibitishwa na mahakama huru ya Kenya, eti aachie ngazi, dah....

kwa muda sasa muungwana,
Dr.William Ruto amekua akitoa wito kwa gen z na makundi mengine ya kisiasa, kiraia na kidini kuja pamoja katika meza ya mazungumzo, kujadili na kuamua pamoja namna bora ya kukidhi na kuboresha hali za maisha, ajira na mambo yanayolalamikiwa....

lakini wamekaidi na kudinda wito huo muhimu sana kwa umoja, utangamano, maendeleo na amani ya waKenya wote...

PLO Lumumba,
mara kwa mara amewaasa na kuwakanya wakenya katika ujumla wao kutafuta suluhu za kistaarabu na amani, katika makosa, dosari na kasoro zinazoonekana na zisizo onekana ndani na nje ya serikali yao, zinazowaathiri waKenya wote kwa ujumla wao nakutafuta suluhu ya amani...
vinginevyo hayupo atakae kua salama likitokea la kutokea,

watakao athirika, watakao umia, watakao poteza maisha, na kuirudisha kenya nyuma ni wenyewe. Ni vizuri kujizuia na ghadhabu katika kutafuta majawabu ya changamoto zinazotukabili...

Ndugu wanafamilia wenzangu wa JF,
kutoka maandamano ya amani, hadi maandamano ya uharibifu, uporaji, ghasia na mauaji, Je, kuna nguvu, ushawishi, uchochezi au ufadhili wa kisiasa nyuma yake kutoka ndani au nje ya nchi?

unadhani Dr.William Ruto atakubali kuondoka madarakani kwa maandamano tu au atajitea? unadhani nini kitatokea?
wakalenjini wanadai kusimama, kumlinda na kumchunga mtoto wao dhidi ya watakao mletea fujo, hii ina ashiria nini?

baada ya kenya ,
ni wapi vuguvugu hili la gen z linaelekea miongoni mwa nchi za Africa Mashariki :pulpTRAVOLTA:
 
vuguvugu la mabadiliko linalochochewa na vijana hususan Africa Mashariki, yaani katika nchi za Kenya, Tanazania, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Sudani Kusini, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, limechukua sura mpya hivi sasa....

mathalani,
kuibuka kwa gen z wa Kenya kulichochewa zaidi na hali ngumu ya maisha, ikiambatana na ukosefu wa ajira, rushwa iliyokithiri, kodi, tozo na ushuru ambao uliongezwa maradufu na kuboreshwa zaidi kwenye musuada wa fedha kwa mwaka 2024/2025 kitu ambacho kiliwaunganisha vijana wa kenya bila kujali ukabila wao na kuupinga kwa maandamano ya amani, kushinikiza muswada huo tata kurekibishwa...

na hata baada ya sauti, maoni, mahitaji na matakwa yao kuskizwa,
na hatimae Rais wa Jamuhiri ya Kenya kulazimika kuufutilia mbali musuada huo muhimu wa kikatiba, na majuzi kuwafuta kazi mawaziri wake wote na kumfuta kazi mkuu wa jeshi la polisi Kenya,

bado gen z wanapanga kuendelea kuandamana, huku wakiibua madai mengine mapya kabisa, kama vile kumtaka na kumshinikiza Rais William Ruto, waliemchagua wenyewe kihalali kikatiba katika uchagizi mkuu wa kidemokrasia uliyofanyika Aug.2022, na kuthibitishwa na mahakama huru ya Kenya, eti aachie ngazi, dah....

kwa muda sasa muungwana,
Dr.William Ruto amekua akitoa wito kwa gen z na makundi mengine ya kisiasa, kiraia na kidini kuja pamoja katika meza ya mazungumzo, kujadili na kuamua pamoja namna bora ya kukidhi na kuboresha hali za maisha, ajira na mambo yanayolalamikiwa....

lakini wamekaidi na kudinda wito huo muhimu sana kwa umoja, utangamano, maendeleo na amani ya waKenya wote...

PLO Lumumba,
mara kwa mara amewaasa na kuwakanya wakenya katika ujumla wao kutafuta suluhu za kistaarabu na amani, katika makosa, dosari na kasoro zinazoonekana na zisizo onekana ndani na nje ya serikali yao, zinazowaathiri waKenya wote kwa ujumla wao nakutafuta suluhu ya amani...
vinginevyo hayupo atakae kua salama likitokea la kutokea,

watakao athirika, watakao umia, watakao poteza maisha, na kuirudisha kenya nyuma ni wenyewe. Ni vizuri kujizuia na ghadhabu katika kutafuta majawabu ya changamoto zinazotukabili...

Ndugu wanafamilia wenzangu wa JF,
kutoka maandamano ya amani, hadi maandamano ya uharibifu, uporaji, ghasia na mauaji, Je, kuna nguvu, ushawishi, uchochezi au ufadhili wa kisiasa nyuma yake kutoka ndani au nje ya nchi?

unadhani Dr.William Ruto atakubali kuondoka madarakani kwa maandamano tu au atajitea? unadhani nini kitatokea?
wakalenjini wanadai kusimama, kumlinda na kumchunga mtoto wao dhidi ya watakao mletea fujo, hii ina ashiria nini?

baada ya kenya ,
ni wapi vuguvugu hili la gen z linaelekea miongoni mwa nchi za Africa Mashariki :pulpTRAVOLTA:
Naona Gen Z wakikinukisha tena baada ya wenzao kuuawa na kufungiwa kwenye viroba kisha kutupwa kwenye dampo la takataka kule Mukuru kwa Njenga-Nairobi. Hali inaweza kuja kuwa mbaya sana
 
Waache na mambo yao wenyewe wanajua wanachokifanya.
ni hatari mno aise

sina hakika kama wanajua wanachofanya na matokeo yake kwao wenyewe,

nadhani wewe unataka yatokee ili ujifunze, kujua na kuthibutisha kwamba hawakujua wanachofanya :pulpTRAVOLTA:
 
ni hatari mno aise

sina hakika kama wanajua wanachofanya na matokeo yake kwao wenyewe,

nadhani wewe unataka yatokee ili ujifunze, kujua na kuthibutisha kwamba hawakujua wanachofanya :pulpTRAVOLTA:
Ukiwasikiliza vizuri utaelewa Wanachofanya Wanakijua

Hii Dunia imeshabadilika 🐼
 
Naona Gen Z wakikinukisha tena baada ya wenzao kuuawa na kufungiwa kwenye viroba kisha kutupwa kwenye dampo la takataka kule Mukuru kwa Njenga-Nairobi. Hali inaweza kuja kuwa mbaya sana
inasikutisha sana, inauma sana....
sifahamu ni hasira za walio haribiwa na kuporwa mali zao au wana usalama?


nadhani vijana wanapaswa kujifunza kwenye hilo, ni mbaya mno...

kama maandamano haya ya tar.16 au 20, yataendeleza uporaji mali na uharibifu wa maduka ya watu zaidi ni dhahiri vifo zaidi vya mafichoni vitaendelea kugundulika.....

sasa hiyo itakua faida au hasara ya nani?:pulpTRAVOLTA:
 
Watakula shaba mpaka basi
ni hatari mbaya sana,

kwanza hata ikifikia tu hatua ya kutangaza hali ya hatari,
athari zitakua kubwa mno, achilia mbali ikifikia hatua ya kuifutilia mbali matumizi ya katiba, kisha utawala wa kijeshi kishika hatamu.

athari za vifo zotakua kubwa zaidi na hakuna atakae faidika kenya:pulpTRAVOLTA:
 
Uzi uko kimtego fulani hivi...
Anyway ni suala muda tu,,,muda wowote Uganda inaweza kutokea.
Kwetu Tanzania haiwezi kutokea hadi 2035,..
 
vuguvugu la mabadiliko linalochochewa na vijana hususan Africa Mashariki, yaani katika nchi za Kenya, Tanazania, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Sudani Kusini, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, limechukua sura mpya hivi sasa....

mathalani,
kuibuka kwa gen z wa Kenya kulichochewa zaidi na hali ngumu ya maisha, ikiambatana na ukosefu wa ajira, rushwa iliyokithiri, kodi, tozo na ushuru ambao uliongezwa maradufu na kuboreshwa zaidi kwenye musuada wa fedha kwa mwaka 2024/2025 kitu ambacho kiliwaunganisha vijana wa kenya bila kujali ukabila wao na kuupinga kwa maandamano ya amani, kushinikiza muswada huo tata kurekibishwa...

na hata baada ya sauti, maoni, mahitaji na matakwa yao kuskizwa,
na hatimae Rais wa Jamuhiri ya Kenya kulazimika kuufutilia mbali musuada huo muhimu wa kikatiba, na majuzi kuwafuta kazi mawaziri wake wote na kumfuta kazi mkuu wa jeshi la polisi Kenya. hivi sasa Dr. William Ruto yuko mbioni kuunda baraza ka mawaziri, huenda likawa na sura ya umoja wa kitaifa likijumuisha wapinzani na vijana....

bado gen z wanapanga kuendelea kuandamana, huku wakiibua madai mengine mapya kabisa, kama vile kumtaka na kumshinikiza Rais William Ruto, waliemchagua wenyewe kihalali kikatiba katika uchagizi mkuu wa kidemokrasia uliyofanyika Aug.2022, na kuthibitishwa na mahakama huru ya Kenya, eti aachie ngazi, dah....

kwa muda sasa muungwana,
Dr.William Ruto amekua akitoa wito kwa gen z na makundi mengine ya kisiasa, kiraia na kidini kuja pamoja katika meza ya mazungumzo, kujadili na kuamua pamoja namna bora ya kukidhi na kuboresha hali za maisha, ajira na mambo yanayolalamikiwa....

lakini wamekaidi na kudinda wito huo muhimu sana kwa umoja, utangamano, maendeleo na amani ya waKenya wote...

PLO Lumumba,
mara kwa mara amewaasa na kuwakanya wakenya katika ujumla wao kutafuta suluhu za kistaarabu na amani, katika makosa, dosari na kasoro zinazoonekana na zisizo onekana ndani na nje ya serikali yao, zinazowaathiri waKenya wote kwa ujumla wao nakutafuta suluhu ya amani...
vinginevyo hayupo atakae kua salama likitokea la kutokea,

watakao athirika, watakao umia, watakao poteza maisha, na kuirudisha kenya nyuma ni wenyewe. Ni vizuri kujizuia na ghadhabu katika kutafuta majawabu ya changamoto zinazotukabili...

Ndugu wanafamilia wenzangu wa JF,
kutoka maandamano ya amani, hadi maandamano ya uharibifu, uporaji, ghasia na mauaji, Je, kuna nguvu, ushawishi, uchochezi au ufadhili wa kisiasa nyuma yake kutoka ndani au nje ya nchi?

unadhani Dr.William Ruto atakubali kuondoka madarakani kwa maandamano tu au atajitea? unadhani nini kitatokea?
wakalenjini wanadai kusimama, kumlinda na kumchunga mtoto wao dhidi ya watakao mletea fujo, hii ina ashiria nini?

baada ya kenya ,
ni wapi vuguvugu hili la gen z linaelekea miongoni mwa nchi za Africa Mashariki :pulpTRAVOLTA:

Serikali ya Ruto ni halali kabisa iwajibike, ikiwezekana hata yeye mwenyewe kujiuzulu.

Maisha ya vijana wenginwaliokuwa wakiandamana kwa amani na kwa mujibu wa katiba, yamepotezwa na polisi wa Kenya. Iliwezekana vipi vijana wengi namna hiyo, kuuawa na polisi bila ya Ruto kuwa na taarifa? Alichukua hatua gani kuzuia mauaji yaliyokuwa yakifanywa na jeshi la polisi?
 
Hawa vijana wangekuja na solution sio kuandamana tu au kwanini kama wananguvu wasianzishe chama chao siasa halafu walete mabadiliko haya hata kama hawatashinda uraisi watapata wawakilishi bungeni wapiganie agenda zao. Kuandamana kutaka kumtoa mtu aliyechaguliwa kihalali sio sawa kama kuondoka basi kisheria lakini fujo sio njia ya kumtoa mtu.
 
Serikali ya Ruto ni halali kabisa iwajibike, ikiwezekana hata yeye mwenyewe kujiuzulu.

Maisha ya vijana wenginwaliokuwa wakiandamana kwa amani na kwa mujibu wa katiba, yamepotezwa na polisi wa Kenya. Iliwezekana vipi vijana wengi namna hiyo, kuuawa na polisi bila ya Ruto kuwa na taarifa? Alichukua hatua gani kuzuia mauaji yaliyokuwa yakifanywa na jeshi la polisi?
Maandamano gani ya amani? unavamia biashara za watu wanaiba, unavamia bunge wewe uachwe tu mwisho watakuja hata kwa mkeo. acheni ujinga, andamana kwa amani sawa, hutaki serikali piga kelele na njia halali za kuitoa serikali zipo. Yes wako watu waliandamana kwa nia nzuri lakini wahuni wapo pia waliingia na kuanza kuiba. Unawarushia mawe askari unategemea nini?
 
Serikali ya Ruto ni halali kabisa iwajibike, ikiwezekana hata yeye mwenyewe kujiuzulu.

Maisha ya vijana wenginwaliokuwa wakiandamana kwa amani na kwa mujibu wa katiba, yamepotezwa na polisi wa Kenya. Iliwezekana vipi vijana wengi namna hiyo, kuuawa na polisi bila ya Ruto kuwa na taarifa? Alichukua hatua gani kuzuia mauaji yaliyokuwa yakifanywa na jeshi la polisi?
kama ni hatua kwakweli Dr. Ruto amechukua vya kutosha ikiwa ni pamoja na siku ya kwanza kabisa ya maandamano tena akiwa pamoja na askofu mkuu wa kanisa Anglican Kenya Jackson Ole Sapiti kwamba amefurahi kuona vijana wamejitambua na kutambua mahitaji yao na akatoa wito na kuwaalika vijana na makundi mengine kwenye meza ya mazungmzo, wakadinda...

akakubali kuufuta muswada wa sheria amboa ndio chimbuko la maandamano...

akapunguza mshahara wake na maafisa wengine serikalini na kusitisha nyongeza ya mishahara kwa watumishi wa umma, akasitisha ununuzi wa magari mapya ya serikali, akasitisha safari na ziara za viongozi nje ya nchi, kaamuru kukata na kupunguza bajeti za idara na Taasisi za serikali....

bado akaenda mbali zaidi,
kuwafuta kazi mawaziri wake wote, haikutosha akamtimua kazi hata mkuu wa Jeshi la police Kenya,

hivi kwa usikivu na ungwana kiasi hiki ulitaka afanye nini tena, hali ya kua gen z wenyewe leo wanadai hiki kesho wanabadili wanadai kile, mpaka unajiuliza hawa vijana ni kweli wanataka hayo wanayoyapigia kelele au kuna kingine nyuma ya pazia?

ama kweli, mkataa pema pabaya pana mwita 🤭
 
Back
Top Bottom