OPEN the Door
Senior Member
- Nov 15, 2024
- 170
- 84
Freeman Aikaeli Mbowe, aka Saluti ya Zege, kwa wanasiasa wengine amekuwa mwalimu na mkufunzi wa siasa za Bongo.
Kati ya wanasiasa wengi, nadhani watamkumbuka kwa mafundisho yake. Aliwafunza wengine namna ya kuongoza.
Maneno yake, nanukuu: "Nimeongoza chama hiki kwa muda mrefu kwa josho na damu, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni."
Kweli aliwafundisha siasa wanasiasa vijana hadi chama tawala kikawaona na kuwapangia kazi, kama ukuu wa wilaya.
Huyu, FAM, namfananisha na nahodha mwaminifu ambaye ameonyesha namna ya kuendesha siasa za kidemokrasia.
Meli yake itatia nanga mnamo tarehe 21/01/2025. Bila shaka, uchaguzi ukiwa wa haki na uwazi, atakubaliana na matokeo, lakini hawa wagombea wengine nao watakubali matokeo.
Pia, nawashauri wanachama wa Chadema wasithubutu kubomoa chama kwa kuhama baada ya mshindi kupatikana. Mimi si mwanachama wa Chadema, ila napenda siasa za ushindani. Tanzania kwanza.
Kati ya wanasiasa wengi, nadhani watamkumbuka kwa mafundisho yake. Aliwafunza wengine namna ya kuongoza.
Maneno yake, nanukuu: "Nimeongoza chama hiki kwa muda mrefu kwa josho na damu, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni."
Kweli aliwafundisha siasa wanasiasa vijana hadi chama tawala kikawaona na kuwapangia kazi, kama ukuu wa wilaya.
Huyu, FAM, namfananisha na nahodha mwaminifu ambaye ameonyesha namna ya kuendesha siasa za kidemokrasia.
Meli yake itatia nanga mnamo tarehe 21/01/2025. Bila shaka, uchaguzi ukiwa wa haki na uwazi, atakubaliana na matokeo, lakini hawa wagombea wengine nao watakubali matokeo.
Pia, nawashauri wanachama wa Chadema wasithubutu kubomoa chama kwa kuhama baada ya mshindi kupatikana. Mimi si mwanachama wa Chadema, ila napenda siasa za ushindani. Tanzania kwanza.