Dodoma: Profesa Mkumbo ajivua sera ya viwanda 100 kila mkoa

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
2,203
5,609
1637174047501.jpeg

Picha: Prof. Mkumbo

Waziri wa Viwanda na Biashara, Profesa Kitila Mkumbo amesema suala la viwanda 100 kila mkoa siyo mpango wake na halipo kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Hata hivyo amesema kazi kubwa ni kusimamia ujenzi wa viwanda kila mtaa na kuanzisha ukanda maalumu wa viwanda.

Profesa Mkumbo ametoa kauli hiyo leo Novemba 17, 2021 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari uhusu miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara.

Amesema hilo halimo kwenye usimamizi wake ambao unaongozwa na Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 ambayo alishiriki kuiandika.

"Suala la viwanda 100 hilo siwezi kulisemea kwa sababu halinihusu na halipo katika mwongozo wa mambo manne ninayoyasimamia chini ya Ilani ya Uchaguzi," amesema Profesa Mkumbo.

Waziri huyo amesema hadi kufikia Julai 2021 Tanzania ilikuwa na jumla ya viwanda 80,696 vyenye uwezo wa kuajiri kati ya watu 1 kuendelea na mtaji unaoanzia Sh1 milioni.

Amesema sekta binafsi bado inaendelea kupewa nafasi kubwa ili kuwavutia wawekezaji kufurahia uwekezaji wao.


Mwananchi
 
Ni muhimu tukapata definition ya neno Kiwanda.

Enzi zile ukitaja kiwanda tunajua ni kama Mutex, Mwatex, Sunguratex, Mang’ula Machine Tools, Zana Za Kilimo Mbeya, Ubungo Farming Impements (UFI), Urafiki Textile, Kilimanjaro Machine Tools, General Tyre, Tanzania Breweries, Keko Pharmaceuticals, Magunia Morogoro, TANICA, TAMCO Kibaha, Nyumbu, Print park, TCC, Bora, etc. Viwanda hivyo vikiwa vinaajiri watu wengi. Sasa hiki kiwanda cha kuajiri mtu mmoja; sawa huenda Technolojia inasaidia lakini bado naona kiwi.

Suala la viwanda 100 kila Mkoa ilikuwa ni maono/matamanio ya Waziri Jaffo wakati huo akiwa TAMISEMI.
 
Katika hali ya kawaida hutegemei kuwa na maprofesa wajinga. Uprofesa ni kiwango cha juu kabisa katika usomi. Uanazuoni pia unatatajiwa ukupe uhuru wa nafsi na mawazo.

Lakini kwa bahati mbaya Tanzania huenda ndiyo nchi pekee ambayo ina maprofesa wajinga, maprofesa wanafiki wasiojitambua ambao hawana mbele wala nya, hakuna wanachosimamia, zaidi ya matumbo yao.

Profesa Mkumbo amekuwa Mkumbo kweli, eti Tanzania ina viwanda zaidi ya 80,000 ambavyo vingine vimeajiri mfanyakazi mmoja. Huyu inaonekana ni miongoni mwa wale maprofesa nadra Duniani, maana si rahisi sana kumpata profesa mnafiki, mwongo na mjinga.
 
Yaani viwanda 100 kwenye mkoa waziri anaviona vingi kuwa lengo gumu kufikiwa?

Mkoa unakuta una wilaya tano kila wilaya kuwa na viwanda 20 inaonekana kuwa nyumu? Wafugaji tu waweza kuwa na viwanda kibao Cha chakula Cha kuku,Cha kutotoa vifaranga ,Cha nyama,Cha viatu,no sioni ugumu sema tu waziri anabweteka tu lengo laweza fikiwa
 
Back
Top Bottom