Dhana ya kurushwa na umeme ukweli ni huu!

Transistor

JF-Expert Member
Aug 8, 2013
1,061
1,637
20241220_231740.jpg

Kurushwa na umeme ni dhana hakuna kitu kama hicho kisayansi ,ukweli ni huu hapa.

Kuna kauli umesha wahi zisikia,mtu akisema amerushwa na umeme si ndiyo..??

Mtu huyo anaweza shuhudia kabisa kuwa karushwa na umeme toka sebuleni hadi chumbani...

Basi ukweli ni huu,umeme haurushi mtu,ila umeme unaweza

1. Shika mtu na akashindwa kujitoa.

kama tu huo umeme utakua katika kiasi cha kupoozesha mfumo wake wa fahamu...mtu huyo hata jichomoa ataganda hapo hapo hadi maji yake mwilini yapungue ndo ataachiwa...

DHANA YA KURUSHWA NA UMEME.

2. Ukikuta umehisi umerushwa na umeme maana yake umeme uliingilia mifumo yako ya fahamu na ukashindwa kukushika(kukunasa,kulukausha maji),hali iliosababisha wewe kupata hitirafu ya fahamu,ya kumbukumbu ambapo ulihama mwenyewe eneo moja kwenda jingine bila kujitambua...

Fahamu kua mfumo wa fahamu wa binadamu huwasiliana kwa njia ya umeme..na ikitokea umeme wa ziada umeingia katika mwili hupelekea mfumo huo kuvurugika...

Pale binadamu anapogusa umeme bahati mbaya,ubongo wake husababisha awashe hisia za kujiokoa..

Kwakua kilichosababisha changamoto ni umeme husababisha taarifa mvurugano hupelekea mtu huyo kusahau nyakati flani ambazo alikua akijiokoa..

Hivyo kama ikitokea umegusa kifaa cha umeme sebuleni na baadae ghafla ukajikuta chumbani si kwamba umerushwa hadi huko...hapana

Ulikimbilia huko wewe mwenyewe kwa miguu yako...sema tukio lilitokea kwa haraka ukiwa katika hali ya kupoteza kumbukumbu...kutokana na mfumo wako wa fahamu kuingiliwa na umeme...

So pale kumbukumbu zitakapo kurejea utahisi umefika hapo kwa kurushwa...

Kuna mmoja alirushwa toka jikoni hadi kwa jirani....hahahah

USIKU MWEMA.

Transistor.
 
Sijaelewa vizuri hapa .

Nilimpoteza my cousin mwaka 2011 alipanda mti ambao juu ya huo mti kulikuwa na 'UMEME' (waya zinapita) alioigwa shoti Kali Sana na kusambaratishwa vibaya Sana.
Mti mbichi,au mti ambao bado upo hai ni vipitisho vya umeme,kwa mti ulio hai mizizi yake inakua imeshikana na ardhi,na ardhi ndipo Umeme au electroni hukimbilia kwa ajili ya kufanya discharge...

Umeme huhitaji ardhi kufanya Discharge ya electron zake,hivyo ikitokea kuna kitu chochote kinaweza kuzipeleka hizo electrons ardhini(Kipitisho)...basi zitapita kupitia kipitisho hicho.

Binadamu ni kipitisho,mti ni kipitisho,hivyo binadamu aliye juu ya mti anakua yeye na mti ni vipitisho vya kupeleka electrons chini.


Electrons zinapopita katika mwili wa binadamu kulingana na ukinzani husababisha joto,hivyo mtu huyo kuungua au kuishiwa maji na hivyo anaweza kufariki.

Ndiyo mana Tanesco hukata miti mirefu inayogusa waya za umeme kuzuia shoti isitokee....
 
Mti mbichi,au mti ambao bado upo hai ni vipitisho vya umeme,kwa mti ulio hai mizizi yake inakua imeshikana na ardhi,na ardhi ndipo Umeme au electroni hukimbilia kwa ajili ya kufanya discharge...

Umeme huhitaji ardhi kufanya Discharge ya electron zake,hivyo ikitokea kuna kitu chochote kinaweza kuzipeleka hizo electrons ardhini(Kipitisho)...basi zitapita kupitia kipitisho hicho.

Binadamu ni kipitisho,mti ni kipitisho,hivyo binadamu aliye juu ya mti anakua yeye na mti ni vipitisho vya kupeleka electrons chini.


Electrons zinapopita katika mwili wa binadamu kulingana na ukinzani husababisha joto,hivyo mtu huyo kuungua au kuishiwa maji na hivyo anaweza kufariki.

Ndiyo mana Tanesco hukata miti mirefu inayogusa waya za umeme kuzuia shoti isitokee....
Ndio.maana tuna vaa viatu wakati tunatembea
 
Hahaa nadhani inatakiwa iwe hivii.....Ndo maana unashauriwa uvae viatu vyenye soli pana wakati unahudumia vifaa vya umeme...

Kwenye matembezi hata peku tembea tu...hahahaha
Huna hoja ya kubishana na mimi..
Mi ni fundi mkuu nimesoma umeme miaka miwili...

Labda niulize chochote kuhusu umeme nikujibu..
Nimesoma umeme toka form 4 na nimetoka na 1 kali ya physics

Adv nimesoma PCM nimesoma umeme wa advance..
Sasa sijui unataka kunirekebisha nini hapo...
Unatanguliza neno unadhani.. mbele yangu..
 
View attachment 3181222
Kurushwa na umeme ni dhana hakuna kitu kama hicho kisayansi ,ukweli ni huu hapa.

Kuna kauli umesha wahi zisikia,mtu akisema amerushwa na umeme si ndiyo..??

Mtu huyo anaweza shuhudia kabisa kuwa karushwa na umeme toka sebuleni hadi chumbani...

Basi ukweli ni huu,umeme haurushi mtu,ila umeme unaweza

1. Shika mtu na akashindwa kujitoa.

kama tu huo umeme utakua katika kiasi cha kupoozesha mfumo wake wa fahamu...mtu huyo hata jichomoa ataganda hapo hapo hadi maji yake mwilini yapungue ndo ataachiwa...

DHANA YA KURUSHWA NA UMEME.

2. Ukikuta umehisi umerushwa na umeme maana yake umeme uliingilia mifumo yako ya fahamu na ukashindwa kukushika(kukunasa,kulukausha maji),hali iliosababisha wewe kupata hitirafu ya fahamu,ya kumbukumbu ambapo ulihama mwenyewe eneo moja kwenda jingine bila kujitambua...

Fahamu kua mfumo wa fahamu wa binadamu huwasiliana kwa njia ya umeme..na ikitokea umeme wa ziada umeingia katika mwili hupelekea mfumo huo kuvurugika...

Pale binadamu anapogusa umeme bahati mbaya,ubongo wake husababisha awashe hisia za kujiokoa..

Kwakua kilichosababisha changamoto ni umeme husababisha taarifa mvurugano hupelekea mtu huyo kusahau nyakati flani ambazo alikua akijiokoa..

Hivyo kama ikitokea umegusa kifaa cha umeme sebuleni na baadae ghafla ukajikuta chumbani si kwamba umerushwa hadi huko...hapana

Ulikimbilia huko wewe mwenyewe kwa miguu yako...sema tukio lilitokea kwa haraka ukiwa katika hali ya kupoteza kumbukumbu...kutokana na mfumo wako wa fahamu kuingiliwa na umeme...

So pale kumbukumbu zitakapo kurejea utahisi umefika hapo kwa kurushwa...

Kuna mmoja alirushwa toka jikoni hadi kwa jirani....hahahah

USIKU MWEMA.

Transiator.
Dah Kweli nimeanza Kuamini Pilau Inalevya Kabisa kabisa kabisa🤣🤣

Mkuu Kurushwa na Umeme unaita Dhana?
🤣🤣🤣

Nimewahi Kushuhudia Mtu akirushwa na Transforma Ilikuwa Chini Ilianguka Bila Kujua Masikini akalita pale alirushwa kama unavyorusha Jiwe..

Nimewah kushuhudia pia Mtu akirushwa na Nyaya Ya umeme Alipaa Mithili ya Kuku karuka Juu kakimbia kitu chini..

Shoti ya Umeme sio Dhana ni Kitu halisi na Licha ya Kurusha inaua pia Usijaribu sumu kwa kuiramba
 
Mti mbichi,au mti ambao bado upo hai ni vipitisho vya umeme,kwa mti ulio hai mizizi yake inakua imeshikana na ardhi,na ardhi ndipo Umeme au electroni hukimbilia kwa ajili ya kufanya discharge...

Umeme huhitaji ardhi kufanya Discharge ya electron zake,hivyo ikitokea kuna kitu chochote kinaweza kuzipeleka hizo electrons ardhini(Kipitisho)...basi zitapita kupitia kipitisho hicho.

Binadamu ni kipitisho,mti ni kipitisho,hivyo binadamu aliye juu ya mti anakua yeye na mti ni vipitisho vya kupeleka electrons chini.


Electrons zinapopita katika mwili wa binadamu kulingana na ukinzani husababisha joto,hivyo mtu huyo kuungua au kuishiwa maji na hivyo anaweza kufariki.

Ndiyo mana Tanesco hukata miti mirefu inayogusa waya za umeme kuzuia shoti isitokee....
Elimu nzuri Sana mkuu barikiwa .
 
Dah Kweli nimeanza Kuamini Pilau Inalevya Kabisa kabisa kabisa🤣🤣

Mkuu Kurushwa na Umeme unaita Dhana?
🤣🤣🤣

Nimewahi Kushuhudia Mtu akirushwa na Transforma Ilikuwa Chini Ilianguka Bila Kujua Masikini akalita pale alirushwa kama unavyorusha Jiwe..

Nimewah kushuhudia pia Mtu akirushwa na Nyaya Ya umeme Alipaa Mithili ya Kuku karuka Juu kakimbia kitu chini..

Shoti ya Umeme sio Dhana ni Kitu halisi na Licha ya Kurusha inaua pia Usijaribu sumu kwa kuiramba
Sawa boss...siwezi kukubishia....
Harafu hii post ya kabla ya tarehe za pilau...😀

Anyways ngoja nikusaidie.....



*Umeme haukurushi umeme una weza fanya vitu viwili vikubwa

1.Kukushikilia sababu unakua umepoozesha neva zako za fahamu hivyo huwezi jinasua...na utaachiwa tu pale maji yako mwilini yakikauka...hivyo matokeo baada ya kuachiwa unaweza ukaonekana umeungua au umekua mweusi(umekauka)..hapo kupona hua nadra

2.Umeme ukaingilia mfumo wako wa fahamu na wewe ukaweza kujinasua...sababu tu Haujawa kipitisho kizuri,au umeme ulio kuingia ulikua ule unaovuja,yaani unao zagaa hivyo hauna chanzo cha mwendelezo.

Ikitokea hivyo mara kadhaa unaweza athiri fahamu zako hivyo wakati wa kujiokoa ukahisi umerushwa.

Umeme hauna uwezo wa kukurusha ila tu kuufanya ubongo wako kutoa tahadhari ya kujiokoa,na wakati unatekeleza hilo kwa nguvu zako mwenyewe kujitoa pale utahisi umerushwa...hapa ni wewe kupitia mfumo wako wa fahamu umelitekeleza hilo tendo la kuruka.

Na utaweza kulitimiza hilo tu kama kwa bahati nzuri hujawa kipitisho kizuri au umeme ulikua ni ule wa kuvuja hauna mwendelezo....
 
Huna hoja ya kubishana na mimi..
Mi ni fundi mkuu nimesoma umeme miaka miwili...

Labda niulize chochote kuhusu umeme nikujibu..
Nimesoma umeme toka form 4 na nimetoka na 1 kali ya physics

Adv nimesoma PCM nimesoma umeme wa advance..
Sasa sijui unataka kunirekebisha nini hapo...
Unatanguliza neno unadhani.. mbele yangu..
Wala sijakubishia boss,na wala sijahitaji CV yako nilikua natania tu...

Maana jinsi ulivyo andika ilikua kama viatu viligunduliwa watu wavae sababu ikiwa ni kuogopa kupigwa shoti za umeme...just like that...
Ndio.maana tuna vaa viatu wakati tunatembea
 
Nimeandika CV ili ujue who is talking....
Kingine usitanie mtu usiyemjua sometimes is you can get harmful
Boss hasira zako ziko jirani sana aisee.......yani from no where uje umejaa kiasi hichi....

Basi nisamehe mkuu...mimi hua sijihusishi na mabishano au ugomvi wa hivi......

Nisamehe boss....wewe upo sahihi kwa kila kitu...
 
Back
Top Bottom