DC wa Kinondoni Mh Ally Salum Hapi kukagua miradi ya maendeleo leo Muungano day

Egnecious

JF-Expert Member
Jul 8, 2015
879
969
DC HAPI KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KINONDONI LEO MUUNGANO DAY

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Salum Hapi leo tarehe 26/04/2016 ambayo ni siku ya maadhimisho ya miaka 52 ya Muungano anafanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo iliyoko manispaa ya Kinondoni ambayo itazinduliwa na Mwenge.
Mh. Hapi ameagiza wakuu wa idara za uchumi, miradi, injinia wa barabara, maji na Mkurugenzi wa manispaa kufika ofisini leo tayari kwa zoezi hilo. Ziara hiyo inalenga kukagua miradi hiyo na kuona kama inalingana na thamani ya fedha iliyotajwa (value for money).
Hadi saa 1 kamili asubuhi Mkuu huyo wa wilaya alikua amewasili ofisini tayari kwa ajili ya majukumu.

Miradi inayotarajiwa kukaguliwa ni pamoja na Soko la Mburahati, ujenzi wa barabara ya Arsenal - Magoti Saranga, ujenzi wa wodi ya wazazi Ubungo, ujenzi wa hostel na kalavati Mabwepande na ujenzi wa kisima cha maji Makongo.

Huu ni muendelezo wa kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu ya Rais Dr. John Magufuli ambayo haiangalii sikukuu wala siku za mapumziko katika kuwatumikia wananchi.
 
3d765878eb1b8e299742578aebd5710e.jpg


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam Mh. Ally Hapi jana tarehe 26/4/2015 alifanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyoko manispaa ya Kinondoni. Katika ziara hiyo ambayo aliambatana na watendaji mbalimbali wa Halmashauri ya manispaa ya Kinondoni, Mh. Hapi alikagua na kupokea taarifa ya miradi mbalimbali iliyokamilika na inayoendelea kukamilika. Miradi iliyotembelewa ni kama vile
-Mradi wa ujenzi wa soko la kisasa Mburahati utakaogharimu Bilioni 1.8,
-Mradi wa ujenzi wa barabara ya Arsenal Magoti uliogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 1,
-Mradi wa ujenzi wa wodi ya wazazi Ubungo uliogharimu shilingi milioni 50,
-Ujenzi wa hostel ya wasichana katika shule ya sekondari Mabwepande utakaogharimu shilingi 283,988,270,
-Ujenzi wa Kalavati Mabwepande utakaogharimu shilingi 320,880,400,
-Ujenzi wa Kituo cha Kilimo Malolo Mabwepande utakaogharimu shilingi 96,412,200 na
-Ujenzi wa kisima cha maji Makongo utakaogharimu shilingi 240,000,000.

Akiwa katika mradi wa Kilimo Mabwepande, Mh. Mkuu wa Wilaya alivutiwa na mradi huo ambao unalenga kuweka programu ya kuwafundisha wananchi kulima mbogamboga, kufuga kuku, samaki na ng'ombe. Mh. Hapi alitoa agizo kwa Mkurugenzi kuhakikisha fedha zilizosalia kulipwa mkandarasi kiasi cha shilingi milioni 30 zilipwe haraka ili kituo kikamilike, jambo ambalo lilikubaliwa palepale.

Miradi ya maendeleo iliyokaguliwa inatarajiwa kuzinduliwa na mwenge wa uhuru ambao unatarajiwa kuwa Kinondoni katikati ya mwezi ujao.
 
35c1c68c863fd769cdea9bec0f7f4003.jpg

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam Mh. Ally Hapi jana tarehe 26/4/2015 alifanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyoko manispaa ya Kinondoni. Katika ziara hiyo ambayo aliambatana na watendaji mbalimbali wa Halmashauri ya manispaa ya Kinondoni, Mh. Hapi alikagua na kupokea taarifa ya miradi mbalimbali iliyokamilika na inayoendelea kukamilika. Miradi iliyotembelewa ni kama vile
-Mradi wa ujenzi wa soko la kisasa Mburahati utakaogharimu Bilioni 1.8,
-Mradi wa ujenzi wa barabara ya Arsenal Magoti uliogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 1,
-Mradi wa ujenzi wa wodi ya wazazi Ubungo uliogharimu shilingi milioni 50,
-Ujenzi wa hostel ya wasichana katika shule ya sekondari Mabwepande utakaogharimu shilingi 283,988,270,
-Ujenzi wa Kalavati Mabwepande utakaogharimu shilingi 320,880,400,
-Ujenzi wa Kituo cha Kilimo Malolo Mabwepande utakaogharimu shilingi 96,412,200 na
-Ujenzi wa kisima cha maji Makongo utakaogharimu shilingi 240,000,000.

Akiwa katika mradi wa Kilimo Mabwepande, Mh. Mkuu wa Wilaya alivutiwa na mradi huo ambao unalenga kuweka programu ya kuwafundisha wananchi kulima mbogamboga, kufuga kuku, samaki na ng'ombe. Mh. Hapi alitoa agizo kwa Mkurugenzi kuhakikisha fedha zilizosalia kulipwa mkandarasi kiasi cha shilingi milioni 30 zilipwe haraka ili kituo kikamilike, jambo ambalo lilikubaliwa palepale.

Miradi ya maendeleo iliyokaguliwa inatarajiwa kuzinduliwa na mwenge wa uhuru ambao unatarajiwa kuwa Kinondoni katikati ya mwezi ujao.
 
Hongera zake, ila akumbuke mshahara wa mwezi huu (bado hajaonja mshahara wa ukuu wa wilaya) anunue ata viatu vya kulingana na cheo chake, naona bado anavaa viatu vya ujana wa disco.
 
Hongera zake, ila akumbuke mshahara wa mwezi huu (bado hajaonja mshahara wa ukuu wa wilaya) anunue ata viatu vya kulingana na cheo chake, naona bado anavaa viatu vya ujana wa disco.
Mkuu huyo DC ameenda "field", unategemea avae suti na viatu vizuri hasa kipindi hiki cha mvua na matope!
 
DC HAPI KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KINONDONI LEO MUUNGANO DAY

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Salum Hapi leo tarehe 26/04/2016 ambayo ni siku ya maadhimisho ya miaka 52 ya Muungano anafanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo iliyoko manispaa ya Kinondoni ambayo itazinduliwa na Mwenge.
Mh. Hapi ameagiza wakuu wa idara za uchumi, miradi, injinia wa barabara, maji na Mkurugenzi wa manispaa kufika ofisini leo tayari kwa zoezi hilo. Ziara hiyo inalenga kukagua miradi hiyo na kuona kama inalingana na thamani ya fedha iliyotajwa (value for money).
Hadi saa 1 kamili asubuhi Mkuu huyo wa wilaya alikua amewasili ofisini tayari kwa ajili ya majukumu.

Miradi inayotarajiwa kukaguliwa ni pamoja na Soko la Mburahati, ujenzi wa barabara ya Arsenal - Magoti Saranga, ujenzi wa wodi ya wazazi Ubungo, ujenzi wa hostel na kalavati Mabwepande na ujenzi wa kisima cha maji Makongo.

Huu ni muendelezo wa kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu ya Rais Dr. John Magufuli ambayo haiangalii sikukuu wala siku za mapumziko katika kuwatumikia wananchi.


Politically formulated no weight
 
Back
Top Bottom