Pre GE2025 Chadema yamlima barua Mchome, yamtaka ajieleze ndani ya siku 14

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
May 16, 2024
2,395
6,617
Wakuu

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mkoa wa Kilimanjaro, kimemwandikia barua Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Mwanga, Lembruce Mchome kikimtaka ajieleze ndani ya siku 14 kwa nini asichukuliwe hatua za kinidhamu.

IMG_3722.jpeg

Mchome ameingia kwenye mgogoro na chama chake baada ya kuhoji uhalali wa akidi ya kikao cha Baraza Kuu ambacho kilichothibitisha uteuzi wa viongozi mbalimbali wa kitaifa.

Soma: Msajili wa Vyama vya Siasa aipa wiki moja CHADEMA ijibu barua ya Mchome

Februari 18, 2025, Mchome aliandika barua ya malalamiko kwa katibu mkuu akipinga uteuzi uliofanywa na mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu, wa viongozi wa juu wa chama na wajumbe wa kamati kuu kwenye mkutano wa Baraza Kuu Taifa uliofanyika Januari 22, 2025.

Kada huyo ambaye pia ni mjumbe wa Baraza Kuu alipeleka nakala ya barua hiyo kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na baada ya ukimya wa siku kadhaa, alikwenda kulalamika kwa Msajili, akitaka majibu ya barua yake na Msajili aliielekeza Chadema imjibu ndani ya wiki moja, kabla ya Machi 31, 2025.

Leo, Machi 26, 2025, Ofisi ya Katibu wa Chadema Kilimanjaro imemwandikia barua Mchome kwa mujibu wa katiba ya chama ya mwaka 2006 toleo la 2019, Maadili ya Viongozi 10.1(vi), 10.2 (ix) na Maadili ya Wanachama 10.3 (iii) ikimtaka maelezo.

Chanzo: Mwananchi
 
Barua yake ndio ilitangulia wajibu kwanza barua yake

Na kaandika kwa katibu mkuu wa Chadema bosi wa huyo katibu wa Kilimanjaro

Sasa huyo bosi mdogo anaingiliaje kesi iliyo mezani kwa bosi wake mnyika?
 
Barua yake ndio ilitangulia wajibu kwanza barua yake

Na kaandika kwa katibu mkuu wa Chadema bosi wa huyo katibu wa Kilimanjaro

Sasa huyo bosi mdogo anaingiliaje kesi iliyo mezani kwa bosi wake mnyika?
Msajili alikuwepo siku Ile Genge la Samia na CCM yake wakivunja Katiba.

Malissa aliohoji, Akafukuzwa uanachama bila hata kuitwa kuhojiwa ,na Tena anafukuzwa Kwa sababu tu KAHÓJI.

Vijana wa CCM mnautindio wa Ubongo??.
 
Barua yake ndio ilitangulia wajibu kwanza barua yake

Na kaandika kwa katibu mkuu wa Chadema bosi wa huyo katibu wa Kilimanjaro

Sasa huyo bosi mdogo anaingiliaje kesi iliyo mezani kwa bosi wake mnyika?
Kama kamwandikia Katibu Mkuu Chadema, kwa Msajili wa vyama ilifikaje?
 
Barua yake ndio ilitangulia wajibu kwanza barua yake

Na kaandika kwa katibu mkuu wa Chadema bosi wa huyo katibu wa Kilimanjaro

Sasa huyo bosi mdogo anaingiliaje kesi iliyo mezani kwa bosi wake mnyika?
Wewe unakipangia CHAMA cha kufanya?.
 
Jana Naibu Msajili aliwataka CHADEMA kujibu barua ya Mchome, Leo CHADEMA wanamlima barua Mchome wakitaka ajieleze.!
Tutegemee Mchome kutupwa out na chama
 
Barua yake ndio ilitangulia wajibu kwanza barua yake

Na kaandika kwa katibu mkuu wa Chadema bosi wa huyo katibu wa Kilimanjaro

Sasa huyo bosi mdogo anaingiliaje kesi iliyo mezani kwa bosi wake mnyika?
Yapo kwenye barua aliyopelekewa
 
Lisu alifanya figisu nyingi na mengine kuvunja hata katiba ya chama chake,hapa wanamsogeza kwenye kilengeo.Kwamba yeye akifanyiwa atajibu nini.Ukiona kitoto cha simba mama yuko karibu
 
Anachotakiwa kumwakilisha ni kujibu barua yake kwanza na nakala apeleke kwa msajili
Mnaoohoji ajibiwe kwanza barua yake hamfatilii jambo hili vema.Barua yaje ilishajibibiwa siku nyingi na aliambiwa na katibu mkuu aende makao makuu akafate.
 
Back
Top Bottom