Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 1,966
- 5,348
Wakuu
Baada ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, kudai kuwa chama hicho kimezuiwa kufanya mkutano wake uliopangwa kufanyika jioni ya leo, Februari 27, 2025, katika hoteli ya Sea Cliff, sasa maandalizi ya Mkutano huo Mkubwa wa chama hicho yanaendelea Makao Makuu, Mikocheni.
Updates!
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (CHADEMA), Tundu Lissu usiku huu February 27, 2025 amezindua Mkakati Maalum wa Kigitali wa CHADEMA uliopewa jina la ‘Tone Tone’ unaolenga kuhakikisha Wafuasi wa CHADEMA na Watu wengine wanakichangia Chama hicho fedha kidogodogo ambayo ikikusanywa kwa Watu wengi itakuwa nyingi na kusaidia shughuli mbalimbali za Chama.
=========================
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Fedha ya chama hicho Godbless Lema ameeleza kuwa mkakati wa Tone Tone ni mpango wa kuchangia fedha kwa chama kwa kutumia mifumo ya kidigitali ambayo utamuwezesha mtu yeyuote kuchangia kwa kutumia mitandao ya simu na malipo ya kurudia rudia.
Lema ameeleza kuwa kupitia tone tone mtu yeyote ataweza kutoa fedha kidogo aliyonayo na pale zitapounganishwa zitajaza na kufikisha kiasi ambacho kitakiwezesha chama kuweza kuendesha mikakati yake.
Aidha amefafanua kuwa watu wataweza kujiunga na mkakati huo kupitia ku-subscribe kwenye mitandao ya kijamii kama instagram, pia kuweka malipo ya kujirudia rudia(standing order) kupitia mitandao ya simu.
Mwenyekiti wa Kamati ndogo ye fedha ya CHADEMA CHADEMA ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Godbless Lema amesema wapo tayari kutumia mfumo wa sarafu za kidijitali (cryptocurrency) ili kuweza kukusanya michango ya kwenye mkakati wa Tone Tone.
Aidha Diaspora wamefanya kazi kubwa na lengo letu hadi Mwezi wa tano tufikishe Diaspora 1000 na tuna mpango wa kufungua kama NGOs kule wawe wanakatwa moja kwa moja kila mwezi, nawasihi Watu wote Nchi nzima, ‘Tonetone’ kidogokidogo “
Kaa Karibu nami kwa updates 🚨
Soma, Pia: John Heche: Walimu walipwe vizuri, wasipewe vitenge vya 'Mama' bure, haya ni matusi kwa Walimu kuvaa mabango
Baada ya Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema, kudai kuwa chama hicho kimezuiwa kufanya mkutano wake uliopangwa kufanyika jioni ya leo, Februari 27, 2025, katika hoteli ya Sea Cliff, sasa maandalizi ya Mkutano huo Mkubwa wa chama hicho yanaendelea Makao Makuu, Mikocheni.
Updates!
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (CHADEMA), Tundu Lissu usiku huu February 27, 2025 amezindua Mkakati Maalum wa Kigitali wa CHADEMA uliopewa jina la ‘Tone Tone’ unaolenga kuhakikisha Wafuasi wa CHADEMA na Watu wengine wanakichangia Chama hicho fedha kidogodogo ambayo ikikusanywa kwa Watu wengi itakuwa nyingi na kusaidia shughuli mbalimbali za Chama.
=========================
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Fedha ya chama hicho Godbless Lema ameeleza kuwa mkakati wa Tone Tone ni mpango wa kuchangia fedha kwa chama kwa kutumia mifumo ya kidigitali ambayo utamuwezesha mtu yeyuote kuchangia kwa kutumia mitandao ya simu na malipo ya kurudia rudia.
Lema ameeleza kuwa kupitia tone tone mtu yeyote ataweza kutoa fedha kidogo aliyonayo na pale zitapounganishwa zitajaza na kufikisha kiasi ambacho kitakiwezesha chama kuweza kuendesha mikakati yake.
Aidha amefafanua kuwa watu wataweza kujiunga na mkakati huo kupitia ku-subscribe kwenye mitandao ya kijamii kama instagram, pia kuweka malipo ya kujirudia rudia(standing order) kupitia mitandao ya simu.
Mwenyekiti wa Kamati ndogo ye fedha ya CHADEMA CHADEMA ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Godbless Lema amesema wapo tayari kutumia mfumo wa sarafu za kidijitali (cryptocurrency) ili kuweza kukusanya michango ya kwenye mkakati wa Tone Tone.
Aidha Diaspora wamefanya kazi kubwa na lengo letu hadi Mwezi wa tano tufikishe Diaspora 1000 na tuna mpango wa kufungua kama NGOs kule wawe wanakatwa moja kwa moja kila mwezi, nawasihi Watu wote Nchi nzima, ‘Tonetone’ kidogokidogo “
Kaa Karibu nami kwa updates 🚨
Soma, Pia: John Heche: Walimu walipwe vizuri, wasipewe vitenge vya 'Mama' bure, haya ni matusi kwa Walimu kuvaa mabango