LGE2024 CHADEMA Simiyu: Hatutaruhusu majina yaliyoongezwa katika Daftari la Wapiga Kura yapige kura na hatutasusa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

KwetuKwanza

Member
Mar 13, 2023
88
166
vlcsnap-2024-10-24-17h36m53s886.png

Juzi zoezi la andikishaji wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2024, limehitimishwa kwa serikali kujipa kongele kubwa kuwa wananchi wengi wamejiandikisha.

Sasa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Simiyu kimesema kuwa katika zoezi hilo wamegundua uwepo wa hujuma ambazo zilifanywa na wasimamizi wa uchaguzi huo.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa Wa Simiyu Mussa Onesmo anasema kuwa baada ya zoezi kumalizika, mawakala wao waliandika jumla ya idadi ya watu ambao waliandikishwa kwa siku zote pamoja na kuandika jina la mtu wa mwisho aliyeandikishwa.

…… Vituo vyote tuliweka mawakala, na siku ile ya mwisho mawakala wetu wote kila kitu walikuwa wanaandika jumla ya watu walioandikishwa, lakini pia tuliwaelekeza waandike jina la mtu wa mwisho kuandikishwa…..

Amesema kuwa baada ya zoezi kukamilika, na kesho yake majina kubandikwa, wamebaini uwepo wa hujuma kubwa kufanyika, ambapo wamekuta kuna majina mengi zaidi yameongezwa ambayo ameadai kuongezwa kinyemela na waliofanya hivyo ni wasimamizi.

Mwenyekiti huyo anasema hayo majina ni hewa na yaliongezwa usiku, kama mjama za kutaka chama Fulani kishinde. Na hizi njama wamefanya wasimamizi eti.

Namnukuu kwenye video ambayo nimeona kwenye mitandao ya kijamii Global tv online anasema…Sisi tuna takwimu zote za kila kituo, na tuna jina la mtu wa mwisho kila kituo, lakini tumekuta majina mengi zaidi hewa kwenye vituo vingi, hili tumesema hatutalikubali hata kidogo, hakuna jina hewa litapiga kura, tutapambana nao…,” anasema..

Soma Pia:
Anasema mfano mtaa wa Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi, kituo cha Gagabali hesabu ya mwisho walikuwa watu 680, lakini waliobandikwa ni 928, Kituo cha Muungano hesabu ya mwisho ni wananchi 496, lakini waliobandikwa ni 574.

Mwenyekiti huyo ametaja mitaa baadhi akisema kuwa hujuma imekuwa kubwa, ambapo alieeleza kuwa mbali na hatua nyingine, lakini chama hicho kitakata rufaa kwa mujibu wa sheria ili majina hayo yasipige kura.

Anasema …..Tunajua hizi ni hujuma za kutaka kupata ushindi kwa chama Fulani, sisi awamu hii hatutakubali na wala hatutasusia uchaguzi, tutachukua hatua zote majina hayo yasipige kura, tumeanza taratibu na kuyakatia rufaa,”..

Nimeona kwenye hiyo taarifa msimamizi wa uchaguzi ambaye ni ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Adrian Jungu, akiwataka viongozi hao kuacha kulalamika kupitia vyombo vya Habari na badala yake wapeleke malalamiko yao kwenye kamati za rufaa ili yapatiwe ufumbuzi.

“ Kanuni za uchaguzi huu ziko wazi kabisa, kuna kamati za rufaa kwenye ngazi ya kata na mitaa au vijiji, tunawaomba ambao wanalalamika wapeleke kwenye hizo kamati malalamiko yao, wasiishie kulalamika tu wapeleke hayo malalamiko kwenye sehemu husika,

Nimweka Link hapo chini wasikilize viongozi wa Chadema Mkoa wa Simiyu.


Chanzo: Global TV Online
 
Cha kushangaza zaidi, mada kama hii hata haina wachangiaji hapa ukumbini!

Kama Tanzania nzima; au hata robo tatu tu ya nchi ingekuwa na CHADEMA wa aina ya hawa wa Simiyu, hali ingekuwa ni tofauti sana na hii iliyopo sasa.
 
CCM ni chama shetani. Haitakuja kutokea hata siku moja chama hiki kije kifanye mambo yaliyo mema kwa Watanzania.
 
CCM ni chama shetani. Haitakuja kutokea hata siku moja chama hiki kije kifanye mambo yaliyo mema kwa Watanzania.
Lakini pamoja na kuujua ushetani wa cham hiki, mbona hatuoni haya yanayo fanywa na hawa CHADEMA, ambao ni kama wanautambua ushetani huo; yakionekana nchi nzima wakati huu?

Huyu shetani kawatia usingizi hata wasio penda kujihusisha naye?

Tukisikia taarifa toka kila mkoa, toka kwa CHADEMA; kama walivyo jitokeza hawa wa Simiyu, hiyo kweli haitakuwa dalili ya mwanzo kuwa "shetani" kaanza kushughulikiwa?

CCM sasa kuitwa majina hakuwastui tena, kama wanajuwa kufanya hivyo hakuwaathiri kivyovyote.
 

Juzi zoezi la andikishaji wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2024, limehitimishwa kwa serikali kujipa kongele kubwa kuwa wananchi wengi wamejiandikisha.

Sasa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Simiyu kimesema kuwa katika zoezi hilo wamegundua uwepo wa hujuma ambazo zilifanywa na wasimamizi wa uchaguzi huo.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa Wa Simiyu Mussa Onesmo anasema kuwa baada ya zoezi kumalizika, mawakala wao waliandika jumla ya idadi ya watu ambao waliandikishwa kwa siku zote pamoja na kuandika jina la mtu wa mwisho aliyeandikishwa.

…… Vituo vyote tuliweka mawakala, na siku ile ya mwisho mawakala wetu wote kila kitu walikuwa wanaandika jumla ya watu walioandikishwa, lakini pia tuliwaelekeza waandike jina la mtu wa mwisho kuandikishwa…..

Amesema kuwa baada ya zoezi kukamilika, na kesho yake majina kubandikwa, wamebaini uwepo wa hujuma kubwa kufanyika, ambapo wamekuta kuna majina mengi zaidi yameongezwa ambayo ameadai kuongezwa kinyemela na waliofanya hivyo ni wasimamizi.

Mwenyekiti huyo anasema hayo majina ni hewa na yaliongezwa usiku, kama mjama za kutaka chama Fulani kishinde. Na hizi njama wamefanya wasimamizi eti.

Namnukuu kwenye video ambayo nimeona kwenye mitandao ya kijamii Global tv online anasema…Sisi tuna takwimu zote za kila kituo, na tuna jina la mtu wa mwisho kila kituo, lakini tumekuta majina mengi zaidi hewa kwenye vituo vingi, hili tumesema hatutalikubali hata kidogo, hakuna jina hewa litapiga kura, tutapambana nao…,” anasema..

Soma Pia:
Anasema mfano mtaa wa Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi, kituo cha Gagabali hesabu ya mwisho walikuwa watu 680, lakini waliobandikwa ni 928, Kituo cha Muungano hesabu ya mwisho ni wananchi 496, lakini waliobandikwa ni 574.

Mwenyekiti huyo ametaja mitaa baadhi akisema kuwa hujuma imekuwa kubwa, ambapo alieeleza kuwa mbali na hatua nyingine, lakini chama hicho kitakata rufaa kwa mujibu wa sheria ili majina hayo yasipige kura.

Anasema …..Tunajua hizi ni hujuma za kutaka kupata ushindi kwa chama Fulani, sisi awamu hii hatutakubali na wala hatutasusia uchaguzi, tutachukua hatua zote majina hayo yasipige kura, tumeanza taratibu na kuyakatia rufaa,”..

Nimeona kwenye hiyo taarifa msimamizi wa uchaguzi ambaye ni ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Adrian Jungu, akiwataka viongozi hao kuacha kulalamika kupitia vyombo vya Habari na badala yake wapeleke malalamiko yao kwenye kamati za rufaa ili yapatiwe ufumbuzi.

“ Kanuni za uchaguzi huu ziko wazi kabisa, kuna kamati za rufaa kwenye ngazi ya kata na mitaa au vijiji, tunawaomba ambao wanalalamika wapeleke kwenye hizo kamati malalamiko yao, wasiishie kulalamika tu wapeleke hayo malalamiko kwenye sehemu husika,

Nimweka Link hapo chini wasikilize viongozi wa Chadema Mkoa wa Simiyu.


Chanzo: Global TV Online
nadhani ni vizuri ikaeleweka wazi my friends, ladies and gentlemen.

uchaguzi wa serikali za mitaa Nov27,2024, utakua wa amani sana nchi nzima. Ni matumaini ya kila mTanzania kwamba uchaguzi huo muhimu wa kihistoria utakua wa wazi, utakua wa huru na wa haki mno.

Yeyote atakajaribu kuleta fujo au ujuaji wa aina yoyote katika zoezi hilo popote nchini. hatavumiliwa hata sekunde moja. Atakabiliwa vilivyo na kudhibitiwa vizuri sana na vyombo vya ulizi na usalama na atawajibishwa ipasavyo ili iwe fundisho kwa wengine wenye mipango na nia za kuleta fujo kwenye uchaguzi huo muhimu Tanzania 🐒
 
Back
Top Bottom