UFISADI UFISADI UFISADI
VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO VIMEPAMBWA NA ULAJI KILA KONA
HIVI HII NCHI KATIKA KIPINDI KILICHOPITA HAIKUWA NA VIONGOZI???????
CHAMA TAWALA NDICHO KILICHOONGOZA UPIGAJI DILI HUU.
Haiingii akilini kabisa kuyaona na kuyasikia haya yote tunayoyasikia na kuyaona kwa macho yetu, kweli hii nchi ilikuwa ya wenyewe kama wanavyojinadi, hakuna sehemu hata moja iliyosalia kwa UFISADI
Yawezekana hata magogoni penyewe pamevimba panatakiwa kutumbuliwa,
Inashangaza sana kuona TFDA wakijikanyagakanyaga kukamata bidhaa wanazoziita feki wakati wao wenyewe ndiyo walioruhusu ziingie, huu ni uhuni na ni uuaji wa hali ya juu sana,
TPA ni donda tena donda baya kabisa, haiwezekani meli 85 ziingie na kutoka bila wao kufahamu, vyombo vya ulinzi na usalama vilikuwa wapi wakati haya yote yanatendeka???
Wakina ni ileile walikuwa wapi wakati mambo haya yanatendeka???
ATCL ni janga tena janga baya kabisa halifai hata kulitazama, ni sumu ya hatari ambayo imekuwa ikitumika kuwauwa Watanzania,
SSRA hili pia ni gonjwa la hatari sana, ni afadhali ya mgonjwa wa ukimwi au kansa kuliko hili dudu
Kuna watu wanaitwa wasomi pamoja na wanasheria wa nchi hii waliokuwa wakitumika katika ni ileile, haya yote walikuwa hawayaoni????
Au ndiyo wengi wao walikuwa wanapata vijiteni pasenti???????
Sasa hapa ndipo pazuri kweli pa kujionea hii sinema, sijui Ngosha ataanzia wapi???? Kwake mwenyewe au??????
Naziona episode nyingi kweli kwenye hii sinema, kaaaaaaaz kwelikweli.