DOKEZO Bugando Hospitali mjitafakari wagonjwa kufia mikononi mwenu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Torra Siabba

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
269
332
Ndugu zangu, hapa Mwanza tuna hospitali ya kanda ya Bugando ambayo lengo la uwepo wake ni kuokoamaisha ya Watanzania wa mikoa ya kanda ya Ziwa na mikoa jirani.

Hospitali hii inaaminika kwakua inao watumishi waliobobea kwenye kada zote, na wapo madaktari bingwa kwenye hospitali hii.

Cha kushangaza ni kwamba baadhi ya wagonjwa hufariki kwa uzembe wa kutoa huduma bora kwenye hospitali hii, mfano mwaka 2023 alifariki ndugu yangu aliyekuwa akipewa matibabu kwenye hii hospitali.

Ilikua hivi, alipelekwa bugando ijumaa na kupimwa kipimo kikubwa cha MRI baada ya kupimwa, tukaambiwa wataalamu wa kusoma majibu wako Off kwakua ni wikendi, tukaambiwa jumatatu yake angepewa majibu, isivyo bahati akafariki jumatatu asubuhi hata kabla ya majibu, na wakati wote walikua wakimpa dawa za maumivu, hivyo hii tabia ife mara moja, maana naambiwa sasa imekuwa mwendelezo, kuna mgonjwa yuko hapo tangu ijumaa anasumbuliwa na Moyo saana, mpaka leo hajapewa majibu ya vipimo Tangu ijumaa badala yake wanampa Amoxline ambazo angepata hata mtaani, huyu nae akifa sababu ya kutopewa huduma stahiki TUTASHINDWA KUVUMILIA, Serikali wekeni mkono hapa Waziri wa Afya simama kidete...
 
True. Ila kwa maoni yangu waziri wa afya yafaa awe Daktari, waziri wa sheria yafaa awe mwanasheria.

Tz waziri wa sheria mara kadhaa sio mwanasheria unajiuliza why?
Yes kwa sababu ni nafasi ya kisiasa, si ya kiufundi moja kwa moja.

Hii ina maana kwamba Rais anaweza kumteua mtu yeyote anayemuamini kuongoza wizara hiyo, hata kama hana taaluma
 
True. Ila kwa maoni yangu waziri wa afya yafaa awe Daktari, waziri wa sheria yafaa awe mwanasheria.

Tz waziri wa sheria mara kadhaa sio mwanasheria unajiuliza why?
Kama waziri WA uchumi....

Mwamba alitangaza noti mpya zenye saini yake ...


Aghastafulilah nimetoa ela Leo Kwa ATM .saini ya noti ni mpango.


Mama katufikia ila noti mpya hazijatufikia

Hivi huyu madelu yeye alisomeaga nini.mandevu au ..?
 
Ndugu zangu, hapa Mwanza tuna hospitali ya kanda ya Bugando ambayo lengo la uwepo wake ni kuokoamaisha ya Watanzania wa mikoa ya kanda ya Ziwa na mikoa jirani.

Hospitali hii inaaminika kwakua inao watumishi waliobobea kwenye kada zote, na wapo madaktari bingwa kwenye hospitali hii.

Cha kushangaza ni kwamba baadhi ya wagonjwa hufariki kwa uzembe wa kutoa huduma bora kwenye hospitali hii, mfano mwaka 2023 alifariki ndugu yangu aliyekuwa akipewa matibabu kwenye hii hospitali.

Ilikua hivi, alipelekwa bugando ijumaa na kupimwa kipimo kikubwa cha MRI baada ya kupimwa, tukaambiwa wataalamu wa kusoma majibu wako Off kwakua ni wikendi, tukaambiwa jumatatu yake angepewa majibu, isivyo bahati akafariki jumatatu asubuhi hata kabla ya majibu, na wakati wote walikua wakimpa dawa za maumivu, hivyo hii tabia ife mara moja, maana naambiwa sasa imekuwa mwendelezo, kuna mgonjwa yuko hapo tangu ijumaa anasumbuliwa na Moyo saana, mpaka leo hajapewa majibu ya vipimo Tangu ijumaa badala yake wanampa Amoxline ambazo angepata hata mtaani, huyu nae akifa sababu ya kutopewa huduma stahiki TUTASHINDWA KUVUMILIA, Serikali wekeni mkono hapa Waziri wa Afya simama kidete...

Bugando Ni moja ya Referral Hospital ambazo Ni mahili na ina wataalamu wa kutosha kabisa tofauti na unavyojaribu kueleza, wewe na Mimi hatuna mwanga wowote wakujua chanzo cha ugonjwa ulikuwa nini na naamini hiyo MRI ilikuwa Ni hatua Tu ya kusaidia kutambua tatizo kwa undani wake na sio matibabu halisi, pia tukumbuke kuwa kweli wagonjwa wote huitaji matibabu lakini sio wote Ni emergency, mfano mtu alipata ajali na kuvuja damu kwenye ubongo Ni tofauti na mtu mwenye uvimbe wa siku nyingi kwenye ubongo na plan za matibabu yatakuwa tofauti Sana
Kuhusu magonjwa kupewa Amoxicillin hapo madaktari tuwape kongole kwani waligundua tatizo moja na kuanza kulishughulikia bila kuchelewa
 
Back
Top Bottom