Benard James na somo kwa watangazaji wa vipindi vya muziki wa dansi

The August

JF-Expert Member
Oct 9, 2018
1,080
2,026
Ni jumatatu yenye hangover ya weekend. Basi lets talk about Music. Good Music.. Rhumba & seben Music.

Kutoka miaka ya 1990 jamii ya Tanzania katika anga la Burudani, muziki wa dansi (nikimaanisha Rhumba na Seben) ulishika sana hatam. Iwe ni maharusini, disco na maredioni nyimbo kama Kalay Boeing yao vijana warembo na watanashati (Wenge Musica) hadi Solola Bien miaka ya 2000 mwanzoni zilitamba sana. Miaka ya 2000 huku kwetu bendi kama Tam Tam yake Mwinjuma Muumini, Twanga Pepeta Chini ya choki na banza stone, FM Academia chini ya kina Malou stonch, Marehem ndanda kosovo kichaa, Patcho mwamba na hata stono musica na kisha kuibuka Mashujaa band. Bado nyakati hizi muziki wa dansi ulitamba sana.

Kuibuka kwa band ya Akudo miaka ya 2007 chini ya Christian Bella kuliibadilisha sana sura muziki wa dansi na kuleta ushindani mkubwa kwa Twanga na Fm Academia. Nyimbo kama Yako wapi mapenzi na Safari sio kifo, zilitikisa anga la muziki wa dansi..

Kushamiri na uwekezaji mkubwa uliofanywa na wanamuziki wa Bongo Flava. Kuliipa dhoruba kubwa muziki wa dansi. Muziki huu ukadidimia sana nchini.. Nyimbo hizi zikawa zinapigwa bar tu. Tena bar chache. Nazo bendi zilizokuwa zinapiga muziki huu ikafika mahala wakaanza kupiga kwenye mabar huku kiingilio kikiwa ni chupa ya bia tu. (HAKIKA NI NYAKATI MBAYA KABISA KATIKA MUZIKI WA DANSI).

Kuanzia mwaka jana, kumekuwa na hamasa na kampeni kubwa sana ya kuhamasisha au kuhuisha muziki wa dansi.

Kampeni hii imehusisha maeneo makubwa hasa matatu.

Moja, ni kutoa kwa nyimbo mpya. Katika eneo hili, mwaka juzi baada ya gawanyiko la band ya FM Academia, Rais Patcho mwamba alianzisha band yake. Bamd hii iitwayo Bogoss Musica ilizinduliwa mwaka jana na kutoa wimbo ulio maarufu kabisa na kuleta sura mpya muziki wa dansi.



Band hii ilikuwa na 75 % sura na damu mpya katika muziki wa dansi. Mathalani mwanamuziki Kelly Hustle naye mwaka huu akaachia nyimbo mpya iitwayo Come Back.



Bado mwaka jana na huu umeshuhudia utoaji wa nyimbo mpya kadhaa.

Mkali Jimmy Manzaka baada ya kutoka na Coco Chanel...

..

Siku kadhaa ameachia nyimbo hii iitwayo Chozi langu..



Papii kocha naye akishirikiana na bwana mdogo mwenye sauti ya kipekee, Melody mbasa nao wakatoa nyimbo iitwayo upepo.. Nayo ni rhumba yenye vionjo vilivyopikwa kiufundi haswa.



Ukiwa mkoani Arusha, unaweza pata muziki mzuri wa band kutoka bendi iitwayo Mjengoni classic band.

Hakika muitikio wa kutoa nyimbo mpya umekuwa ni mkubwa.

Hatua ya pili ni uchezwaji wa nyimbo hizi kwenye vyombo vya habari.

Ni hatua ya kupongezwa kuwa muitikio sio mbaya.. Wapo watangazaji wengi wamefanya vyema kuupigania muziki huu.

Mathalani.

Sunday mwakanosya na Ben Kinyaiya katika Channel Ten na Magic fm wanaufanyia haki muziki huu.

Dakota de lavida a.k.a Abdacadabra huwezi acha thamini mchango wake. Kipindi cha Mama land cha Clouds TV na pia weekend bonanza cha Clouds FM. Pia ana program yake ya Buzuki Time ambayo anafanya kipindi kutokea bar fulani. Hii inaweka ufaham mtaani juu ya kipindi na muziki wa dansi.

Irene Gabriel. Mwanadada huyu kupitia radio uhuru hakika anawapa nafasi muziki wa dansi.

Zuhuru mwinyi yuko active na mwepesi kutoa nafasi kwa wanamuziki wa dansi.

Benard James.. Kwa upekee kabisa, Ben james amastahili pongezi na pia somo moja kutoka kwake napenda watangazaji wengine wamuige. Anafanya vipindi viwili maarufu sana. Anaongoza kipindi kiitwacho Afrika kabisa kupitia kituo cha Star Tv na Tanzania Stars cha RFA. Jambo moja la kipekee ni kanuni yake ni kucheza kwa 95% nyimbo mpya tu katika vipindi vyake.

Hii inatoa nafasi kwa nyimbo mpya kucheza, hamasa kwa watu kutoa nyimbo, na muhimu kabisa kuutangaza muziki huu.

Ni ajabu kukuta kipindi cha muziki wa dansi unasikia nyimbo za kina Gato, Tabu Ley, Fally ipupa Associe, Fere Gola Mercure, FM Academia Vuta N kuvute. Hakika njia hii haikuzi muziki kabisa.

Kwa hili ninaomba sana watangazaji wa muziki wa dansi, tuige kanuni hii ya Ben James, hakika itakuza sana muziki wetu huu dansi, kwani ni hakika hujawahi sikia kipindi cha XXL nyimbo zinazopigwa humo ni Wachuja Nafaka, Monduli Mobb, Hard Blasters Crew au Watu Pori.

Asanteni.
0.jpeg


Cc rogaroga GENTAMYCINE
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakatafute na wahenga wa kuwajaza ukumbini! Kila zama na mambo yake! Ilikuwa Taarab ikaja bend na sasa ni zama za kina Aslay!
Hayo mabendi yatuburudishe tu tukiwa bar tunalamba kvant zetu na kiingilio kibaki kuwa ni bia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakatafute na wahenga wa kuwajaza ukumbini! Kila zama na mambo yake! Ilikuwa Taarab ikaja bend na sasa ni zama za kina Aslay!
Hayo mabendi yatuburudishe tu tukiwa bar tunalamba kvant zetu na kiingilio kibaki kuwa ni bia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kiingilio kikiwa bia, je hawa waimbaji watapata faida gani? Ikumbukwe kuendesha band ni gharama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi binafsi nyimbo za sasa za ki congo hata sizielewi kabisa!!! Ila zile za miaka ya 1990's ndio nazipenda sana, pepe kale, ghato, kofi olomide, madilu, defao, wenge bcbg, bongoman, nyiboma, zinanikosha sana, lakini ya kizazi hiki bado kabisa, bora hata za mzee mzima kofi olomide.
 
Mimi binafsi nyimbo za sasa za ki congo hata sizielewi kabisa!!! Ila zile za miaka ya 1990's ndio nazipenda sana, pepe kale, ghato, kofi olomide, madilu, defao, wenge bcbg, bongoman, nyiboma, zinanikosha sana, lakini ya kizazi hiki bado kabisa, bora hata za mzee mzima kofi olomide.
Naomba usikilize hii, japo si ya kicongo kisha ipe Rating out of 5.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
*Fahamu Ratiba ya Vipindi vya Dansi kwa watu wa Media*

*GOLDEN*
*- TBC (Nyumbani ni Nyumbani)*, Jumatatu saa 11:00 – 12:00 jioni.

*IRENE GABRIEL*
*- Uhuru Fm (Ambiance Shituka),* Jumamosi na Jumapili Saa 10:00 – 11:00 jioni

*DJ CON*
*- E-fm (Afropower)* Jumamosi 8:00 mchana -10:00 jioni

*RAJABU ZOMBOKO*
*- Redio One (Afrotz)* Jumatatu, Jumanne, Jumatano na Alhamisi 4:00– 7:00 usiku.

*KHAMISI DACOTA )*
*- Clouds (Weekend Bonanza)* Jumamosi 4:00 – 7:00 usiku
*- Clouds TV (Mama Land)* Jumapili 11:00 jioni

*BERNAD JAMES*
*- Redio Free Africa (Tanzania Stars),* Jumamosi 4:05 – 5:00
*- Star TV (Afrika Kabisa)* Alhamisi 11.30 jioni

*MC PETIT -Times Fm*
*(Dansi na Baninga)*
Jumapili 1:00 jioni -2:00 Usiku

*MASTER E*
*- Rasi Fm Dodoma, (Afro Dance)*, Jumamosi na Jumapili 11:00 jioni - 2:00 usiku

*FURAHISHA/MR MBEYA*
*- Highland Fm Mbeya, (Africa leo),* Jumapili 11.00 Jioni - 2:00 usiku

*MWAKAMZIMA*
*- Jembe Fm, (Saturday Express)* Jumamosi 1:00 jioni 3:00 Usiku

*ZUHURA MWINYI*
*- Maisha Fm Dodoma, (Africa Mobimba)* Ijumaa -Jumapili Saa 10:00 - 12:00 Jioni

*MKUBWA DALE*
*- Tanga FM (Bantu Beat),* Jumatatu - Ijumaa 2:00 - 4:00 Usiku

*SUNDAY MWAKANOSYA*
*- Channel Ten (Afro Dance)*, Jumamosi saa 6:00 usiku Jumapili saa 6:00 usiku
*- Magic Fm (Afro Bongo)*, Jumatatu saa 4 Asubuhi, Jumanne 11:30 Alfajiri, Jumatano saa 3:30 Asubuhi, Ijumaa saa 10:00 Jioni na saa 5:00 usiku

*MWINYIAMI MAFTAH 'Stazo'*
*-Magic FM (Zilipendwa) Jumapili

*JOHN KITIME*
*- E FM* (Zilipendwa) Jumapili

*DJ MACKEY*
*- East Africa FM* (Zilipendwa) Jumamosi

*ADAM ZUBERI*
*- Uhai FM* *(Saturday Rhumba)* Jumamosi 3:00 - 6:00 Usiku
*(Sunday Rhumba)* Jumapili 3:00 - 5:00 Asubuhi

*BARAKA SUNGA*

*- Sunrise Radio* *(Afrika Mambo)* Jumatatu- Alhamisi 10:15 Alasiri - 1:00 Usiku
*Tuzikumbuke* Ijumaa 10:15 Alasiri - 1:00 Usiku

**********
*WAANDISHI WA MAGAZETI*

*JONATHAN TITO NA CHRISTOPHA MSEKENA*
*- (Gazeti la Bingwa),* Kila Jumanne usikose *Habari za Dansi*

*RHOBI CHACHA*
*- Gazeti la Mwanaspoti*
Jumapili, Jumatatu na Alhamisi *(Habari za Dansi)*

- Gazeti la *Mwananchi*, kila siku *(Habari za Dansi)*

*- MCL Digital, (MCL Extra)*, Ijumaa, Jumamosi 7:00 Mchana.
*NB: Kwa upande wa online kila siku na muda wowote habari za dansi zinapandishwa.*

*TAARIFA*
Hawa ni baadhi ya wanahabari waliokuwepo kwenye Magroup ya whatsApp ya Dansi. Kama kuna mtu nimemwacha na yuko kwa group aweke jina lake na kipindi chake pamoja na muda.

Kazi kwenu wanamuziki nimewarahisishia kujua media zinazofanya muziki ili iwe rahisi kupeleka kazi zenu na msiwe na akili ya redio moja tu ndio inayofanya muziki wa dansi pekee .

Na kwa upande wa wadau wa dansi kufahamu siku ya kupata burudani kwenye media.

*Imetaharishwa* na
*Rhobi Chacha*
*Mwandishi na mdau wa muziki wa Dansi.*



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uzi mkali wewe kweli mpenzi wa muziki wa dansi, hapo kwa Rajab Zomboko wa Radio 1 pia Ijumaa kipindi cha HIZI NAZO kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 7 mchana
 
Back
Top Bottom