Bashe kaletwa kututoa kwenye reli suala la utekaji na mauaji ya watu wasiyojulika pamoja na kesi ya afande, tusitoke kwenye reli

Cute Wife

JF-Expert Member
Nov 17, 2023
1,857
4,866
Wakuu Salaam,

Mtakuwa mmekutana na vijembe kvya Bashe na Mpina, tena naye kaanza kutumia vichambo kibasaaa, na Millard eti kaweka kaweka kichwa cha kimbea, soma hapa - Hussein Bashe: Luhaga Mpina uwe na shukrani kwa serikali, chezea sekta nyingine sio kilimo

Hapa anajua lazima Watanzania watahama kwenda kwenye jambo lingine na kuachana na mambo ya kudai uchuguzi ili wasiyojulikana wajulikane na afande pamoja na wale askari wengine waliofanyia ukatili binti iende kimya kimya.

Yaani muda wote huo aliokuwa nao wa kujibu tuhuma za Mpina jana ndio kaona aongee, tena siyo hata kwa kutuambia cha maana! Jamani tusidanganywe kiboya hivi.

Watanzania tusitoke kwenye reli, tushikilie hapa hapa, leo wametekekwa na kuuliwa ambao hawakugusi moja kwa moja kesho atatekwa na kuuliwa unayekuhusu usage meno.

Huu ndio muda wa kudai uwajibikaji na kurudisha mamlaka kwa wananchi kama inavyotakiwa, wakati ni sasa.
 
Ikitoka connection ya mdada mweupe mwenye msambwanda mkubwa unaong'ara. Watu watasahau kila kitu 🤣🤣
 
Kweli kabisa hapa jioni utaona press release toka Kizimkazi upepo utageuka watu wataanza kumjadili Bashe sasa na kusahau move ya utekaji hovyo
 
Back
Top Bottom