Baba ajinyonga baada ya kumuua mwanaye

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
55,887
29,210
Watu wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti likiwemo la baba kumuua mtoto wake mwenye umri wa miaka mitatu kisha na yeye kujinyonga.

Akizungumza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa, amesema tukio hilo limetokea Julai 28 mwaka huu katika kijiji cha Sayaka wilayani Magu ambapo mtuhumiwa ambaye pia ni marehemu kwa sasa Kisumo Emmanuel (38) alimuua mtoto wake huyo kisha kuuutupa mwili wa mtoto huyo kwenye kisima cha maji.

Kwa mjibu wa Kamanda Mutafungwa mwanaume huyo alifikia uamzi huo baada ya kumtuhumu mkewe kuzaa watoto na wanaume wengine.

Kamanda Mutafungwa amesema baada ya tukio hilo baba huyo alijinyonga kwa kutumia kipande cha shuka alichokifunga kwenye mti umbali wa kilomita moja kutoka nyumbani kwake.

"Kabla ya tukio hilo la mauaji Julai 26 baba huyo alimpokea mtoto wake aitwaye Lukonys Kisumo kutoka kwa mama ambaye jina linahifadhiwa kwa sababu za kiusalama na Julai 28 ndipo alipopata nafasi ya kuongozana na mtoto huyo umbali wa mita 500 kutoka nyumbani kwake na kutekekeleza mauaji hayo,"amesema DCP Mutafungwa.

Furaha FM
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Sofia Jongo amesema kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo linamshikilia Flora Maplo (33), mkazi wa Kitongoji cha Amrima, Kata ya Rwamgasa, kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wake mwenye umri wa miezi miwili.

Mtoto huyo anadaiwa kuuawa kwa kunyongwa shingo na kukatwa mkono wa kulia na mguu wa kulia kisha mwili kutelekezwa njiani.

Kamanda Jongo alisema tukio hilo lilitokea Julai 22, mwaka huu, katika kitongoji cha Mienze, wilayani Bukombe.

#furahafmupdates #hizininyakatizafuraha
 
Wanawake wamezidi kuwasingizia wanaume watoto.... Na kwa hal hii mauaji hayataishaaa
Kuna page Moja ya mahusiano IG wanawake wanatoa shuhuda huko Hadi unabaki kushangaa. Wanaume wengi mnalea watoto sio wenu ni basi mengine Acha yasisemwe.
 
Chanzo kikuu cha hayo mauaji ni jamaa kubambikiwa mtoto ambaye sio wake,si support mauaji aliyoyafanya ila kwenye tukio ni lazima tuangalie chanzo cha tukio na sio matokeo baada ya tukio.
 
Mutafungwa kwamakosa kama hayo ikiwa mtu atabainika...
Napia naiomba serikali ichukue hatua kali sana kwawanao chochea au kueneza matukio ya mauaji.
 
Hiki ni kichaa inakuwaje unamuua malaika mtoto ambaye hana Hata hatia?Kama umejua kuwa mtoto sio wako si achaneni tu?Kwanini uue na kujiua?maisha yenyewe mafupi usijipe stress za bure kuoana Sio kifungo songa mbele maisha mengine yaendelee.
 
Itungwe sheria,kila mtoto anayezaliwa apimwe DNA TEST ili kuthibitisha kua mtoto ni wa Mume halali,

Najua hii italeta tabu kwenye familia nyingi ila itafanya wanawake walio olewa kua makini na kuacha kubambikia waume zao watoto ambao sio wao.
 
Watu wawili wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti likiwemo la baba kumuua mtoto wake mwenye umri wa miaka mitatu kisha na yeye kujinyonga.

Akizungumza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Wilbroad Mutafungwa, amesema tukio hilo limetokea Julai 28 mwaka huu katika kijiji cha Sayaka wilayani Magu ambapo mtuhumiwa ambaye pia ni marehemu kwa sasa Kisumo Emmanuel (38) alimuua mtoto wake huyo kisha kuuutupa mwili wa mtoto huyo kwenye kisima cha maji.

Kwa mjibu wa Kamanda Mutafungwa mwanaume huyo alifikia uamzi huo baada ya kumtuhumu mkewe kuzaa watoto na wanaume wengine.

Kamanda Mutafungwa amesema baada ya tukio hilo baba huyo alijinyonga kwa kutumia kipande cha shuka alichokifunga kwenye mti umbali wa kilomita moja kutoka nyumbani kwake.

"Kabla ya tukio hilo la mauaji Julai 26 baba huyo alimpokea mtoto wake aitwaye Lukonys Kisumo kutoka kwa mama ambaye jina linahifadhiwa kwa sababu za kiusalama na Julai 28 ndipo alipopata nafasi ya kuongozana na mtoto huyo umbali wa mita 500 kutoka nyumbani kwake na kutekekeleza mauaji hayo,"amesema DCP Mutafungwa.

Furaha FM
Itungwe sheria,kila mtoto anayezaliwa apimwe DNA TEST ili kuthibitisha kua mtoto ni wa Mume halali,

Najua hii italeta tabu kwenye familia nyingi ila itafanya wanawake walio olewa kua makini na kuacha kubambikia waume zao watoto ambao sio wao.
Absolutely true.

DNA Test iwe ni sharti la lazima kwa wazazi wa mtoto mara tu anapozaliwa.

Hii itakuwa suluhisho la tatizo la usaliti katika ndoa na janga la kubambikia Wanaume watoto wasiokuwa wao.
 
Back
Top Bottom