LGE2024 Baada ya kupuuza Ule msemo wa jinsi ya kula na kipofu, Leo wanatafutwa wananchi wa kujiandikisha Kwa tochi ili kura ziibwe!

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Rabbon

JF-Expert Member
Apr 16, 2022
21,190
33,095
Salaam, shalom!!

Viongozi tulikuwa tukiwaonya kupunguza viburi, mlikuwa mkitamba Kwa kauli za kejeli kuwa " Hata msipoipigia CCCM kura Bado itaunda Serekali"

Wengine wakaenda mbali na kudai kuwa " CCM kamwe haitatoka madarakani Hadi ipende yenyewe kama ambavyo Pascal Mayalla amekuwa akidai,

Viongozi wetu mkashindwa kujua kuwa kauli zenu ni sawa na kumshika mkono kipofu wakati mnamwibia chakula chake,

Matokeo ya kauli zenu, wananchi wamestuka, wamesusa,wamepuuza wamekaa pembeni.

Sasa Kuna Ile KANUNI ya ushindi wa mazingira, kuwa, wakijitokeza wapiga kura waliojiandikisha, unaongeza na za wizi Ili ionekane chama kimeshinda Kwa HAKI,

Sasa watu hawajiandikishi, wamegoma, mtaiba kura zipi ilhali watu hawajitokezi!!

Sasa uhalali wa kuongoza utatoka wapi ikiwa wananchi wamegoma kushiriki chaguzi sababu ya wizi na viburi vyenu?

Suluhu pekee iliyobaki mbeleni ni kubadili mgombea wa nafasi ya juu kuliko zote Ili angalau Nchi ipumue, chama kiendelee kuwepo japo Kwa miaka 10 ijayo, tofauti na hapo, yajayo...

Wana chi Si wajinga, mkae mkijua Hilo.

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿.

Karibuni 🙏
 
Kituko, uhamasishaji unafanyika mpaka makanisani wananchi wakajiandikishe. Cha ajabu wahamasishaji ni viongozi wa ccm kata, wilaya, mkoa wanaingia makanisani na kusema wametumwa na ngazi za juu kuja kuhamasisha uandikishaji huku wengine wakiwa wamevaa sare zao za kijani. Cha ajabu zaidi wanatoa sadaka nzuri tu hata kama watakuta muda wa kutoa sadaka umepita. Wakishatoa sadaka wanatoka mbio kuwahi kanisa jingine kabla hawajatoka ibadani. Kwa sasa wanawafuata wananchi majumbani mwao kuwaandikisha kwa kuwabembeleza. Wananchi wanawakubalia kuandikishwa japo wanasema hawataenda kupiga kura, hawana muda huo wa kupoteza shughuli zao
 
Serikali hii ni ya kipuuuzi sana! Mpk kwenye misiba mtu anakurupuka huko anatoa tangazo la kuhamasisha watu kujiandikisha! Pumbavu sana!
 
Hili zoezi la uandikishaji wapiga kura linaenda mwendo wa konokono, kasi ni ndogo mno inabidi zibuniwe mbinu zingine kupata waliojiandikisha wawe wengi kama kuingia mitaani kwa wananchi majumbani mwao na kwenye shughuli zao tena kwa kuwabembeleza. Nimeingia kituo kimoja kujiandikisha nikakuta mwandikishaji amelala usingizi hana cha kuandika. Hakuna foleni, fasta nikaandiishwa chini ya dakika tano nikatoka bila kuona wa nyuma yangu anayekuja kuandikishwa. Tusubiri vituko zaidi wakati wa kupiga kura na kutoa matokeo
 
Nchi inaongozwa na wasio uwezo. Mkuu tunza huo tushahidi utasaidia siku za usoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…