Baada ya kuona Rais wa Uturuki anaitamani sana Syria, Benjamin Netanyahu aizibia njia Uturuki

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
9,321
14,826
Netanyahu kama alivyo mwenzake Donald Trump akili zao si za kawaida.Wanajiamini kuwachokoza na kutaka kupigana na kila mtu duniani kwa kujiamini kwa hali ya juu.

Hiyo ni kwa vile Israel kwa sasa imeridhika kuwa waarabu wote ni kama maboya tu.Sasa hivi wamejiamini kuichokonoa Uturuki ambapo hapo jana jeshi la Israel liliendelea kupiga maeneo kadhaa ya Syria hasa hasa zilizokuwa kambi za jeshi za Bashar Al Assad.Njia za kufikia kambi hizo zimebomolewa na makombora kutoka angani ili Uturuki isiweze kuzifikia na kuzitumia.

Israel inafanya hivyo huku ikijua kuwa yenyewe inachukua maeneo ya nchi hiyo na ambayo yapo chini ya makatazo ya maazimio ya Umoja wa mataifa.Imekuwa ikitoa amri kwa watawala wapya wa Syria kutopeleka vikosi vyake maeneo mengi ya kusini mpaka kusini ya mji mkuu wa nchi hiyo.

Inashangaza sana akili za Netanyahu na Trump zilivyo na ambazo zinawachokoza mataifa na kila mtu.Kile wanachopenda wakipate na wanachofanya wao huwa hawapendi wengine wavipate wala kufanya kama wanavyopenda hata kama ni haki na viko chini ya mamlaka zao.
 
Netanyahu kama alivyo mwenzake Donald Trump akili zao si za kawaida.Wanajiamini kuwachokoza na kutaka kupigana na kila mtu duniani kwa kujiamini kwa hali ya juu.

Hiyo ni kwa vile Israel kwa sasa imeridhika kuwa waarabu wote ni kama maboya tu.Sasa hivi wamejiamini kuichokonoa Uturuki ambapo hapo jana jeshi la Israel liliendelea kupiga maeneo kadhaa ya Syria hasa hasa zilizokuwa kambi za jeshi za Bashar Al Assad.Njia za kufikia kambi hizo zimebomolewa na makombora kutoka angani ili Uturuki isiweze kuzifikia na kuzitumia.

Israel inafanya hivyo huku ikijua kuwa yenyewe inachukua maeneo ya nchi hiyo na ambayo yapo chini ya makatazo ya maazimio ya Umoja wa mataifa.Imekuwa ikitoa amri kwa watawala wapya wa Syria kutopeleka vikosi vyake maeneo mengi ya kusini mpaka kusini ya mji mkuu wa nchi hiyo.

Inashangaza sana akili za Netanyahu na Trump zilivyo na ambazo zinawachokoza mataifa na kila mtu.Kile wanachopenda wakipate na wanachofanya wao huwa hawapendi wengine wavipate wala kufanya kama wanavyopenda hata kama ni haki na viko chini ya mamlaka zao.
Moderator kaweka kichwa cha habari kwa matamanio yake..Kilichokuwepo kabla kilikuwa ni bora zaidi.
 
Uturuki ibinywe tu, inataka kuwa na ushawishi mashariki ya kati na kuwa tishio kwa Israel. Israel ichukue hatu za kujilinda na majirani zake wengi wao wakiwa ni maadui zake
ukiwa ni binadamu usiwe jeuri kiasi hicho.Wenzako watakuchoka na kukutafutia mbinu.
Si maumbile ya binadamu kukubali kutawaliwa na kuendeshwa na binadamu mwenzake.
 
Israel inayo sababu za kujilinda dhidi ya maadui zao. Uturuki idhibitiwe isiweze kujipenyeza huko mashariki ya kati
Kwani mashariki ya kati ipo kwa ajili yao pekee kwamba wengine wote wasikaribie.
Wanajidanganya
 
Hapo uturuki itabondwa na NATO itakaa kimya.Huyo mwanachama mpya wa NATO hana sifa ya kuwa mwanachama, atanyukwa na hatapata usaidizi toka ulaya na amerika
 
Back
Top Bottom