JOYOPAPASI
JF-Expert Member
- Jan 10, 2016
- 250
- 409
UKWELI AMBAO WANANCHI WENGI WANAUTAMBUA CHINI YA SERIKALI YA AWAMU YA 5.
Katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Tano wananchi wameweza kuyaona mambo ambayo awakuyatarajia yafanyike ndani ya muda wa miaka 5 pekee. Mambo hayo yanayo washangaza wengi ni pamoja na yafuatayo:
SEKTA YA MAJI
1. Wananchi wa maeneo ya Chalinze, Ubena Zomozi, hadi Bwawani wote walikuwa hawana maji ya kunywa na kuteseka sana kwa shida ya maji licha ya kuwepo kwa mradi wa maji wa wami ambao ulikuwa kama mapambo tu. Leo hii wananchi walewale walio teseka miaka yote wanapata maji chini ya Serikali ya awamu ya tano.
2. Wananchi wa Makurunge, Fukayosi, hadi Kiwangwa Wilayani Bagamoyo wameteseka miaka yote lakini ndani ya miaka 5 ya Serikali ya Awamu ya Tano wanapelekewa mradi mkubwa wa maji kutoka chanzo cha maji cha Ruvu chini.
3. Wananchi wa Kisarawe toka Wilaya ya Kisarawe ilipoanzishwa mwaka 1907 walikuwa hawajawahi kuona maji ya bomba licha ya mto Ruvu kupita ndani ya Wilaya yao lakini ndani ya kipindi kifupi cha Serikali ya Awamu ya Tano wananchi hao wameona muujiza wa kupata maji ya bomba.
4. Wananchi wa Mkuranga miaka yote wameteseka lakini ndani ya muda mfupi wa Serikali ya Awamu ya Tano wanapata maji ambayo ambayo ayakuwepo kabisa katika ndoto zao.
5. Jiji la DSM lilikiwa na uhaba mkubwa wa maji ambapo kuna maeneo kulisambazwa mabomba kwa muda mrefu maarufu kwa jina la mabomba ya Mchina lakini Serikali ya Awamu ya Tano imewezesha kupatikana kwa maji mengi ya kutosha kutoka chanzo cha Ruvu juu na Ruvu chini hivyo kuyafanya mabomba hayo na maeneo mengine kuweza kupata maji ya kutosha kwasasa.
6. Kupitia visima virefu vya Kimbiji na Mipera vinakwenda kuondoa kabisa shida ya maji kwa wakazi wa Kigamboni, Mbagala, na Maeneo ya Wilaya ya Mkuranga kupitia mradi mkubwa unao tekelezwa na DAWASA.
7. Wakazi wa Simanjiro wameteseka miaka yote lakini ndani ya miaka 5 mradi kubwa wa maji hadi Olkesmet umekamilika
8. Wakazi wa Korogwe , Same, hadi Mwanga wanakamilishiwa mradi mkubwa wa maji wa kihistoria katika Wilaya hizo tatu.
9. Jiji la Arusha limenufaika na mradi mkubwa wa maji wa zaidi ya shilingi bilion 520
10. Mradi kubwa wa maji unao endelea kutoka Ziwa Victoria ambapo wakazi wa Nzega,Igunga, Tabora, hadi Sikonge wanapatiwa maki kwa mradi unao gharimu Dola za Kimarekani milion 268.35 (zaidi ya shilingi bilion 600 pesa za Kitanzania)
11. Miradi mikubwa ya maji kwa maeneo ya Lamadi, Bukoba, Kigoma, Lindi, Longido, na maeneo mengi nchini imekuwa ukombozi kwa wananchi ambayo yote inatekelezwa chini ya serikali ya Awamu ya Tano.
SEKTA YA ELIMU
1. Serikali imeweza kuwawezesha watoto wa ki-Tanzania kupata elimu bila kubaguliwa kwa kuwawezesha utoaji wa zaidi ya shilingi bilion 23.86 kila mwezi hivyo kuwawezesha hata watoto wa kutoka familia masikini kuweza kupata elimu
2. Utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu
3. Zoezi kubwa la Ukarabati wa shule zote 89 Kongwe hapa nchini ambapo shuleni 73 tayari zimekamika na shule 16 zilizobaki zinaendelea na hatua mbalimbali za maboresho
4. Ujenzi wa mabweni, mabwalo, madarasa, matundunya vyoo, na nyumba za walimu unaendelea Nchi nzima kwa shule za msingi na Sekondari. Na kwasasa serikali imepeleka zaidi ya shilingi bilion 170 kwaajili ujenzi wa miundombinu mipya katika shule za msingi na Sekondari
5. Kila Afisa Elimu mkoa (REO) amepewa gari jipya kwaajili ya kusimamia elimu hapa nchini
6. Waratibu elimu kata (WEO) wamepewa pikipiki mpya kila mmoja kwaajili ya kusimamia elimu katika shule zao ndani ya Kata wanazo zisimamia
7. Taratibu za manunuzi ya magari kwa maafisa Elimu (DEO) wa Wilaya zote unakamilika
8. Vifaa vya maabara vimenunuliwa na kusambazwa kwa lengo la kuwajengea vijana uwezo wa kusoma kivitendo masomo ya sayansi
9. Zaidi ya walimu elfu 21 wa shule za msingi na Sekondari wameajiriwa na kusambazwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini
10. Hosteli nyingi za wanafunzi pamoja na majengo ya maktaba, maabara, na vyumba vya midahalo vimejengwa katika vyuo mbalimbali hapa nchini vikiwemo Chuo Kikuu cha DSM, SUA, MUST, Mkwawa, na vyuo vingine vya umma.
11. Kuongezeka kwa kiwango cha fedha za mikopo pamoja na wanufaika wa mikopo, n.k
SEKTA YA AFYA
Katika Sekta ambayo imefanyiwa mapinduzi makubwa hapa nchini ndani ya miaka 5 ni Sekta ya Afya. Mafanikio yaliyo patikana ni kama ifuatavyo:
1. Ujenzi wa vituo vya Afya 487 vyenye uwezo wa kufanya huduma ya upasuaji ikilinganishwa na vituo vya Afya 115 vilivyokuwa na uwezo wa kufanya huduma ya upasuaji mwaka 2015.
2. Ujenzi wa hospitali mpya 99 za Wilaya ikilinganishwa na hospitali 77 za serikali tulizokuwa nazo kabla ya serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani. Ikumbukwe kwamba serikali ya Awamu ya Tano ilianza kujenga hospitali mpya 67 za wilaya na sasa imeongeza ujenzi wa hospitali zingine 32 mpya na hivyo kuweka historia ya kipekee hapa nchini katika uimarishaji wa Sekta ya Afya hapa nchini.
3. Ujenzi wa hospitali za rufaa na hospitali za kanda zaidi ya 11 hapa nchini
4. Upelekeaji wa dawa na vifaa tiba ambapo bajeti yake imeongezeka kutoka bilion 31 kwa mwaka 2015 hadi bilion 270 kwasasa
5. Usambazaji wa magari ya wagonjwa
6. Ongezeko la watumishi kwani zaidi ya watumishi elfu 12 wameajiriwa na kusambazwa katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma ya afya.
Juhudi hizi zilizofanywa na Rais DKT. JOHN POMBE MAGUFULI zimesaidia kuokoa maisha ya kinamama mengi wajawazito pamoja na watoto kwani ikumbukwe wananchi wengi walikuwa wanazifuata huduma mbali sana wengine walikuwa wanasafiri zaidi ya kilometa 140 kufuata huduma ya upasuaji pindi mama mjamzito anaposhindwa kujifungua kwa njia ya kawaida.
UBORESHAJI WA MIJI YETU
Katika kipindi cha miaka 5 tumeshuhudia uboreshaji wa hali ya juu katika miji yetu hapa nchini. Zaidi ya shilingi Trilion 2.1 zinatumika. Tumeshuhudia Jiji la DSM, Tanga, Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma, Manispaa zote, na halmashauri za miji yote ikifanyiwa mapinduzi makubwa. Mambo makubwa yaliyo fanyika ndani ya kipindi hiki cha miaka 5 ni pamoja na yafuatayo;
1. Ujenzi wa mtandao wa barabara za Lami za kisasa zaidi zilizowekwa mataa
2. Ujenzi wa mifereji ya kusafirishia maji
3. Ujenzi wa standi za Kisasa na masomo ya kisasa zaidi
4. Ujenzi wa madampo ya Kisasa na ununuzi wa mitambo ya kuzolea taka
5. Miji yote imeandalia Master Plan ikilinganishwa na hapo awali
UJENZI WA MIUNDOMBINU
Tanzania inashuhudia mapinduzi makubwa sana kwasasa. Ujenzi wa barabara za Lami kila eneo unaendelea. Miongoni mwa miradi mikubwa inayo endelea ni pamoja na
1. Ujenzi wa barabara ya Mpanda hadi Tabora, Mpanda kwenda Kigoma, Tabora kwenda Kigoma, Kigoma kwenda Nyakanazi.
2. Ujenzi wa barabara ya Mbinga kwenda Bambabay na Tabora kwenda Itigi.
3. Kukamilishwa kwa barabara ya Iringa kwenda Dodoma, Dodoma kwenda Babati
4. Ujenzi wa barabara katika mikoa yote hapa nchini
5. Ujenzi wa barabara 8 ya Ubungo hadi Kibaha
6. Upanuzi wa barabara ya mwenge, Mwanza kati kwenda airport, Iringa kwemda Mbeya.
7. Ujenzi wa madaraja makubwa yakiwemo Thibiti, Kilombero, Nyerere, Magala, Tanzanite, na daraja la Busisi-Kigongo, daraja la Mfugale, na njia za juu za Ubungo.
8. Upanuzi wa bandari za DSM, Tanga, Mtwara, Kigoma na bandari zingine katika maziwa yetu
9. Ununuzi wa ndege mpya 11 kwa fedha za watanzania
10. Ujenzi wa meli mpya na ukarabati wa meli kadhaa pamoja na ujenzi na ukarabati wa vivuko vingi
Ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege vikiwemo DSM Terminal III, Tabora, Mtwara, Katavi, Dodoma, na Mwanza
11. Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR kutoka DSM hadi Makotopora Wilayani Manyoni ambapo zaidi ya shilingi Trilion 7 zinatumika.
12. Ujenzi wa mradi mkubwa wa Umeme wa Nyerere ambapo zaidi ya shilingi Trilion 6.5 fedha za walipa kodi wa Tanzania zinatumika. Mradi utakao zalisha Megawat 2115 ikilinganushwa MW.1560 tunazo zalisha sasa.
13. Upanuzi wa Kinyerezi 1 na Kinyerezi 2
14. Vijiji vyenye umeme vimeongezeka kutoka wastani wa vijiji 2000 kwa mwaka 2015 hadi zaidi ya vijiji 9000 hadi Juni, 2020.
MAKUSANYO YA SERIKALI
Kama mnavyo fahamu serikali yetu hadi mwaka 2015 tulikuwa tunakusanya wastani wa shilingi bilion 800 kwa mwezi. Lakini kwasasa makusanyo yameweza kuimarika kufikia wastan wa shilingi trillion 1.5 kwa mwezi. Makusanyo haya yameweza kuelekezwa katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali kama ilivyo elezwa hapo juu ili kukuza Uchumi wa Nchi yetu. Kwasasa Nchi yetu imepata heshima kwa kuingia katika nchi ya Uchumi wa kipato cha kati(wa hali ya chini) kama ilivyo ainishwa na Bank ya Dunia mnamo tarehe 01 July, 2020. Kinacho takiwa kwasasa ni kwakila Mtanzania kuchapa kazi ili pato letu lizidi kuongezeka kwa kufikia Nchi yenye Uchimi wa Kipato cha kati ulio imarika.
Haya ni baadhi ya mambo mengi yaliyo fanyika ndani ya miaka 5 ambayo mengine kwa Sekta za Utalii, Viwanda, Mifugo, Uvuvi, Sanaa, na Utamaduni ambayo ni mengi zaidi ambayo sikuweza kuyaeleza hapa.
Safari hii yenye kutia matumaini makubwa ni safari ya watanzania wote. Tunapaswa kuungana na maono makubwa ya Rais wetu ambaye amejipambanua katika kuwatumikia wananchi kwa moyo wake wote.
Mungu akubariki sana Rais wetu DR. JOHN POMBE MAGUFULI


Mungu tubariki watanzania

Katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Tano wananchi wameweza kuyaona mambo ambayo awakuyatarajia yafanyike ndani ya muda wa miaka 5 pekee. Mambo hayo yanayo washangaza wengi ni pamoja na yafuatayo:
SEKTA YA MAJI
1. Wananchi wa maeneo ya Chalinze, Ubena Zomozi, hadi Bwawani wote walikuwa hawana maji ya kunywa na kuteseka sana kwa shida ya maji licha ya kuwepo kwa mradi wa maji wa wami ambao ulikuwa kama mapambo tu. Leo hii wananchi walewale walio teseka miaka yote wanapata maji chini ya Serikali ya awamu ya tano.
2. Wananchi wa Makurunge, Fukayosi, hadi Kiwangwa Wilayani Bagamoyo wameteseka miaka yote lakini ndani ya miaka 5 ya Serikali ya Awamu ya Tano wanapelekewa mradi mkubwa wa maji kutoka chanzo cha maji cha Ruvu chini.
3. Wananchi wa Kisarawe toka Wilaya ya Kisarawe ilipoanzishwa mwaka 1907 walikuwa hawajawahi kuona maji ya bomba licha ya mto Ruvu kupita ndani ya Wilaya yao lakini ndani ya kipindi kifupi cha Serikali ya Awamu ya Tano wananchi hao wameona muujiza wa kupata maji ya bomba.
4. Wananchi wa Mkuranga miaka yote wameteseka lakini ndani ya muda mfupi wa Serikali ya Awamu ya Tano wanapata maji ambayo ambayo ayakuwepo kabisa katika ndoto zao.
5. Jiji la DSM lilikiwa na uhaba mkubwa wa maji ambapo kuna maeneo kulisambazwa mabomba kwa muda mrefu maarufu kwa jina la mabomba ya Mchina lakini Serikali ya Awamu ya Tano imewezesha kupatikana kwa maji mengi ya kutosha kutoka chanzo cha Ruvu juu na Ruvu chini hivyo kuyafanya mabomba hayo na maeneo mengine kuweza kupata maji ya kutosha kwasasa.
6. Kupitia visima virefu vya Kimbiji na Mipera vinakwenda kuondoa kabisa shida ya maji kwa wakazi wa Kigamboni, Mbagala, na Maeneo ya Wilaya ya Mkuranga kupitia mradi mkubwa unao tekelezwa na DAWASA.
7. Wakazi wa Simanjiro wameteseka miaka yote lakini ndani ya miaka 5 mradi kubwa wa maji hadi Olkesmet umekamilika
8. Wakazi wa Korogwe , Same, hadi Mwanga wanakamilishiwa mradi mkubwa wa maji wa kihistoria katika Wilaya hizo tatu.
9. Jiji la Arusha limenufaika na mradi mkubwa wa maji wa zaidi ya shilingi bilion 520
10. Mradi kubwa wa maji unao endelea kutoka Ziwa Victoria ambapo wakazi wa Nzega,Igunga, Tabora, hadi Sikonge wanapatiwa maki kwa mradi unao gharimu Dola za Kimarekani milion 268.35 (zaidi ya shilingi bilion 600 pesa za Kitanzania)
11. Miradi mikubwa ya maji kwa maeneo ya Lamadi, Bukoba, Kigoma, Lindi, Longido, na maeneo mengi nchini imekuwa ukombozi kwa wananchi ambayo yote inatekelezwa chini ya serikali ya Awamu ya Tano.
SEKTA YA ELIMU
1. Serikali imeweza kuwawezesha watoto wa ki-Tanzania kupata elimu bila kubaguliwa kwa kuwawezesha utoaji wa zaidi ya shilingi bilion 23.86 kila mwezi hivyo kuwawezesha hata watoto wa kutoka familia masikini kuweza kupata elimu
2. Utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa Elimu ya juu
3. Zoezi kubwa la Ukarabati wa shule zote 89 Kongwe hapa nchini ambapo shuleni 73 tayari zimekamika na shule 16 zilizobaki zinaendelea na hatua mbalimbali za maboresho
4. Ujenzi wa mabweni, mabwalo, madarasa, matundunya vyoo, na nyumba za walimu unaendelea Nchi nzima kwa shule za msingi na Sekondari. Na kwasasa serikali imepeleka zaidi ya shilingi bilion 170 kwaajili ujenzi wa miundombinu mipya katika shule za msingi na Sekondari
5. Kila Afisa Elimu mkoa (REO) amepewa gari jipya kwaajili ya kusimamia elimu hapa nchini
6. Waratibu elimu kata (WEO) wamepewa pikipiki mpya kila mmoja kwaajili ya kusimamia elimu katika shule zao ndani ya Kata wanazo zisimamia
7. Taratibu za manunuzi ya magari kwa maafisa Elimu (DEO) wa Wilaya zote unakamilika
8. Vifaa vya maabara vimenunuliwa na kusambazwa kwa lengo la kuwajengea vijana uwezo wa kusoma kivitendo masomo ya sayansi
9. Zaidi ya walimu elfu 21 wa shule za msingi na Sekondari wameajiriwa na kusambazwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini
10. Hosteli nyingi za wanafunzi pamoja na majengo ya maktaba, maabara, na vyumba vya midahalo vimejengwa katika vyuo mbalimbali hapa nchini vikiwemo Chuo Kikuu cha DSM, SUA, MUST, Mkwawa, na vyuo vingine vya umma.
11. Kuongezeka kwa kiwango cha fedha za mikopo pamoja na wanufaika wa mikopo, n.k
SEKTA YA AFYA
Katika Sekta ambayo imefanyiwa mapinduzi makubwa hapa nchini ndani ya miaka 5 ni Sekta ya Afya. Mafanikio yaliyo patikana ni kama ifuatavyo:
1. Ujenzi wa vituo vya Afya 487 vyenye uwezo wa kufanya huduma ya upasuaji ikilinganishwa na vituo vya Afya 115 vilivyokuwa na uwezo wa kufanya huduma ya upasuaji mwaka 2015.
2. Ujenzi wa hospitali mpya 99 za Wilaya ikilinganishwa na hospitali 77 za serikali tulizokuwa nazo kabla ya serikali ya awamu ya tano kuingia madarakani. Ikumbukwe kwamba serikali ya Awamu ya Tano ilianza kujenga hospitali mpya 67 za wilaya na sasa imeongeza ujenzi wa hospitali zingine 32 mpya na hivyo kuweka historia ya kipekee hapa nchini katika uimarishaji wa Sekta ya Afya hapa nchini.
3. Ujenzi wa hospitali za rufaa na hospitali za kanda zaidi ya 11 hapa nchini
4. Upelekeaji wa dawa na vifaa tiba ambapo bajeti yake imeongezeka kutoka bilion 31 kwa mwaka 2015 hadi bilion 270 kwasasa
5. Usambazaji wa magari ya wagonjwa
6. Ongezeko la watumishi kwani zaidi ya watumishi elfu 12 wameajiriwa na kusambazwa katika vituo mbalimbali vya kutolea huduma ya afya.
Juhudi hizi zilizofanywa na Rais DKT. JOHN POMBE MAGUFULI zimesaidia kuokoa maisha ya kinamama mengi wajawazito pamoja na watoto kwani ikumbukwe wananchi wengi walikuwa wanazifuata huduma mbali sana wengine walikuwa wanasafiri zaidi ya kilometa 140 kufuata huduma ya upasuaji pindi mama mjamzito anaposhindwa kujifungua kwa njia ya kawaida.
UBORESHAJI WA MIJI YETU
Katika kipindi cha miaka 5 tumeshuhudia uboreshaji wa hali ya juu katika miji yetu hapa nchini. Zaidi ya shilingi Trilion 2.1 zinatumika. Tumeshuhudia Jiji la DSM, Tanga, Mwanza, Arusha, Mbeya, Dodoma, Manispaa zote, na halmashauri za miji yote ikifanyiwa mapinduzi makubwa. Mambo makubwa yaliyo fanyika ndani ya kipindi hiki cha miaka 5 ni pamoja na yafuatayo;
1. Ujenzi wa mtandao wa barabara za Lami za kisasa zaidi zilizowekwa mataa
2. Ujenzi wa mifereji ya kusafirishia maji
3. Ujenzi wa standi za Kisasa na masomo ya kisasa zaidi
4. Ujenzi wa madampo ya Kisasa na ununuzi wa mitambo ya kuzolea taka
5. Miji yote imeandalia Master Plan ikilinganishwa na hapo awali
UJENZI WA MIUNDOMBINU
Tanzania inashuhudia mapinduzi makubwa sana kwasasa. Ujenzi wa barabara za Lami kila eneo unaendelea. Miongoni mwa miradi mikubwa inayo endelea ni pamoja na
1. Ujenzi wa barabara ya Mpanda hadi Tabora, Mpanda kwenda Kigoma, Tabora kwenda Kigoma, Kigoma kwenda Nyakanazi.
2. Ujenzi wa barabara ya Mbinga kwenda Bambabay na Tabora kwenda Itigi.
3. Kukamilishwa kwa barabara ya Iringa kwenda Dodoma, Dodoma kwenda Babati
4. Ujenzi wa barabara katika mikoa yote hapa nchini
5. Ujenzi wa barabara 8 ya Ubungo hadi Kibaha
6. Upanuzi wa barabara ya mwenge, Mwanza kati kwenda airport, Iringa kwemda Mbeya.
7. Ujenzi wa madaraja makubwa yakiwemo Thibiti, Kilombero, Nyerere, Magala, Tanzanite, na daraja la Busisi-Kigongo, daraja la Mfugale, na njia za juu za Ubungo.
8. Upanuzi wa bandari za DSM, Tanga, Mtwara, Kigoma na bandari zingine katika maziwa yetu
9. Ununuzi wa ndege mpya 11 kwa fedha za watanzania
10. Ujenzi wa meli mpya na ukarabati wa meli kadhaa pamoja na ujenzi na ukarabati wa vivuko vingi
Ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege vikiwemo DSM Terminal III, Tabora, Mtwara, Katavi, Dodoma, na Mwanza
11. Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR kutoka DSM hadi Makotopora Wilayani Manyoni ambapo zaidi ya shilingi Trilion 7 zinatumika.
12. Ujenzi wa mradi mkubwa wa Umeme wa Nyerere ambapo zaidi ya shilingi Trilion 6.5 fedha za walipa kodi wa Tanzania zinatumika. Mradi utakao zalisha Megawat 2115 ikilinganushwa MW.1560 tunazo zalisha sasa.
13. Upanuzi wa Kinyerezi 1 na Kinyerezi 2
14. Vijiji vyenye umeme vimeongezeka kutoka wastani wa vijiji 2000 kwa mwaka 2015 hadi zaidi ya vijiji 9000 hadi Juni, 2020.
MAKUSANYO YA SERIKALI
Kama mnavyo fahamu serikali yetu hadi mwaka 2015 tulikuwa tunakusanya wastani wa shilingi bilion 800 kwa mwezi. Lakini kwasasa makusanyo yameweza kuimarika kufikia wastan wa shilingi trillion 1.5 kwa mwezi. Makusanyo haya yameweza kuelekezwa katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali kama ilivyo elezwa hapo juu ili kukuza Uchumi wa Nchi yetu. Kwasasa Nchi yetu imepata heshima kwa kuingia katika nchi ya Uchumi wa kipato cha kati(wa hali ya chini) kama ilivyo ainishwa na Bank ya Dunia mnamo tarehe 01 July, 2020. Kinacho takiwa kwasasa ni kwakila Mtanzania kuchapa kazi ili pato letu lizidi kuongezeka kwa kufikia Nchi yenye Uchimi wa Kipato cha kati ulio imarika.
Haya ni baadhi ya mambo mengi yaliyo fanyika ndani ya miaka 5 ambayo mengine kwa Sekta za Utalii, Viwanda, Mifugo, Uvuvi, Sanaa, na Utamaduni ambayo ni mengi zaidi ambayo sikuweza kuyaeleza hapa.
Safari hii yenye kutia matumaini makubwa ni safari ya watanzania wote. Tunapaswa kuungana na maono makubwa ya Rais wetu ambaye amejipambanua katika kuwatumikia wananchi kwa moyo wake wote.
Mungu akubariki sana Rais wetu DR. JOHN POMBE MAGUFULI



Mungu tubariki watanzania


