Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 29,488
- 31,528
KKKT Ina MKUU MMOJA TU
Naona KKKT imepamba moto kutokana na matamshi ya mmoja wa Maaskofu wake. Kwa kimbelembele nilicho nacho naomba umma wa watanzania uelewe yafuatayo:
1. KKKT ina Mkuu mmoja tu. Dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja.
2. KKKT hakuna cheo kinaitwa “Mkuu wa Kanisa Mstaafu”. Tunaweza kuwa na cheo cha “Aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa”. Hivi sasa tuna “aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa” ambaye amechaguliwa tena Mkuu wa Kanisa. Kama angekuwa Mstaafu asingechaguliwa. Inawezekana “aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa” akachaguliwa kuwa Mkuu tena. Sitashangaa aliyepita hivi karibuni, kuchaguliwa tena.
3. Kama kuna mstaafu, ASTAAFU. Si lazima kuhudhuria; si lazima kusema. Ukipenda, usipende kwa niaba. Ukichukia, usichukie kwa niaba. Kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe,
4. KKKT ni shirikisho, siyo kanisa moja. Ukitaka kusema kwa niaba ya shirikisho, unashawishi siyo kuburuza, Hatujashawishika na hatujakaa.
5. Nampenda rais Samia, lakini sijatumwa na kanisa. Naweza kumpenda na kukikosoa chama chake. Naweza kukipenda chama chake nikamkosoa yeye. Hayo nitayasemea Karagwe siyo penginepo. Na nikiyasema, ni yangu na tumbo langu; siyo ya Wanyambo wala Walutheri walio wenye vyama vyao. Wanyambo haturuhusu mgeni kupiga mluzi katika nyumba ya mwenyeji.
6. Kanisa lina wanachama wa vyama vyote na waumini wasio na vyama. Chadema msitutolee macho na CCM msishangilie. Shoka lipo shinani, mti usiozaa matunda unakatwa.
7. Rais Samia ana uwezo wa kujiharibia. Tusimharibie. CCM ina uwezo kujiharibia; haijaomba msaada wa kuisaidia kuharibu. Lipo kundi linalodhani linamsaidia rais Samia, wakati linamharibia. Lipo linalodhani linamharibia lakini linamjenga. Anayesimama na HAKI anamsaidia rais Samia.
8. Tuna tatizo kitaifa: Kuna watu wanatumia dini kueneza siasa. Na kuna watu wanatumia siasa kueneza dini. Mimi si mmoja wa hao wawili. Mimi natumia ujinga kueneza dini na siasa. Wajinga tu, ndio wananisikiliza na kunifuata. Wewe mjuaji kaa pembeni tuendelee na safari.
9. Nikisema jambo mkanishangilia, mnanipa kiburi cha kusema bila kufikiri.
Nidhamu ya washangiliaji huja kwa kutafakari; si kuhemuka. Mkishangilia, mnamnyima msemaji nidhamu ya kufikiri kabla ya kusema. Anayesema kweli hahitaji kukumbuka alisema nini jana.
10. Mungu analipenda Taifa hili kuliko mtu au chama chochote kinavyoweza kudai kulipenda. Usiombe Mungu akuonyeshe anavyolipenda hili taifa. Ina gharama nzito kushuhudia Mungu anavyolipenda hili taifa.
Hata anayerudi nyuma ana mbele anakoelekea. Ukisifiwa kuwa na mbio, jihadhari usipitilize nyumbani kwenu.
Source: FB page yake
Pia soma
Naona KKKT imepamba moto kutokana na matamshi ya mmoja wa Maaskofu wake. Kwa kimbelembele nilicho nacho naomba umma wa watanzania uelewe yafuatayo:
1. KKKT ina Mkuu mmoja tu. Dereva wawili hawawezi kuendesha gari moja kwa wakati mmoja.
2. KKKT hakuna cheo kinaitwa “Mkuu wa Kanisa Mstaafu”. Tunaweza kuwa na cheo cha “Aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa”. Hivi sasa tuna “aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa” ambaye amechaguliwa tena Mkuu wa Kanisa. Kama angekuwa Mstaafu asingechaguliwa. Inawezekana “aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa” akachaguliwa kuwa Mkuu tena. Sitashangaa aliyepita hivi karibuni, kuchaguliwa tena.
3. Kama kuna mstaafu, ASTAAFU. Si lazima kuhudhuria; si lazima kusema. Ukipenda, usipende kwa niaba. Ukichukia, usichukie kwa niaba. Kila ulimi una uwezo wa kuonja wenyewe,
4. KKKT ni shirikisho, siyo kanisa moja. Ukitaka kusema kwa niaba ya shirikisho, unashawishi siyo kuburuza, Hatujashawishika na hatujakaa.
5. Nampenda rais Samia, lakini sijatumwa na kanisa. Naweza kumpenda na kukikosoa chama chake. Naweza kukipenda chama chake nikamkosoa yeye. Hayo nitayasemea Karagwe siyo penginepo. Na nikiyasema, ni yangu na tumbo langu; siyo ya Wanyambo wala Walutheri walio wenye vyama vyao. Wanyambo haturuhusu mgeni kupiga mluzi katika nyumba ya mwenyeji.
6. Kanisa lina wanachama wa vyama vyote na waumini wasio na vyama. Chadema msitutolee macho na CCM msishangilie. Shoka lipo shinani, mti usiozaa matunda unakatwa.
7. Rais Samia ana uwezo wa kujiharibia. Tusimharibie. CCM ina uwezo kujiharibia; haijaomba msaada wa kuisaidia kuharibu. Lipo kundi linalodhani linamsaidia rais Samia, wakati linamharibia. Lipo linalodhani linamharibia lakini linamjenga. Anayesimama na HAKI anamsaidia rais Samia.
8. Tuna tatizo kitaifa: Kuna watu wanatumia dini kueneza siasa. Na kuna watu wanatumia siasa kueneza dini. Mimi si mmoja wa hao wawili. Mimi natumia ujinga kueneza dini na siasa. Wajinga tu, ndio wananisikiliza na kunifuata. Wewe mjuaji kaa pembeni tuendelee na safari.
9. Nikisema jambo mkanishangilia, mnanipa kiburi cha kusema bila kufikiri.
Nidhamu ya washangiliaji huja kwa kutafakari; si kuhemuka. Mkishangilia, mnamnyima msemaji nidhamu ya kufikiri kabla ya kusema. Anayesema kweli hahitaji kukumbuka alisema nini jana.
10. Mungu analipenda Taifa hili kuliko mtu au chama chochote kinavyoweza kudai kulipenda. Usiombe Mungu akuonyeshe anavyolipenda hili taifa. Ina gharama nzito kushuhudia Mungu anavyolipenda hili taifa.
Hata anayerudi nyuma ana mbele anakoelekea. Ukisifiwa kuwa na mbio, jihadhari usipitilize nyumbani kwenu.
Source: FB page yake
Pia soma